huyu alisema aesh alisema wazi kuwa kikwete ni MUNGU, yeye ni YESU KRISTO, na yule DIwanini ROHO MTAKATIFU, sasa mahakama imetengua ushindi wa YESU KRISTO!!!!!!!
laana hizi za kujiita Mungu zitawatafuna wote watatu, kwa kuwa sijamsikia kikwete akikana kuwa yeye si MUNGU kama alivyotajwa huko Sumbawanga, ni wakati muafaka wa yeye kukataa hili
"Wewe unauliza, lakini unajua ni nani aliyetoa kauli ya kukata rufani? Tamko la kukata rufani ilitolewa na yeye au chama? Kuuliza wapi tumefikia, muulize yeye. Yeye asingeweza kukata rufani bila kuwasiliana na uongozi," alisema Nape.
Aidha Nape, alipohojiwa juu ya hatua iliyofikiwa ya ukusanyaji ushahidi wa tetesi za ufisadi kwa baadhi ya makada wa chama hicho wakiwamo wabunge, unaofanywa na kamati ya maadili ya CCM, alisema kwa sasa hawako kwenye nafasi ya kutoa taarifa ya kamati hiyo.
Mwigulu na Nape wapo Nkinga Igunga leo nielekezeni namna ya kupost niwaletee habari kamili.Hapo kwenye red majibu
yanaonyesha kuna kafrustration flani hasa baada ya CDM kumpeleka kwa
Pilato. Ila pia kanikumbusha mbali sana enzi zile unaomba pocket money
kwa Mdingi halafu hana hela, utakula majibu ya hasira, ha ha
haaaa!!!!!
Uchaguzi Sumbawanga Mjini,
unanukia baada ya muda wa kukata rufani kwa mujibu wa sheria za uchaguzi
kupita na upande wa mrufani kugubikwa na ukimya.
Katibu wa CCM (itikadi na uenezi), Nape Nnauye, alipotakiwa kuzungumzia
msimamo wa chama kuhusiana na rufani hiyo, alisema aliyekuwa mbunge wa
jimbo hilo, Aeshi Hilaly, asingeweza kukata rufani bila kuwasiliana na
uongozi.
Nape pia, aliongeza kuwa suala la kukata rufani lilitolewa na Aeshi na
sio chama ambapo alimtaka mwandishi wa gazeti hili kuwasiliana na
mhusika (Aeshi), iwapo anataka kujua hatma ya kauli hiyo.
Wewe unauliza, lakini unajua ni nani aliyetoa kauli ya kukata rufani?
Tamko la kukata rufani ilitolewa na yeye au chama? Kuuliza wapi
tumefikia, muulize yeye. Yeye asingeweza kukata rufani bila kuwasiliana
na uongozi, alisema Nape.
Aidha Nape, alipohojiwa juu ya hatua iliyofikiwa ya ukusanyaji ushahidi
wa tetesi za ufisadi kwa baadhi ya makada wa chama hicho wakiwamo
wabunge, unaofanywa na kamati ya maadili ya CCM, alisema kwa sasa hawako
kwenye nafasi ya kutoa taarifa ya kamati hiyo.
NIPASHE ilipozungumza na Aeshi jana alisema; Nimekiachia chama, ni muda
mrefu umepita nasubiri majibu. Mimi si msemaji wa chama, nasubiri kukaa
na chama ndipo niweze kueleza, maana hata hivyo siwezi kujua kama wewe
kweli ni mwandishi wa NIPASHE au la, alisema Aeshi.
Kwa upande mwingine, NIPASHE ilimtafuta Naibu Spika, Job Ndugai, kujua
kama Bunge limeshapeleka taarifa kwa Tume ya Uchaguzi Nchini (NEC)
kwamba jimbo hilo liko wazi baada ya muda wa kukata rufani kupita
kisheria, alisema:
Tutalitolea maelezo Oktoba kwenye mkutano ujao wa Bunge. Hatuna
uhakikika, tunataka kujiridhisha kwanza kwa mahakama ili tuweze
kulitolea maelezo suala hilo kwenye Bunge lijalo.
Aprili 30 mwaka huu, Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga
ilitangaza kuenguliwa kwa ubunge wa Aeshi (CCM), baada ya kushindwa
katika kesi iliyokuwa inamkabili ya ushindi wake uliodaiwa kugubikwa na
utata dhidi ya aliyekuwa mgombea mwenzake Norbert Yamsebo (Chadema)
katika Jimbo la Sumbawanga Mjini, Oktoba, 2010.
Katika uchaguzi huo, Aeshi alishinda kwa zaidi ya kura 17, 328 dhidi ya
Yamsebo aliyepapata kura17,132.
Kesi hiyo namba 01 ya mwaka 2010 ilifunguliwa na Yamsebo.
Uamuzi wa kutengua matokeo hayo ulitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama
Kuu Kanda ya Mbeya, Bethwell Mmilla, ambaye alisikiliza kesi hiyo na
kuisoma kwa takribani saa matatu.
CHANZO: NIPASHE
huyu alisema aesh alisema wazi kuwa kikwete ni MUNGU, yeye ni YESU KRISTO, na yule DIwanini ROHO MTAKATIFU, sasa mahakama imetengua ushindi wa YESU KRISTO!!!!!!!
laana hizi za kujiita Mungu zitawatafuna wote watatu, kwa kuwa sijamsikia kikwete akikana kuwa yeye si MUNGU kama alivyotajwa huko Sumbawanga, ni wakati muafaka wa yeye kukataa hili
Mh this is very serious, MUNGU awarehemu na kuwasamehe, na wakatubu la sivyo wataoza wanajiona
Another opportunity ya kuigalagaza CCM.
Mwigulu na Nape wapo Nkinga Igunga leo nielekezeni namna ya kupost niwaletee habari kamili.
huyu alisema aesh alisema wazi kuwa kikwete ni MUNGU, yeye ni YESU KRISTO, na yule DIwanini ROHO MTAKATIFU, sasa mahakama imetengua ushindi wa YESU KRISTO!!!!!!!
laana hizi za kujiita Mungu zitawatafuna wote watatu, kwa kuwa sijamsikia kikwete akikana kuwa yeye si MUNGU kama alivyotajwa huko Sumbawanga, ni wakati muafaka wa yeye kukataa hili
Siamini hata kidogo kama ccm hawatakat rufaa coz hawana ujanja wa kushinda uchaguzi huo
Ni rahisi,fuata haya maelekezo.
Pale katika home page ya Jamii Forums kuna majukwaa mbalimbali.
1.Kwa kuwa hoja yako ni ya siasa bonyeza option ya ''jukwaa la siasa''.
2.Kisha bonyeza sehemu iliyoandikwa ''post a new mesage'',
3.Baada ya ukurasa kufunguka andika kichwa cha habari (mfano, ''Nchemba na Nape walopoka''),then shuka chini andika ujumbe wenyewe.
4.Baada ya kufanya hivyo,chini kabisa bonyeza option iliyoandikwa ''submit''.
5.Ukifuata hatua zote hizo kwa ukamilifu tutakuwa tumeweza kupata ujumbe wako