CCM ni wajanja sana wanatakakuifundisha CHADEMA ili ifuate matakwa yao kwa kisingizio cha demokrasia.Isije ikawa magamba wamemwandaa mamuluki ambae wanataka kumupenyeza kwenye safu ya uongozi wa CHADEMA ili wapate kaunafuu fulani baada ya kubanwa kisawa sawa na uongozi uliyopo.Hii huruma ya magamba kwa CHADEMA wanaitoa wapi?Tangu lini magamba wakawa na demokrasia ya kweli kiasi cha kutaka kuifundisha CHADEMA demokrasia?.Mbona Mwenyekiti wao wa kwanza Jk Nyerere alikaa kwenye uongozi wa TANU bila kuitisha uchaguzi mpaka akaipeleka kwenye uhuru mwaka1961 hata baada ya nchi kupata uhuru aliendelea kuwa mwenyekiti.Ikazaliwa CCM akaendelea kuwa mwenyekiti hivyo hivyo huku akiendelea kuwa Rais wa Tz hata alipoacha urais kwa kipindi cha zaidi ya miaka 30 alikataa kukabidhi nafasi ya mwenyekiti wa chama alikuja kukabidhi baada ya kujiridhisha kuwa sasa ni wakati muafaka wa kukabidhi nafasi hiyo.tangu wakati huo nafasi ya Urais na kwenye chama wagombea walikuwa ni mwenyekiti na kivuli mtindo ambao unaendelea mpaka sasa kwenye nafasi ya uwenyekiti wa chama ambapo ni maruku mwenyekiti wao kupingwa mpaka baada ya muda fulani kupita.Ukija upande wa CHADEMA hakuna hata kiongozi mmoja aliekaa zaidi ya miaka 30 wawe waasisi wa chama au awe nani.Ukiangalia kwenye safu ya uongozi wote ni viongozi wapya humukuti kiongozi wa mwaka 47.CHADEMA wanafaa kuwa walimu wa demokrasia.