Uaminifu wa mapenzi na password ya simu

Uaminifu wa mapenzi na password ya simu

Kama sio mwaminifu sio mwaminifu tu je kama nimefuta mambo yangu yote sim haina hata miss call nakupa unaona n mwaminifu asee kuna mambo sio kuaminiana kirahis namna hiyo halaf paswod za nini wakat nyie n wanandoa kuna kaka toka aanza kutumia tachi skrini ameanza kuweka paswod na ni kicheche balaaa asishuhudie sketi mbele yake huyo mkewe kutwa kujisifia nimepata mume kumbe kaliokota gumegume hua tunamchoraga tu
 
Kamwe huwezi kuifaidi tamu ya penzi kwa yule uliyemchagua kutoka moyoni mwako ingali bado nafsi yako ina wasi wasi na mashaka dhidi yake,uwanja wa mapenzi unataka uwe huru kifikra na kimwili na ndio maana wanandoa wanaambiwa kuwa ni mwili mmoja kutokana na kila mmoja kumkabidhi mwenzie moyo wake katika upendo,wasi wasi unatoa ladha na tamu ya penzi unashindwa vipi kumuamini mtu uliyesema kuwa siku haiiishi bila ya uwepo wake hapa duniani.

Unashindwa kumuamini mtu ambaye anakamilisha furaha yako hapa duniani. Usipende kuweka vitu rohoni, kama una mashaka na mpenzi wako,tafuta muda ongea nae kuhusu lile linalokukera,weka mambo bayana pengine aliteleza tu maana yeye pia ni mwanadamu na hana mapungufu vile vile kama walivyo wanadamu wengine,unatakiwa ukiwa na yule umpendae ujisikie fahari na ujisike kama umefika mahali penye pumziko na amani moyoni
 
Utakuta huyo mwenye password ndio anatafuta sana kuifahamu simu ya mwenzie
 
Ndio maana ukimwi hauishi


Ujumbe: kabla ya kugegedana muombe mpenzi wako (kama njia ya kumuandaa) akupe simu yake/zake na uchungulie; akikupa jua ni mwaminifu na endelea hata bila ndomu ila akikataa geuka mzungu wa tano. Wekeend njema

Maana password ndio imegeuka kipimo....
 
Wengi naowafahamu mimi simu zao hazina password yoyote kama zangu zilivyo, siweki hayo ma-paswword naona usumbufu simu yangu mwenyewe alafu kila nikitaka kuingia nitoe kizuizi kwanza ya nini.
 
Ndio maana ukimwi hauishi




Maana password ndio imegeuka kipimo....
Password ni kipimo tosha cha kuzuia ukimwi. Naomba nijieleze, unaweza kupima mwenza wako nyote mashallah mkawa hamna, baada ya miezi mitatu mkarudi mkathibitisha hamna. Mkaanza kutumbua ile halua kwa raha zenyu nyama kwa nyama. Kivumbi mmoja wenu anachepuka na kuupata, mwenzangu na mie anaamini kuwa mwenzake hachepuki, la haula kumbe anaogelea katika liukimwi. Lakini kama unafahamu password, kuchepuka hakuwezekani. Siku hizi mtu akitaka kutongoza anaomba namba ya simu, kama unajua mpenzi wako ana password, huwezi kumpatia na hapo umeepusha ukimwi. Miss Chagga hii ni kweli au uongo
 
Password imekuwa janga kwenye mahusiano sina hamu angalau vijana wasiooa waweke lakini sio wanandoaa agggggrrrrr.uuwi inaboa sana jitu ndani liko below perfomance eti lina weka tena siyo password bali finger print yake tu ndio yafungua.dawa yao ni kuchepuka ili nawe aone raha ya kuweka hizo pass upuuzi
 
Uuiwii mmenigusa nateswa sana na password ya mume,imagine nimekuwa muaminifu kupita kawaida dah so sad.badilikeni mnaofanya hivo.kama huchepuki pass ya nini??????
 
Mapenzi kama pori zito usilolijua historia yake maana hujui wapi utapata maji ya kunywa,wapi kitoweo,wapi kivuri kizuri mabacho ni nadra kukuta nyoka,wapi njia nzuri isiyokuwa na maporomoko ya maji.....haihitaji umakini au kujitoa akili kujifanya hujali kinachoendelea ila Mungu ndio inapaswa atuongozee kinyume ya hapo hali inaweza kuwa tata sana
 
Binadamu yeyote haaminiki kwa lolote .kwetu wakristo tunasema amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu.
wakristo tunaposeamini kuw amelaaniwa kila amtegemeaye mwanadamu tunamaanisha kitu tofauti ndugu..hapa inamaanisha kuamini kuwa mwanadamu flani ndo anawezesha existence yako katika mambo ya riziki, afya, uhai na mengineyo, na kwamba mwanadamu fulani ana power ya kucontrol destiny yako.

Hii inaapply zaidi kwa watu wenye kuamini waganga wa ramli, wasoma nyota na the likes.

Never use maneno ya Biblia if you dont fully understand their meaning, yanaweza kumpindisha njia mtu..."ole wake amsababishiaye mtu kutenda dhambi"

dont get your facts mixed up...ubarikiwe
 
Wengine passwords tunaweka ili simu ikiibiwa au kupotea upate time kidogo ya kui-block simcard yako kabla damage haijafanyika. Ila ikitokea nikawa na manzi halafu simu yangu au yake ikatunyima amani, then hatuwezi kuendelea tena cos hakuna uaminifu. If u can't trust my word, then you ain't the one.
 
Back
Top Bottom