Mkuu
Shark kama alivyoonyesha namba Mkuu
Mag3 hiyo ndiyo hali ilivyo
Niongezee kidogo kuhusu mchanganuo wa hizo namba na jinsi unavyotueleza
Republican
Namba inyotakiwa kwa mgombea kubeba bendera ya chama ni 1237
Trump ndiye mwenye wajumbe wengi hadi sasa na hivyo kuwa mfano mzuri wa hesabu
Idadi ya wajumbe wa Trump ni 743 kukiwa na tofauti ya 494 kuifikia magic number 1237
Wajumbe waliobaki katika majimbo yaliyo salia ni 838.
Idadi ya wajumbe anaotakiwa apate kutoka 838 ni 494 ili kufikia 1237 sawa na asilimia 58.9
Hii ina maana, kwa majimbo yaliyobaki Trump lazima ashinde kwa asilimia 58.9 kila moja
Tatizo linakuja katika hali zifuatazo
1. Hadi sasa Trump hajaweza kushinda jimbo lolote kwa asilimia 58
2. Wapo wagombea 3, katika asilimia 100 mmoja wao akipata asilimia 10 katika jimbo na wawili kugawana zilizobaki itakuwa 45% kwa 45% (Hii ni nadharia tu) hapo front runner Trump hataweza kupata ile 58% hata kama ni jimbo moja tu. Hivyo ile nafasi ya kufikia 1237 inapungua
3. Uchaguzi wa Republican ni ule wa winner take all ambapo uwezekano wa Trump kupoteza jimbo moja upo katika majimbo yaliyobaki. Hivyo atakuwa amepoteza 58% ya jimbo ambalo atashindwa.
Asilimia ya kufikia 1237 itakuwa zaidi ya 60 na kufanya ugumu.
Akipoteza majimbo 3 tu katika yaliyobaki namba 1237 haitawezekana
Pili, uchaguzi wa Republican kuna baadhi ya majimbo ni winner take most. Kwamba watagawana wajumbe kutokana na ushindi katika district congressional. Hapo uwezekano wa kupata asilimia 58 anayohitaji ni mdogo sana
Hili linatueleza jambo moja, kwamba kwa Republican uwezekano wa mmoja wao kupata 1237 ni kama haupo.
Kinachowezekana ni kukaribia katika 1237 pengine kukiwa na upungufu wa wajumbe 100 au 200
Katika mazingira hayo lazima uchaguzi uende RNC (mkutano mkuu)
Huko nako mzunguko wa kwanza hautazaa tofauti. Taratibu ni kuwa wajumbe alio nao mgombe watampigia kura watake wasitake. Hivyo, Trump anaweza kuwa na wajumbe 1200 hao watampigia kura kama Cruz na Kasich kwa wajumbe wao
Mzunguko wa pili, asilimia 55 ya wajumbe itakuwa huru kumpigia yoyote. Inawezekana Trump akapata 1237 au la
Mzunguko wa tatu asilimia 85 itakuwa huru kumpigia mgombea, hapa ndipo tutarajie mgombea kupatikana
Hili la mkutano mkuu si rahisi. Kwa mfano, inajenga picha gani Trump mwenye wajumbe (mfano) 1200 akiachwa mzunguko wa tatu na Kasich mwenye wajumbe 160(mfano) kwa wakati huo?
Tumeeleza haya kutoa picha, na tunakiri sheria zinazohusiana na RNC ni ngumu kueleweka.
Mathalani kuna majimbo yana taratibu zake, ndani ya RNC wajumbe watagawanywa kufuatana na takwimu za matokeo ya uchaguzi mkuu 2012 n.k
Tutaangalia Democrat nako hali ikoje kutokana na namba hizo hizo alizoweka Mag3