Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,754
Ni uasi ambao haujapata kutokea ndani ya chama cha mapinduzi CCM.. Baada ya kukaa madarakani muda mrefu sana ni kama kuna kikundi ndani yake kimejikuta kinajiona wao ndio ELITES wa hii nchi, na lolote ama chochote kinachofanyika ni lazima kipate kibali chao.
Imefika mahali kikundi hicho kilichojitengenezea ukwasi na mtandao wa ajabu wenye ufadhili mkubwa wa matajiri waliojatajirikia CCM ambao si watanzania asilia kwa asilimia 100. Kina uwezo wa nani awe nani kwenye nafasi gani.
Ujio wa mwendazake ulifanikiwa kwa kiasi chake kuudhoofisha huu mtandao wa hiki kikundi lakini naye akanaza kuharibu kwa kuanza kutengeneza himaya nyingine mpya ya upande mmoja tena kwa ukatili mkubwa sana.
Hapa kitisho kilikuwa wazi ni vita kati ya himaya mpya ya mwendazake vs mtandao kongwe THE ELITES ... Halafu sasa hiki kirusi kipya cha visiwani chenye vinasaba vingi na The elites! Hili linakolezwa na fununu zisizothibitishwa kwamba Taifa la Tz liko chini ya watoto wa familia moja.. 'Baba mmoja'... Ni TUHUMA!
Yaliyotokea ya mhimili mwingine mpaka kupelekea kujiuzulu, kauli ya mkuu wa kaya kuhusiana na 2025, uteuzi wa baraza jipya la mawaziri na makatibu wakuu pamoja na wengine wote kuna tafsiri moja tuu... Uasi ujao na vita mpya kati ya sukuma gang, mtandao wa the elites , visiwani na bara na chawa wenye maslahi kwa kila upande..
Kila kundi liko chimbo likijiandaa kivyake... Ni mchezo wa kuwindana...uasi mkubwa waja...na ndio nafasi pekee ya walio nje ya mfumo ku take cover!
Imefika mahali kikundi hicho kilichojitengenezea ukwasi na mtandao wa ajabu wenye ufadhili mkubwa wa matajiri waliojatajirikia CCM ambao si watanzania asilia kwa asilimia 100. Kina uwezo wa nani awe nani kwenye nafasi gani.
Ujio wa mwendazake ulifanikiwa kwa kiasi chake kuudhoofisha huu mtandao wa hiki kikundi lakini naye akanaza kuharibu kwa kuanza kutengeneza himaya nyingine mpya ya upande mmoja tena kwa ukatili mkubwa sana.
Hapa kitisho kilikuwa wazi ni vita kati ya himaya mpya ya mwendazake vs mtandao kongwe THE ELITES ... Halafu sasa hiki kirusi kipya cha visiwani chenye vinasaba vingi na The elites! Hili linakolezwa na fununu zisizothibitishwa kwamba Taifa la Tz liko chini ya watoto wa familia moja.. 'Baba mmoja'... Ni TUHUMA!
Yaliyotokea ya mhimili mwingine mpaka kupelekea kujiuzulu, kauli ya mkuu wa kaya kuhusiana na 2025, uteuzi wa baraza jipya la mawaziri na makatibu wakuu pamoja na wengine wote kuna tafsiri moja tuu... Uasi ujao na vita mpya kati ya sukuma gang, mtandao wa the elites , visiwani na bara na chawa wenye maslahi kwa kila upande..
Kila kundi liko chimbo likijiandaa kivyake... Ni mchezo wa kuwindana...uasi mkubwa waja...na ndio nafasi pekee ya walio nje ya mfumo ku take cover!