Uchaguzi mdogo wanukia Sumbawanga Mjini

OSOKONI

JF-Expert Member
Oct 20, 2011
10,965
5,336
Uchaguzi Sumbawanga Mjini, unanukia baada ya muda wa kukata rufani kwa mujibu wa sheria za uchaguzi kupita na upande wa mrufani kugubikwa na ukimya.

Katibu wa CCM (itikadi na uenezi), Nape Nnauye, alipotakiwa kuzungumzia msimamo wa chama kuhusiana na rufani hiyo, alisema aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Aeshi Hilaly, asingeweza kukata rufani bila kuwasiliana na uongozi.
Nape pia, aliongeza kuwa suala la kukata rufani lilitolewa na Aeshi na sio chama ambapo alimtaka mwandishi wa gazeti hili kuwasiliana na mhusika (Aeshi), iwapo anataka kujua hatma ya kauli hiyo.

“Wewe unauliza, lakini unajua ni nani aliyetoa kauli ya kukata rufani? Tamko la kukata rufani ilitolewa na yeye au chama? Kuuliza wapi tumefikia, muulize yeye. Yeye asingeweza kukata rufani bila kuwasiliana na uongozi,” alisema Nape.

Aidha Nape, alipohojiwa juu ya hatua iliyofikiwa ya ukusanyaji ushahidi wa tetesi za ufisadi kwa baadhi ya makada wa chama hicho wakiwamo wabunge, unaofanywa na kamati ya maadili ya CCM, alisema kwa sasa hawako kwenye nafasi ya kutoa taarifa ya kamati hiyo.

NIPASHE ilipozungumza na Aeshi jana alisema; “Nimekiachia chama, ni muda mrefu umepita…nasubiri majibu. Mimi si msemaji wa chama, nasubiri kukaa na chama ndipo niweze kueleza, maana hata hivyo siwezi kujua kama wewe kweli ni mwandishi wa NIPASHE au la,” alisema Aeshi.

Kwa upande mwingine, NIPASHE ilimtafuta Naibu Spika, Job Ndugai, kujua kama Bunge limeshapeleka taarifa kwa Tume ya Uchaguzi Nchini (NEC) kwamba jimbo hilo liko wazi baada ya muda wa kukata rufani kupita kisheria, alisema:

“Tutalitolea maelezo Oktoba kwenye mkutano ujao wa Bunge. Hatuna uhakikika, tunataka kujiridhisha kwanza kwa mahakama ili tuweze kulitolea maelezo suala hilo kwenye Bunge lijalo.”

Aprili 30 mwaka huu, Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga ilitangaza kuenguliwa kwa ubunge wa Aeshi (CCM), baada ya kushindwa katika kesi iliyokuwa inamkabili ya ushindi wake uliodaiwa kugubikwa na utata dhidi ya aliyekuwa mgombea mwenzake Norbert Yamsebo (Chadema) katika Jimbo la Sumbawanga Mjini, Oktoba, 2010.

Katika uchaguzi huo, Aeshi alishinda kwa zaidi ya kura 17, 328 dhidi ya Yamsebo aliyepapata kura17,132.
Kesi hiyo namba 01 ya mwaka 2010 ilifunguliwa na Yamsebo.

Uamuzi wa kutengua matokeo hayo ulitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Bethwell Mmilla, ambaye alisikiliza kesi hiyo na kuisoma kwa takribani saa matatu.

CHANZO: NIPASHE
 
Kwa kweli ccm wana hali ngumu kama uchaguzi ukirudiwa wajue kuwa hawana chao kwa jinsi wa sumbawanga mjini walivyokichoka chama hiki cha magamba.
 
huyu alisema aesh alisema wazi kuwa kikwete ni MUNGU, yeye ni YESU KRISTO, na yule DIwanini ROHO MTAKATIFU, sasa mahakama imetengua ushindi wa YESU KRISTO!!!!!!!
laana hizi za kujiita Mungu zitawatafuna wote watatu, kwa kuwa sijamsikia kikwete akikana kuwa yeye si MUNGU kama alivyotajwa huko Sumbawanga, ni wakati muafaka wa yeye kukataa hili
 
huyu alisema aesh alisema wazi kuwa kikwete ni MUNGU, yeye ni YESU KRISTO, na yule DIwanini ROHO MTAKATIFU, sasa mahakama imetengua ushindi wa YESU KRISTO!!!!!!!
laana hizi za kujiita Mungu zitawatafuna wote watatu, kwa kuwa sijamsikia kikwete akikana kuwa yeye si MUNGU kama alivyotajwa huko Sumbawanga, ni wakati muafaka wa yeye kukataa hili

.....ni Kweli huu ni Utatu Mtakavitu.... (JK,Aeshi,Diwani)
 
"Wewe unauliza, lakini unajua ni nani aliyetoa kauli ya kukata rufani? Tamko la kukata rufani ilitolewa na yeye au chama? Kuuliza wapi tumefikia, muulize yeye. Yeye asingeweza kukata rufani bila kuwasiliana na uongozi," alisema Nape.

Aidha Nape, alipohojiwa juu ya hatua iliyofikiwa ya ukusanyaji ushahidi wa tetesi za ufisadi kwa baadhi ya makada wa chama hicho wakiwamo wabunge, unaofanywa na kamati ya maadili ya CCM, alisema kwa sasa hawako kwenye nafasi ya kutoa taarifa ya kamati hiyo.

Hapo kwenye red majibu yanaonyesha kuna kafrustration flani hasa baada ya CDM kumpeleka kwa Pilato. Ila pia kanikumbusha mbali sana enzi zile unaomba pocket money kwa Mdingi halafu hana hela, utakula majibu ya hasira, ha ha haaaa!!!!!
 
Hapo kwenye red majibu
yanaonyesha kuna kafrustration flani hasa baada ya CDM kumpeleka kwa
Pilato. Ila pia kanikumbusha mbali sana enzi zile unaomba pocket money
kwa Mdingi halafu hana hela, utakula majibu ya hasira, ha ha
haaaa!!!!!
Mwigulu na Nape wapo Nkinga Igunga leo nielekezeni namna ya kupost niwaletee habari kamili.
 
Uchaguzi Sumbawanga Mjini,
unanukia baada ya muda wa kukata rufani kwa mujibu wa sheria za uchaguzi
kupita na upande wa mrufani kugubikwa na ukimya.

Katibu wa CCM (itikadi na uenezi), Nape Nnauye, alipotakiwa kuzungumzia
msimamo wa chama kuhusiana na rufani hiyo, alisema aliyekuwa mbunge wa
jimbo hilo, Aeshi Hilaly, asingeweza kukata rufani bila kuwasiliana na
uongozi.
Nape pia, aliongeza kuwa suala la kukata rufani lilitolewa na Aeshi na
sio chama ambapo alimtaka mwandishi wa gazeti hili kuwasiliana na
mhusika (Aeshi), iwapo anataka kujua hatma ya kauli hiyo.

“Wewe unauliza, lakini unajua ni nani aliyetoa kauli ya kukata rufani?
Tamko la kukata rufani ilitolewa na yeye au chama? Kuuliza wapi
tumefikia, muulize yeye. Yeye asingeweza kukata rufani bila kuwasiliana
na uongozi,” alisema Nape.

Aidha Nape, alipohojiwa juu ya hatua iliyofikiwa ya ukusanyaji ushahidi
wa tetesi za ufisadi kwa baadhi ya makada wa chama hicho wakiwamo
wabunge, unaofanywa na kamati ya maadili ya CCM, alisema kwa sasa hawako
kwenye nafasi ya kutoa taarifa ya kamati hiyo.

NIPASHE ilipozungumza na Aeshi jana alisema; “Nimekiachia chama, ni muda
mrefu umepita…nasubiri majibu. Mimi si msemaji wa chama, nasubiri kukaa
na chama ndipo niweze kueleza, maana hata hivyo siwezi kujua kama wewe
kweli ni mwandishi wa NIPASHE au la,” alisema Aeshi.

Kwa upande mwingine, NIPASHE ilimtafuta Naibu Spika, Job Ndugai, kujua
kama Bunge limeshapeleka taarifa kwa Tume ya Uchaguzi Nchini (NEC)
kwamba jimbo hilo liko wazi baada ya muda wa kukata rufani kupita
kisheria, alisema:

“Tutalitolea maelezo Oktoba kwenye mkutano ujao wa Bunge. Hatuna
uhakikika, tunataka kujiridhisha kwanza kwa mahakama ili tuweze
kulitolea maelezo suala hilo kwenye Bunge lijalo.”

Aprili 30 mwaka huu, Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga
ilitangaza kuenguliwa kwa ubunge wa Aeshi (CCM), baada ya kushindwa
katika kesi iliyokuwa inamkabili ya ushindi wake uliodaiwa kugubikwa na
utata dhidi ya aliyekuwa mgombea mwenzake Norbert Yamsebo (Chadema)
katika Jimbo la Sumbawanga Mjini, Oktoba, 2010.

Katika uchaguzi huo, Aeshi alishinda kwa zaidi ya kura 17, 328 dhidi ya
Yamsebo aliyepapata kura17,132.
Kesi hiyo namba 01 ya mwaka 2010 ilifunguliwa na Yamsebo.

Uamuzi wa kutengua matokeo hayo ulitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama
Kuu Kanda ya Mbeya, Bethwell Mmilla, ambaye alisikiliza kesi hiyo na
kuisoma kwa takribani saa matatu.

CHANZO: NIPASHE

Nape na Mwigulu wapo Nkinga Igunga leo nipo kwenye tukio nielekezeni namna ya kupost habari niwaletee moja kwa moja ni mgeni ha Jf
 
huyu alisema aesh alisema wazi kuwa kikwete ni MUNGU, yeye ni YESU KRISTO, na yule DIwanini ROHO MTAKATIFU, sasa mahakama imetengua ushindi wa YESU KRISTO!!!!!!!
laana hizi za kujiita Mungu zitawatafuna wote watatu, kwa kuwa sijamsikia kikwete akikana kuwa yeye si MUNGU kama alivyotajwa huko Sumbawanga, ni wakati muafaka wa yeye kukataa hili

Mh this is very serious, MUNGU awarehemu na kuwasamehe, na wakatubu la sivyo wataoza wanajiona
 
sirikali-ccm na mahakama yake itapiga jungu hapo utashangaa kuambiwa rufani ishawasilishwa wanavunja katiba hao kila siku.............. wanajua wakigombea watapoteza, wakikata rufaa kesi itavutwa mpaka uchaguzi ujao.....
 
Mwigulu na Nape wapo Nkinga Igunga leo nielekezeni namna ya kupost niwaletee habari kamili.


Ni rahisi,fuata haya maelekezo.
Pale katika home page ya Jamii Forums kuna majukwaa mbalimbali.
1.Kwa kuwa hoja yako ni ya siasa bonyeza option ya ''jukwaa la siasa''.
2.Kisha bonyeza sehemu iliyoandikwa ''post a new mesage'',
3.Baada ya ukurasa kufunguka andika kichwa cha habari (mfano, ''Nchemba na Nape walopoka''),then shuka chini andika ujumbe wenyewe.
4.Baada ya kufanya hivyo,chini kabisa bonyeza option iliyoandikwa ''submit''.
5.Ukifuata hatua zote hizo kwa ukamilifu tutakuwa tumeweza kupata ujumbe wako
 
huyu alisema aesh alisema wazi kuwa kikwete ni MUNGU, yeye ni YESU KRISTO, na yule DIwanini ROHO MTAKATIFU, sasa mahakama imetengua ushindi wa YESU KRISTO!!!!!!!
laana hizi za kujiita Mungu zitawatafuna wote watatu, kwa kuwa sijamsikia kikwete akikana kuwa yeye si MUNGU kama alivyotajwa huko Sumbawanga, ni wakati muafaka wa yeye kukataa hili

Aaa! Umenikumbusha kumbe huyu ndo alijiita utatu mtakatifu. Na kweli kanisa katoliki lililaani hii kauli ila serikali ya Jk ikatulia na hata huyo anayejiita mlezi wa vyama vya siasa sikumsikia akisema chochote. Na hii laana lazima imtafune .
 
Ni rahisi,fuata haya maelekezo.
Pale katika home page ya Jamii Forums kuna majukwaa mbalimbali.
1.Kwa kuwa hoja yako ni ya siasa bonyeza option ya ''jukwaa la siasa''.
2.Kisha bonyeza sehemu iliyoandikwa ''post a new mesage'',
3.Baada ya ukurasa kufunguka andika kichwa cha habari (mfano, ''Nchemba na Nape walopoka''),then shuka chini andika ujumbe wenyewe.
4.Baada ya kufanya hivyo,chini kabisa bonyeza option iliyoandikwa ''submit''.
5.Ukifuata hatua zote hizo kwa ukamilifu tutakuwa tumeweza kupata ujumbe wako

Bofya sehemu ambayo inasema post a new topic af andika kichwa cha habari af uanze kuflow.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom