Twaweza wakwepesha jina la anayeongoza

Twaweza wakwepesha jina la anayeongoza

Kipenzi Changu

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
58,047
Reaction score
134,349
Mwakilishi wa Twaweza Aidan Ayakuze alikuwa ITV Habari akiongelea matokeo ya utafiti kuhusu uchaguzi.Amesema kadhaa kwa ufupi ikiwa pamoja na uwepo wa watanzania wasiojua taasisi inayosimamia uchaguzi.Pia 46% wanataka kusikiliza sera kabla ya kuchagua...Ila jina la mgombea anayeongoza hakutajwa.Sina uhakika kama dodoso halikuwa na swali hilo au lah
 
kuna utafiti wanaufanya tena kuanzia wiki ijayo
 
Wanajua EL ndio mpangaji wa magogoni mtarajiwa
 
Watanzania wengi tumeshaamua kuwa tutamchagua lowassa kuwa rais na amiri jeshi mkuu wa jmt.
 
Lowasa atasikiliza na atasimamia tiba bure kwa wwzee na watoto.ccm wameshindwa.wanacho haidi hawatekelezi
 
WATANZANIA WENGI TUMESHAAMUA KUWA HATUTAMCHAGUA LOWASSA KUWA RAIS NA AMIRI JESHI MKUU WA JMT, porojo tunawaachia wapumbavu.
La kwanza, je hao wapumbavu nao ni Watanzania? La pili, je hao wapumbavu watazuiwa kupiga kura? La tatu, huoni kama ungefanya vema kuwaambia wasio wapumbavu wamchague nani au jina lenyewe halina mvuto? Na mwisho unaonaje ukitilia maanani ustaarabu wa mtandao, mbona wapumbavu wao wanajua etiquette ya internet?

Mods nawaomba kwa heshima na taadhima, maandishi kama haya yawe yanafutwa mara moja, hayaoneshi adabu na yanatuumiza macho.

CC: Cookie, Mhariri, Active, Moderator
 
Kazi mnayo,mwaka huu,niEL wa tz tumeamua
 
Alichonifurahisha alisema wananchi wengi waliohojiwa walisema wamechoshwa na ahadi zisizotekelezwa halafu mwishoni akasema wananchi wamesema wanasikiliza Sera na sio maneno ya wagombea wenye fedha hapo mwishoni ni wazi ndicho alichokuwa katumwa.
 
Magufuli...ndie rais wetu wanyonge....
 
Lowassa hazuiliki! Hata mganga wenu kingunge alishawaambia hamshindi
 
kwa dalili hizi ni dhahiri kwamba hali si nzuri kwa upande fulani
 
Back
Top Bottom