Straight corner
JF-Expert Member
- Nov 18, 2010
- 385
- 132
Habari za siku wana JF?
Leo asubuhi tulikuwa tunaangalia kipindi cha 'Tuongee Asubuhi' kinachorushwa Star TV, mada ilikuwa MSWADA WA SHERIA YA KUTUNGA KATIBA MPYA. Mojawapo ya wageni alikuwa Simbachawene (Mb) na Bw. Marcos kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadam.
Katika majadiliano huyu Bw. Marcos akasema mswada unazuia kuongelea mambo kadhaa kama muungano, urais n.k. lakini huyu mbunge akakanusha na kusema watu wanaelewa vibaya kwani hawajazuiwa kujadili mambo ya muungano, urais ... na hapo ndo ulikuwa mwisho wa kuangalia mjadala kwani rafiki yangu aliyekuwa pembeni akinywa chai alirusha kikombe kwenye screen upande wa yule mbunge na kuvunja screen!
Nilipomuuliza kulikoni alisonya na kuuliza kwamba inamaana Majaji na wanasheria woote wanaosema mswada unazuia kujadili mambo hayo ni wajinga? Hatimaye akaishia kuniomba radhi na kusema Viongozi wanatuona wapumbavu mno!
My take:
Kama sikosei Madaktari wana chama chao ambapo akitokea dactari amekiuka maadili yao wanamchukulia hatua, hivi hawa wanasheria wenyewe hawana cha kuwawajibisha wanapowahadaa wananchi makusudi? Maana inadaiwa huyu mbunge naye ni mwanasheria.
Leo asubuhi tulikuwa tunaangalia kipindi cha 'Tuongee Asubuhi' kinachorushwa Star TV, mada ilikuwa MSWADA WA SHERIA YA KUTUNGA KATIBA MPYA. Mojawapo ya wageni alikuwa Simbachawene (Mb) na Bw. Marcos kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadam.
Katika majadiliano huyu Bw. Marcos akasema mswada unazuia kuongelea mambo kadhaa kama muungano, urais n.k. lakini huyu mbunge akakanusha na kusema watu wanaelewa vibaya kwani hawajazuiwa kujadili mambo ya muungano, urais ... na hapo ndo ulikuwa mwisho wa kuangalia mjadala kwani rafiki yangu aliyekuwa pembeni akinywa chai alirusha kikombe kwenye screen upande wa yule mbunge na kuvunja screen!
Nilipomuuliza kulikoni alisonya na kuuliza kwamba inamaana Majaji na wanasheria woote wanaosema mswada unazuia kujadili mambo hayo ni wajinga? Hatimaye akaishia kuniomba radhi na kusema Viongozi wanatuona wapumbavu mno!
My take:
Kama sikosei Madaktari wana chama chao ambapo akitokea dactari amekiuka maadili yao wanamchukulia hatua, hivi hawa wanasheria wenyewe hawana cha kuwawajibisha wanapowahadaa wananchi makusudi? Maana inadaiwa huyu mbunge naye ni mwanasheria.