Head teacher
JF-Expert Member
- Mar 10, 2012
- 1,796
- 413
Ninatumia king'amuzi cha Zuku, ambacho kifurushi nilicholipia kinaniwezesha kuona Citizen TV,QTV Kenya, na NTV. Tunafahamu kuwa Kenya wana janga la uvamizi wa Westgate Mall. Jambo lililonistaajabisha ni Uzalendo wa vituo hivi vya TV kuripoti janga hili kwa muda wa masaa zaidi ya 12 wakiwa live. Pia wameweza kuwahamasisha maelfu ya wakenya kuchangia damu kwa majeruhi wa shambulio. Hii ni tofauti sana kwa TV zetu za kibongo ambazo hazitoi taarifa kwa majanga ya dharura kama mafuriko, nk live. Wao kutwa kupiga bongo fleva na taarabu...!