MAFILILI
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 2,377
- 1,200
Gazeti la Tanzania Daima limefanikisha kuzima msuguano kati ya kambi ya Lema na Zito ambao ulitishia uhai wa CHADEMA kisiasa. Hali hii imetokana na gazeti husika kupamba kurasa za mbele habari zinazomhusu kada wa CCM, Mheshimiwa Profesa Kapuya. Kwa kweli hili gazeti lina sababu za msingi kupelekwa mbele ya dawati la kamati ya maadili ya TCRA kutokana na mwenendo wa kuandika habari za kukashifu viongozi walipewa dhamana na wananchi kwa kura nyingi. Huku ni kudhihirisha kuwa BARAZA la MAADILI la Vyombo wa Habari limeshindwa kutumia mamlaka yake kudhibiti hili gazeti. Huu ni wakati muafaka kwa taifa kutunga sheria za magazeti kwa lengo la kuadabisha waandishi kama wa Tanzania Daima ambao wameweka mbele maslahi ya CHADEMA huku maslahi ya nchi yakipewa umuhimu mdogo