MchunguZI
JF-Expert Member
- Jun 14, 2008
- 4,009
- 2,169
Mashaka yangu yanatokana na matamshi yake ambayo hayaonyeshi kama ana wajibika kwa Wizara yake. Naona kama hayana ufahamu tunaoutegemea kutokana na kisomo chake.
Kuna wakati nilimuona akiwadhalau watumishi wa vyuo vikuu kwa kudai mabadiliko ktk mfumo wa malipo ya PPF. Badala ya kuwasaidia, akawadhalau na kusema wafanye utafiti ili wapate pesa. "Wasisubiri kulishwa midomoni....", Ohhh! (akaigiza kwa kupanua mdomo wake mbele ya kamera ya TV). Sikujuwa uhusiano wa madi yao na utafiti.
Sasa kuna tatizo la wanafunzi wa vyuo vikuu kushindwa kupiga kura kwa likizo ya lazima waliyopewa bila sababu. Majibu yake tena yamekuwa ya aina hiyo. Anasema eti wasifanye siasa vyuoni. Yamaanisha wameondolewa kwa sababu za kisiasa, basi!
Huyo ndo Waziri akijibu kwa kutumia akili yake yote wakati huo huo anafahamu CCM ndo wanaingiza siasa vyuoni na wamekuwa wakifungua matawi ya CCM vyuoni. Nawasikia sasa wakifungua hata nje ya nchi sijui kwa faida ipi!
Nadhani ni waziri asiyekuwa na faida kwa wadau wa Wizara husika. Huko Maliasili ndo hatuna haja ya kusema ubora wake pamoja na kwamba yeye ni bwana miti.
Kuna wakati nilimuona akiwadhalau watumishi wa vyuo vikuu kwa kudai mabadiliko ktk mfumo wa malipo ya PPF. Badala ya kuwasaidia, akawadhalau na kusema wafanye utafiti ili wapate pesa. "Wasisubiri kulishwa midomoni....", Ohhh! (akaigiza kwa kupanua mdomo wake mbele ya kamera ya TV). Sikujuwa uhusiano wa madi yao na utafiti.
Sasa kuna tatizo la wanafunzi wa vyuo vikuu kushindwa kupiga kura kwa likizo ya lazima waliyopewa bila sababu. Majibu yake tena yamekuwa ya aina hiyo. Anasema eti wasifanye siasa vyuoni. Yamaanisha wameondolewa kwa sababu za kisiasa, basi!
Huyo ndo Waziri akijibu kwa kutumia akili yake yote wakati huo huo anafahamu CCM ndo wanaingiza siasa vyuoni na wamekuwa wakifungua matawi ya CCM vyuoni. Nawasikia sasa wakifungua hata nje ya nchi sijui kwa faida ipi!
Nadhani ni waziri asiyekuwa na faida kwa wadau wa Wizara husika. Huko Maliasili ndo hatuna haja ya kusema ubora wake pamoja na kwamba yeye ni bwana miti.