TV Program Alert: Msidanganywe na Wanasiasa Kuhusu Uchaguzi Mkuu: Ulikuwa Huru na wa Haki!. Shuhudia!

TV Program Alert: Msidanganywe na Wanasiasa Kuhusu Uchaguzi Mkuu: Ulikuwa Huru na wa Haki!. Shuhudia!

Mag3, kwanini Lowassa and co hataki kuzungumzia jinsi walivyoibiwa kura ili watu waelewe? Niliona hata alipohojiwa na Tido akaulizwa swali juu ya uchaguzi aling'aka na kusema waache kutonesha vidonda! BTW Mimi naamini uchaguzi wa Tanzania sio huru na kuna wizi mwingi hutokea lakini bado nashangaa ni kwanini wanaoibiwa hata siku moja hawajaonyesha waliibiwaje!
1. Ina maana na wao hawajui wanavyoibiwa bali ni hisia tu?
2. Kama wanajua kwanini inakuwa vigumu kuelezea walivyoibiwa ili na wananchi wakajua loopholes zilizopo na uchaguzi mwingine wazizibe?
Ningetamani sana wewe ungekuwa Lowassa unijibu haya maswali, lakini hata hivyo kama unaweza kunijibu nitashukuru!
Watabaruku
Macho_Mdiliko.
Wanajua ila hata wakisema haisaidii kwani kila uchaguzi wezi hubadiri mbinu!
 
Wanabodi,

Hii ni TV Program Alert, ambapo Tume ya Taifa ya Uchaguzi, inashiriki katika maonyesho ya kilimo ya Nane Nane katika uwanja wa Mwl. J.K Nyerere mjini Morogoro.

Ushiriki huo wa Tume ya Uchaguzi kwenye Maonyesho, ni fursa nzuri kwa wale wote wenye madukuduku kuhusu Tume kama ni tume huru, na uchaguzi, kama ulikuwa huru na wa haki.

Kwa vile sii wote wataweza kutembelea banda hilo huko Morogoro, kwa faida ya wengi, nimetembelea banda hilo, na nitarusha vipindi maalum vya banda hilo ndani ya Nane Nane na PPR.

Leo Waziri Mkuu ametembelea banda la Tume, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva, Makamisha Mary Longway na Athina Omari, pamoja na msimamizi mbobezi, Spora Liana, watazungumzia uchaguzi uliopita.

Usikose kuangalia mfululizo wa vipindi vya Tume ya Uchaguzi kwenye Maonyesho ya Nane Nane, kipindi cha kwanza kinaanza leo saa 1:00-1:30 Star TV.

Mkuu Pasco, na Jecha Salim Jecha wa ZEC atakuepo???
Kesho ni Channel Ten, keshokutwa ITV kisha TBC.

Karibuni msikie na kushuhudia jinsi ambavyo huwezi kudanganya matokeo ya uchaguzi!, msidanganywe na viongozi wa vyama kuhusu bao la mkono!, hakuna kitu kama hicho!.

Paskali
 
Wanabodi,

Hii ni TV Program Alert, ambapo Tume ya Taifa ya Uchaguzi, inashiriki katika maonyesho ya kilimo ya Nane Nane katika uwanja wa Mwl. J.K Nyerere mjini Morogoro.

Ushiriki huo wa Tume ya Uchaguzi kwenye Maonyesho, ni fursa nzuri kwa wale wote wenye madukuduku kuhusu Tume kama ni tume huru, na uchaguzi, kama ulikuwa huru na wa haki.

Kwa vile sii wote wataweza kutembelea banda hilo huko Morogoro, kwa faida ya wengi, nimetembelea banda hilo, na nitarusha vipindi maalum vya banda hilo ndani ya Nane Nane na PPR.

Leo Waziri Mkuu ametembelea banda la Tume, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva, Makamisha Mary Longway na Athina Omari, pamoja na msimamizi mbobezi, Spora Liana, watazungumzia uchaguzi uliopita.

Usikose kuangalia mfululizo wa vipindi vya Tume ya Uchaguzi kwenye Maonyesho ya Nane Nane, kipindi cha kwanza kinaanza leo saa 1:00-1:30 Star TV.

Kesho ni Channel Ten, keshokutwa ITV kisha TBC.

Karibuni msikie na kushuhudia jinsi ambavyo huwezi kudanganya matokeo ya uchaguzi!, msidanganywe na viongozi wa vyama kuhusu bao la mkono!, hakuna kitu kama hicho!.

Paskali


Paskali kwa nini Jamii Forum iliondolewa hewani wakati wa uchaguzi? Ukinijibu kwa ufasaha huenda nikayaamini hayo maonyesho yako ya kilimo cha kura huko nane8
 
Sasa naanza kuamini Magufuli hakushinda kihalali...huu utetezi si bure. Mizuka ya udanganyifu haitamwacha Lubuva apumzike kwa amani...na bado.
Kusoma hujui...... Ok!
Picha nayo je,.......... Unaweza kuiona!
Haya, twende sasa;
Unafikiri nguvu kubwa iliyotumika kuwakamata vijana wa IT wa chadema ilikuwa kwa nia gani?
Nakupa na hii, unafikiri sababu ya kuvamia kituo cha haki za binadamu pale kijito nyama na kukamata wafanyakazi 7na simu za ofisi waliokuwa wakiratibu mchakato wa uchaguzi ilikuwa ni nini?
Tukio hilo lilitokea wk moja baada ya kuwakamata wale wa chadema na kufunguliwa kesi za kuwa hawakuwa raia wa tz.
Na mwezi uliopita ndipo wamerudisha komputa za kituo cha haki za binadamu zikiwa zimefutwa program zote!
Ccm walishinda kihalali mara ya mwisho 2005.
 
Sasa mbona kuna kesi zipo mahakaman na baadhi ya wabunge wamekuwa wakitenguliwa kwa kusingizia kulikuwa na wizi Wa kura. Alafu Mtoa mada hapo unasema kuhujumu matokeo haiwezekan
 
Uovu waliofanya kwenye uchaguzi ule bado unawatafuna ndani kwa ndani.

Sasa naanza kuamini Magufuli hakushinda kihalali...huu utetezi si bure. Mizuka ya udanganyifu haitamwacha Lubuva apumzike kwa amani...na bado.
 
Nyie ndio maadui kwa kupotosha watu, eti tume emechakachua wakati kosa mlilolifanya ni kumkumbatia fisadi.
Mi huwa nawashangaa sana mnapoishia kutupayukia kuwa ni fisadi halafu hamchukui hatua huko ni kokosa hoja na kutoitendea haki nchi!
Mpelekeni mahakamani.........!
Mahakama ni yenu, majeshi munayo!
Tatizo ni nini hapo.
Mpaka hapo nishaamini kuwa mnamwogopa lowasa .
Na mnamwogopa kwa sababu hoja zenu dhidi ya ufisadi wake ni za kutunga hofu yenu ni kuwa mkithubutu kufanya hivyo atawavua nguo mchana kweupe.
Haiwezekani rais, mawaziri wake, makada na watu mashuhuli waendelee kulalama pasipo kuchukua hatua.
Mimi nilidhani mahakama ya mafisadi iliyokuwa ikisubiliwa ianze ingeanza na watu kama Lowasa lkn kinachotokea ni ngojera na maigizo tupu.
 
Wewe unauliza wanaibiwaje? Nenda kaulize nini kilitokea Zanzibar. Hujaona uchaguzi wa kupata mmea Jiji laTanga na Dar na morogoro,hujaona uchanguzi wa serikali za mitaa na ubunge,aliyeshindwa anatangazwa mshindi.Tume huru kwa sssa haiepukiki.Hao wakurugenzi wanaotangaza matokeo ya ubunge ni makada wa chama gani?Ni wangapi waliotangaza wapizani wameshinda na bado wapo kwenye nafasi zao?Nafisi ya MTU huwa haiwezi kudaganywa,hata kama utapita muda gani bado zitasema ukweli ndani yao,tuwaachie wao na nafisi zao ziwahukumu,Tanzania kwanza.
 
Wao wenyewe wanajua walishindwa
Huwezi kula matapishi yako ukaonekana mzima
Lazima upelekwe kupimwa.

Watanzania wanalifahamu hilo
Uchaguzi ule ulijawa na mihemuko na mbwembwe lakini kwa uhalisia
Upinzani haukuwa na hoja za maana kuchaguliwa
Watu hawajachagua hoja. wamechagua mtu. hoja hazingii kwenye sanduku la kula
 
Wanabodi,

Hii ni TV Program Alert, ambapo Tume ya Taifa ya Uchaguzi, inashiriki katika maonyesho ya kilimo ya Nane Nane katika uwanja wa Mwl. J.K Nyerere mjini Morogoro.

Ushiriki huo wa Tume ya Uchaguzi kwenye Maonyesho, ni fursa nzuri kwa wale wote wenye madukuduku kuhusu Tume kama ni tume huru, na uchaguzi, kama ulikuwa huru na wa haki.

Kwa vile sii wote wataweza kutembelea banda hilo huko Morogoro, kwa faida ya wengi, nimetembelea banda hilo, na nitarusha vipindi maalum vya banda hilo ndani ya Nane Nane na PPR.

Leo Waziri Mkuu ametembelea banda la Tume, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva, Makamisha Mary Longway na Athina Omari, pamoja na msimamizi mbobezi, Spora Liana, watazungumzia uchaguzi uliopita.

Usikose kuangalia mfululizo wa vipindi vya Tume ya Uchaguzi kwenye Maonyesho ya Nane Nane, kipindi cha kwanza kinaanza leo saa 1:00-1:30 Star TV.

Kesho ni Channel Ten, keshokutwa ITV kisha TBC.

Karibuni msikie na kushuhudia jinsi ambavyo huwezi kudanganya matokeo ya uchaguzi!, msidanganywe na viongozi wa vyama kuhusu bao la mkono!, hakuna kitu kama hicho!.

Paskali
Kama kudanganyika mi nshadanganyika. niache hivyo hivyo. sina haja na huo ukweli
 
Back
Top Bottom