Ubinadamu wa Mmarekani mweusi ni muhimu kuliko ubinadamu wa Mtanzania Mweusi?

Elice Elly

JF-Expert Member
Dec 9, 2018
1,268
1,593
Najiuliza Swali hilo hapo juu Lakini nakosa jibu. Mwl Nyerere alitufundisha kuwa Binadamu wote ni sawa. Cha ajabu Leo hii uthamani wa Mwafrika aliyeko Marekani na Mwafrika aliyeko Bongo ni tofauti.

Wabongo wanalaani vitendo viovu vinavyo tendwa na wazungu dhidi ya Waafrika lakini hawalaani vitendo viovu vinavyotendwa na Waafrika dhidi ya Waafrika wenzao. Tunashuhudia watu wanauawa, wanapigwa risasi, wanatekwa, wanafunguliwa kesi za kubumbabumba. Lakini hayo kwavile yanatendwa na Waafrika dhidi ya Waafrika wenzao kila mmoja anaona sawa. Ile kauli ya Mwalimu Nyerere ina maana gani?

Matendo yanayotendwa Leo na watawala ni yaleyale waliyo tenda makaburu nasi tukawa mstari wa Mbele kupiga kelele, leo kipo wapi? Tunayatenda tena kwa Uhuru bila kificho na baadhi ya wabunge wakiyashabikia tena wakiwa ndani ya Ukumbi wa Bunge. Waafrika Tuache unafiki, tukemee kwanza ya hapa nyumbani kwani yanatisha zaidi kiasi kwamba watu wameogopeshwa na wanaogopa kufungua vinywa vyao.
 

Attachments

  • IMG-20200505-WA0007.jpeg
    IMG-20200505-WA0007.jpeg
    16.6 KB · Views: 1
Aliyeiba akili zetu alikwenda kuzificha na funguo akatupa baharini, Tanzania tunaitaji elimu kubwa sana kuhusu kujitambua kwanza.
 
MATAGA ndio wanatoa kibanzi kwa jicho lako wakati kwake kuna boriti.
 
Elice Elly,

Mtu mwenye utimamu wa fikra anaguswa na jambo kulingana na alivyolipokea sio kulingana na alivyoshawishiwa, Mkuu kwa kitendo kile kila binadamu mwenye utimamu wa fikra lazima aguswe, Twende kwa mfano tukio lipi la hapa Tanzania ambalo lina akisi sawa na ule unyama, tuanzie hapo Mkuu.
 
Mtu mwenye utimamu wa fikra anaguswa na jambo kulingana na alivyolipokea sio kulingana na alivyoshawishiwa, Mkuu kwa kitendo kile kila binadamu mwenye utimamu wa fikra lazima aguswe, Twende kwa mfano tukio lipi la hapa Tanzania ambalo lina akisi sawa na ule unyama, tuanzie hapo Mkuu.
Una akili NYINGI sana mkuu. Nimeelewa point yako vizuri sana na ni sahihi.
 
Mtu mwenye utimamu wa fikra anaguswa na jambo kulingana na alivyolipokea sio kulingana na alivyoshawishiwa, Mkuu kwa kitendo kile kila binadamu mwenye utimamu wa fikra lazima aguswe, Twende kwa mfano tukio lipi la hapa Tz ambalo lina akisi sawa na ule unyama, tuanzie hapo Mkuu.
Kama tukio la Mwangosi, Lissu, watu kuokotwa kwenye mifuko,matukio haya kama hayakukugusa ubinadamu wako una mashaka. Matukio ya hapa nyumbani wala siyo ya kuokoteza,yapo mengi mnooo yanatokea na watu ziiiiiii
 
Mtu mwenye utimamu wa fikra anaguswa na jambo kulingana na alivyolipokea sio kulingana na alivyoshawishiwa, Mkuu kwa kitendo kile kila binadamu mwenye utimamu wa fikra lazima aguswe, Twende kwa mfano tukio lipi la hapa Tz ambalo lina akisi sawa na ule unyama, tuanzie hapo Mkuu.
Mkuu wa Mkoa kumpiga risasi dereva wa daladala na kumuua, afu siku ya hukumu anaingilia mlango anaoingilia jaji na kesi anashinda hiyo yote sababu anakoneksheni na JMK. Je, wapi duniani ilishawahi kutokea?
 
Mkuu wa Mkoa kumpiga risasi dereva wa daladala na kumuua,afu siku ya hukumu anaingilia mlango anaoingilia jaji na kesi anashinda hiyo yote sababu anakoneksheni na JMK.Je wapi duniani ilishawahi kutokea?
DED kumpiga risasi muumini tena kwa kumfuata kanisani si habari
 
Mtu mwenye utimamu wa fikra anaguswa na jambo kulingana na alivyolipokea sio kulingana na alivyoshawishiwa, Mkuu kwa kitendo kile kila binadamu mwenye utimamu wa fikra lazima aguswe, Twende kwa mfano tukio lipi la hapa Tz ambalo lina akisi sawa na ule unyama, tuanzie hapo Mkuu.
Yule mwandishi kulipuliwa bomu na kubaki nyama tu inamaana hukuwepo?
 
Mtu mwenye utimamu wa fikra anaguswa na jambo kulingana na alivyolipokea sio kulingana na alivyoshawishiwa, Mkuu kwa kitendo kile kila binadamu mwenye utimamu wa fikra lazima aguswe, Twende kwa mfano tukio lipi la hapa Tz ambalo lina akisi sawa na ule unyama, tuanzie hapo Mkuu.
DED kumpiga risasi muumini kanisani,
Aquilini kupigwa risasi then mhusika akiendelea kulamba cha kila mwezi.
Dogo Allen kufa kwa kipigo cha mbwa Koko kwa kuchukuliwa barazani kwao.
Kwa uchache.
And then no justice for them
USA kufutwa kazi na hukumu jela 35 yrs
Askari kuomba radhi familia na Jamii nzima USA na dunia kwa ujumla
hapajustice imeplay part.
 
Mtu mwenye utimamu wa fikra anaguswa na jambo kulingana na alivyolipokea sio kulingana na alivyoshawishiwa, Mkuu kwa kitendo kile kila binadamu mwenye utimamu wa fikra lazima aguswe, Twende kwa mfano tukio lipi la hapa Tz ambalo lina akisi sawa na ule unyama, tuanzie hapo Mkuu.
Mkuu Fatilia kifo cha daud mwangosi rip alafu urudi hapa tujadiliane.
 
Kama tukio la Mwangosi,Lissu,watu kuokotwa kwenye mifuko,matukio haya kama hayakukugusa ubinadamu wako una mashaka. Matukio ya hapa nyumbani wala siyo ya kuokoteza,yapo mengi mnooo yanatokea na watu ziiiiiii
Ni kweli Mkuu hayo matukio yote ni ya kinyama kiwango kisichoelezeka, kama tukio la Lissu ni tukio ambalo lilimgusa kila mtanzania ukiachana na kuingiliwa kisiasa.

Unafikiri kwanini tukio la Lissu liligusa watu wengi tofauti na tukio la Mwangosi wakati yote ni matukio ya kinyama? hapa unagundua ni kwa sababu tu ya taarifa, tukio la Lissu taarifa zilienea kwa kasi sana, Mantiki yangu ni kwamba mtu anaguswa sana kwa kuona kuliko kuambiwa. Kuona mtu anakata roho si jambo la kuzoeleka Mkuu.
 
Ni kweli Mkuu hayo matukio yote ni ya kinyama kiwango kisichoelezeka, kama tukio la Lissu ni tukio ambalo lilimgusa kila mtanzania ukiachana na kuingiliwa kisiasa. Unafikiri kwanini tukio la Lissu liligusa watu wengi tofauti na tukio la Mwangosi wakati yote ni matukio ya kinyama? hapa unagundua ni kwa sababu tu ya taarifa, tukio la Lissu taarifa zilienea kwa kasi sana, Mantiki yangu ni kwamba mtu anaguswa sana kwa kuona kuliko kuambiwa. Kuona mtu anakata roho si jambo la kuzoeleka Mkuu.
Uko sahihi ila nikwambie kitu watanzania kuna upumbavu Fulani wa kuona wale wasiowapenda wanastahili kupata mabaya kwa hiyo hawawezi kuguswa kwa sababu ya roho mbaya. Alafu la mwangosi lilionwa na watu wengi sana pia na kutangazwa na ukizingatia alikuwa Mwana habari.
 
Back
Top Bottom