Uchaguzi Arumeru: Wawekezaji wachanganyikiwa

EMT

Platinum Member
Jan 13, 2010
14,483
15,308
Kampeni za uchaguzi mdogo jimbo la Arumeru zinaelekea kuwachanganya wawekezaji hasa wa biashara ya maua jimboni humo kutokana na vyama vya CCM and Chadema kudai kwenye kampeni zao kuwa kama mgombea wao atachaguliwa watafanya mabadiliko makubwa kwenye umiliki wa ardhi jimboni humo.

Wawekezaji hao wakubwa wanaogopa kuwa watanyang'anywa ardhi wanayoimiki na kupewa wazawa wa kipato cha chini. Wakati wa ufunguzi wa kampeni za CCM, Rais mstaafu, Mh. Benjamini Mkapa aliwahaidi wananchi wa Arumeru kuwa atamshauri Rais Kikwete afanye mabadiliko ya umiliki wa ardhi jimboni humo.

Mkapa alisema land reform itawezesha kubadili umiliki wa ardhi kutoka mikononi mwa matajiri wachache kwenda kwa wananchi maskini ambao hawana hata ardhi ya kulima. Mgombea wa Chadema Joshua Nasar nae amehaidi kama akichaguliwa atahakikisha kuwa umiliki wa ardhi Arumeru unarudishwa kwa wananchi wa Arumeru.

Ripoti zinadai kuwa kilimo cha maua (horticulture) kimeingizia Tanzania fedha za kigeni karibu $990 million kwa miaka mitatu iliyopita. Karibia asilimia 80 ya kilimo cha maua Tanzania kinafanyika maeneo ya mlima Meru na wanaondesha kilimo hicho ni wawekezaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa Muungano wa Horticulture Tanzania, Jacqueline Mkindi anapinga vikali mapendekezo ya kubadili umiliki wa ardhi Arumeru. Anadai kuwa wanachama wake wako kisheria Arumeru na jitihada zozote za kujaribu kuwaondoa zitaigharimu nchi. Bi Mkindi pia amedai wanafuatilia kwa karibu kampeni za uchaguzi Arumeru.

Dean wa Kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu cha Tumaini Elifuraha Laltaika, amedai kuwa mapendekezo ya land reform Arumeru yako kimyume na Sheria ya Uwekezaji Tanzania ya mwaka 1997 and pia Katiba ya Tanzania. Anadai kwa vile makampuni ya maua yalifanya maombi kupitia ya Sheria ya Uwekezaji ya mwaka 1997, wana-enjoy "investment guarantees" ikiwa ni pamoja na "predictable investment climate."

Bw. Laltaika amezungumzia kifungu cha 22 cha sheria ya uwekezaji ambacho kinasema kuwa "no person who owns, whether wholly or in part, the capital of any business enterprise, shall be compelled by law to cede his interest in the capital to any other person." Pia amedai Ibara ya 13(2) ya Katiba inasema kuwa "No law enacted by any authority in the United Republic shall make any provision that is discriminatory either of itself or in its effect."
 
Hakuna ardhi itakayonya'anywa tena Tanzania; huu si wakati wa nyerere wa kutaifisha mali za watu kipuuzi..

Atakayejaribu awe cdm au ccm tutakutana mahakamani
 
watanzania tumekubali kuongopewa kila kukicha. hawa wanaoahidi wanajua kabisa si kweli wanaweza kutekeleza wanachoahidi. ILA CCM ifahamu ya kwamba, udanganyifu wake huu wa leo ndio kikwazo na shida watakayokutana kesho
 
Hata mimi imenishangaza kidogo maana nilibahatika kuwepo siku ya uzinduzi wa kampeni zote za CDM na CCM, na kubaliana na hilo kuwa kila chama imefanya suala la ardhi kuwa agenda.

Shida ni utekelezani sijui utakuwaje maana naona EMT kaeleza kwa ufasaha.
 
Hakuna ardhi itakayonya'anywa tena Tanzania; huu si wakati wa nyerere wa kutaifisha mali za watu kipuuzi..

Atakayejaribu awe cdm au ccm tutakutana mahakamani


hee! ulikuwa wapi yaani hujui tayarikuwa kuna ardhi inanyang'anywa Tanzania sasa hivi na baadhi ya sehemu watu wanahamishwa au wamehamishwa kwa nguvu kwa ajili ya wawekezaji? Wakatiwa Nyerere ardhi haikuwanyangwa kwa wananchi ili kuwapa wawekezaji!! at least not in the scale we are witnessing now.
 
hee! ulikuwa wapi yaani hujui tayarikuwa kuna ardhi inanyang'anywa Tanzania sasa hivi na baadhi ya sehemu watu wanahamishwa au wamehamishwa kwa nguvu kwa ajili ya wawekezaji? Wakatiwa Nyerere ardhi haikuwanyangwa kwa wananchi ili kuwapa wawekezaji!! at least not in the scale we are witnessing now.

Wakati wa nyerere ilikuwa balaa (wewe hujui kwasababu sio victim) wazee wamenyang'anywa ekari kibao wakajenga juu ya ardhi zetu vijiji, zingine walichukua viongozi in the name of village farm?? hakuna tofauti wakati ule investors ni vijiji vya ujamaa sasa wawekezaji...

Zote ni ujinga ambao hakuna mtu anaweza kufanya..bila kupelekwa mahakamani, let them go mahakamani..
 
Huwezi kumpa mtu ardhi.
Unaweza kumuuzia, lakini siyo kumpa tu ardhi kwa sababu eti amezaliwa maeneo hayo.
 
Mbona watu mnasound kama hii nchi sio yetu?? Yaani kama sheria ipo inayowalinda wawekezaji huku sisi wazawa tukiendelea kusota bila ardhi na kubakia kuwa vibarua kwenye mashamba ya wawekezaji basi tuendelee kukaa kimya na kuumia tu??Hapana sheria zipo na zinabadilishwa kulingana na mazingira , muda na mahitaji. Haingiii akilini muwekezaji anamiliki hekta 1000 huku mzawa wa Meru hana hata nusu hatua!hivi ni mtanzania gani anaweza kwenda ulaya marekani au Asia akamiliki hata nusu eka? Tuache kuwa so cheap na tuone kuwa Tanzania ni nchi yetu na tuna haki ya kuishi ikiwa ni pamoja na kuwa na ardhi.,Land reform in Meru is must!isipofanyika kiutaratibu na kisheria soon bomu tunalokalia la ukosefu wa ardhi litalipuka na hapo wawekezaji watapata hasara kubwa zaidi ingefanyika kwa utaratibu, si dalili zilishaanza kuonekana mwaka juzi watu walipovamia madira estate hapo karibu na sadec??
 
Hakuna ardhi itakayonya'anywa tena Tanzania; huu si wakati wa nyerere wa kutaifisha mali za watu kipuuzi..

Atakayejaribu awe cdm au ccm tutakutana mahakamani

Kwa hiyo hapa wanasiasa wanawazuga wapiga kura tuu?
 
hivi inakuwaje sheria na kila kitu kikabaki kama kilivyo lakin ikaendeshwa hujuma ya kuunguza na kuyaharibu maua yote? hao wezi watahimili kweli? lazima waondoke, wazawa wakiamua
 
hakuna ardhi itakayonya'anywa tena tanzania; huu si wakati wa nyerere wa kutaifisha mali za watu kipuuzi..

Atakayejaribu awe cdm au ccm tutakutana mahakamani

waulize wale wawekezaji wa mbulu watakueleza kuwa mahakama ilizuia kutokuchomwa mali zao..tena hayo makaratasi ya nailon kazi hapo ni nyepesi sana..si kwamba mtaondoka kwa utaratibu bali mtakimbia
 
hee! ulikuwa wapi yaani hujui tayarikuwa kuna ardhi inanyang'anywa Tanzania sasa hivi na baadhi ya sehemu watu wanahamishwa au wamehamishwa kwa nguvu kwa ajili ya wawekezaji? Wakatiwa Nyerere ardhi haikuwanyangwa kwa wananchi ili kuwapa wawekezaji!! at least not in the scale we are witnessing now.

Fuatilia visa vya "kwa nini mkulima Mwamwindi alimwua Dr. Kleruu" vya bwana Magid Mjengwa.
Mimi naona tofauti ni kuwa Nyerere alinyanganwa kila mtu. Ila kwa sasa kumnyanganya tajiri(mwekezaji) ni kosa, ila kwa mlalahoi(Mkulima wa kawaida) hiyo haina tatizo.
 
Wakati wa nyerere ilikuwa balaa (wewe hujui kwasababu sio victim) wazee wamenyang'anywa ekari kibao wakajenga juu ya ardhi zetu vijiji, zingine walichukua viongozi in the name of village farm?? hakuna tofauti wakati ule investors ni vijiji vya ujamaa sasa wawekezaji...

Zote ni ujinga ambao hakuna mtu anaweza kufanya..bila kupelekwa mahakamani, let them go mahakamani..

Ntakupinga kwa nguvu zote viongozi hawakujilimbikizia ardhi
 
kama alifanya kipuuzi mbona hawakushitaki? yawezekana wewe ndio mpuuuzi maana hujui mazingira ya utaifisha wa awali....... nakushauri kama hujui jambo sil lazima uchangie

Hakuna ardhi itakayonya'anywa tena Tanzania; huu si wakati wa nyerere wa kutaifisha mali za watu kipuuzi..

Atakayejaribu awe cdm au ccm tutakutana mahakamani
 
Huwezi kumpa mtu ardhi.
Unaweza kumuuzia, lakini siyo kumpa tu ardhi kwa sababu eti amezaliwa maeneo hayo.

ndo maana mnawauzia wazungu? Kwa nn msitangaze wabongo wanunue aafu wawakodishie hao wawekezaji? Mbona vyote vinafanyika kimya kimya bila kushirikisha wananchi wakati sheria inataka mwekezaji akaombe ridhaa ya wananchi kwanza?
 
Ntakupinga kwa nguvu zote viongozi hawakujilimbikizia ardhi

hawa ndio watanzania wenzetu ambao wanafurahia mtanzania apokwe ardhi na kupewa mzungu aje kulima vanila badala ya mpunga. Muda mfupi baadaye njaa inatokea wanafurahia nyie mnavyowaomba. Sijaona umuhimu wa wanasheria wa nchi hii,wengi wao wanafikiria matumbo yao kwanza na wakishiba wanalala usingizi. Wamekuwa watu wa kuwaelekeza wazungu weakness za sheria za nchi na namna ya kutuibia badala ya kuishauri serikali kuboresha sheria kwa manufaa ya watanzania.
 
Fuatilia visa vya "kwa nini mkulima Mwamwindi alimwua Dr. Kleruu" vya bwana Magid Mjengwa.
Mimi naona tofauti ni kuwa Nyerere alinyanganwa kila mtu. Ila kwa sasa kumnyanganya tajiri(mwekezaji) ni kosa, ila kwa mlalahoi(Mkulima wa kawaida) hiyo haina tatizo.

Hivi ni sheria gani inayotumika kumnyang'anya mlala hoi ardhi lakini inashindikana kutumiwa kumnyang'anya asiye mlala hoi ardhi?
 
Waziri amkana Mkapa Arumeru. Awatetea wawekezaji Arumeru

NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodlucky Ole Medeye amewatetea walowezi wanaomiliki maeneo makubwa ya ardhi katika Jimbo la Arumeru Mashariki kwamba wanamiliki mashamba hayo kwa mujibu wa sheria.
Kauli ya Ole Medeye ambaye alikuwa akimnadi mgombea wa CCM, Sioi Sumari katika kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo hilo inapingana na ile iliyotolewa na Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa alipokuwa akizindua kampeni za CCM, Machi 12 mwaka huu mjini Usa River.

Kadhalika, kauli hiyo inapingana na kauli zote za makada wa CCM na vyama vya upinzani akiwamo mgombea wa CCM Sioi ambao wanakiri kuwapo kwa matatizo makubwa ya ardhi Arumeru, huku wakiahidi kuyashughulikia.

Ole Medeye alisema mashamba yote 13 yanayotajwa yanamilikiwa kihalali na kwamba ikiwa kuna tatizo lolote basi wizara yake itafuatilia ili kuchukua hatua. "Masuala ya umiliki wa ardhi yanasimamiwa na sheria za nchi, kwa hiyo wawekezaji hawa wanaotajwa, wanamiliki maeneo yao kwa mujibu wa sheria. Sasa kama kuna maeneo hayajaendelezwa basi hilo ni suala la kuona jinsi ya kuchukua hatua," alisema Medeye katika mkutano wa kumnadi Sioi uliofanyika katika Kijiji cha Sing'isi.

Medeye ambaye pia ni Mbunge wa Arumeru Magharibi alisema Serikali imekuwa ikichukua hatua madhubuti kutatua kero ya ardhi ndani ya wilaya hiyo na kwa sasa itayatwaa mashamba yote yanayomilikiwa na watu binafsi endapo hayataendelezwa ili yagawiwe kwa wananchi. Aliyataja mashamba ambayo hayajaendelezwa kuwa ni Valeska, Madira na Tanzania Plantation.

Alisema akiwa Naibu Waziri wa Ardhi tayari ametembelea mashamba yote na kwamba Serikali inajipanga jinsi ya kutatua migogoro iliyopo. Alisema endapo watamchagua mgombea wa CCM atashirikiana naye kwa kuwa atakuwa anamkubusha juu ya utekelezaji wa kero za ardhi. Alisema hoja za wapinzani kwamba wanaweza kurejesha ardhi kwa wananchi si kweli kwani ili kufikia hatua hiyo lazima sheria zifuatwe.

Mwananchi
 
Sawa hatukatai wanayamiliki kihalali dada yetu mkindi ili swali la kujiuliza toka wamepewa je wametimiza masharti walopewa?tunafahamu kuwa wengi wao hao walowezi kwanza kabisa pesa walowekeza mashambani hapo wamechukua mikopo kutoka benki zetu wakshindwa kulipa toka 2003 mpaka leo au unabisha tuyataje hayo makampuni na benki yenyewe najua ni mabilioni mengi wamechukua toka benki zetu za ndani lakini mpaka leo ulipaji ni wa kusuasua achilia mbali mauzo ya mau yanayofanyikanje, arafu tunajua hiyo TAHA yenyewe baadhi ya viongozi wa juu wenyewe ni wakopaji na wasiofuta masharti ya mikopo ndio maana Mkindi unatetea..pia kuna fununu kuwa baadhi ya kampuni za wageni BOT imenunua mikopo yao kutoka ulaya hapo unasemaje?
 
Mi napita tu wenye habari mtujuze, ila lazima wachanganyikiwe kwasababu walipewa na magamba hivyo wanaogopa cdm m4c
 
Back
Top Bottom