Ua gani

Ua gani

Idd Ninga

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2012
Posts
5,539
Reaction score
4,854
1>rangi yako ya waridi,nzuri kama samawati.
Nikahisi ni zawadi,ilojawa na swifati.
Kumbe siyo maridadi,wewe kama afiriti.
Ua hili ua gani,kila mtu alichuma.
2>vijana hadi watoto,wanapenda kulichuma.
Hadi wala misokoto,walichuma kama sima.
Ningekupa mkong'oto,ila sitaka lawama.
Ua hili ua gani,kila mtu alichuma.
3>wengi waliniambia,ua hili ni balaa.
Sikutaka wasikia,nikajifanya kichaa.
Ila leo najutia,hadi nahisi kinyaa.
Ua hili ua gani,kila mtu alichuma.
4>ua sasa lachukiza,lachukiza linakera.
Limekuwa kama giza,msimamo wa bendera.
Tena sitolichunguza,nitaliacha segera.
Ua hili au gani,kila mtu alichuma.
5>ua tena silitaki,chooni nenda litupa.
Lanuka kama samaki,sitolifata kwa pupa.
Nalinda yangu hamaki,nitoe hasira papa.
Ua hili ua gani,kila mtu alichuma.
Shairi=UA GANI.
Mtunzi=IDD NINGA wa Tengeru Arusha.
0755519736.
 
1>rangi yako ya waridi,nzuri kama samawati.
Nikahisi ni zawadi,ilojawa na swifati.
Kumbe siyo maridadi,wewe kama afiriti.
Ua hili ua gani,kila mtu alichuma.
2>vijana hadi watoto,wanapenda kulichuma.
Hadi wala misokoto,walichuma kama sima.
Ningekupa mkong'oto,ila sitaka lawama.
Ua hili ua gani,kila mtu alichuma.
3>wengi waliniambia,ua hili ni balaa.
Sikutaka wasikia,nikajifanya kichaa.
Ila leo najutia,hadi nahisi kinyaa.
Ua hili ua gani,kila mtu alichuma.
4>ua sasa lachukiza,lachukiza linakera.
Limekuwa kama giza,msimamo wa bendera.
Tena sitolichunguza,nitaliacha segera.
Ua hili au gani,kila mtu alichuma.
5>ua tena silitaki,chooni nenda litupa.
Lanuka kama samaki,sitolifata kwa pupa.
Nalinda yangu hamaki,nitoe hasira papa.
Ua hili ua gani,kila mtu alichuma.
Shairi=UA GANI.
Mtunzi=IDD NINGA wa Tengeru Arusha.
0755519736.

duh bro unaonekana una kipaji cha iyo mambo
 
Back
Top Bottom