warumi
R I P
- May 6, 2013
- 16,213
- 18,455
Hakuna vipengele vinavyoniboa kwenye Tuzo za watu, kama hivi vya sijui mwanamuziki na muigizaji anayependwa, binafsi sioni kama kuna mantiki apo, yani msanii ata kama hufanyi vizuri ila kwa kuwa akina matikiboko yao wanakupenda kule insta kwa mambo yako binafsi, na sio kazi ya msanii, basi wewe unafaa kupewa tuzo, hii inakera sana, tujifunze kutofautisha kati ya wasanii wanaofanya sanaa kama kazi na wale wanaofanya kama fashion (in Lulu's voice ) .
Ni aibu kumpambanisha Riyama Ally na akina Wolper, Lulu na Wema, eti kwa kuwa tu Lulu anapendwa sana Instagram jinsi anavyovaa na kujipiga ma selfies basi wampe tuzo yeye na kumuacha Odama, huu ni uonevu na tunawavunja moyo sana wasanii wenye vipaji halisi. Ni bora mkawatoa kabisa akina Riyama ili muwaweke wale mnaoona wanastahili.
Hao akina Lulu na Wema wana tuzo zao uko kwa Shigongo zinaitwa IJUMAA SEXIEST GIRL kila mwaka wanashindanishwa makalio na kukaa uchi, ila kwenye vipaji kwa kweli hamuwatendei haki. Mwaka jana Wema sepetu alichukua tuzo ya Ijumaa sexiest girl, pale alistahili kabisa kwa kuwa Wema ni sex kabisaa, tuzo ambayo ilichukuliwa pia na jJck kabla ya kuitwaa Wema.
Kama kweli mmeamua kutoa tuzo za heshima kwa wasanii wenye vipaji basi zingatieni vipaji na sio vinginevyo.
Unapompa tuzo Wema au Lulu kuwa msanii bora wa kike, kwa kazi gani? Kwa filamu ipi? Na kwa kiwango gani? Mnawaacha akina Thea, Mainda, Wellu sengo, Odama, Nisha, Johari wanaohangaika kwa ajili ya sanaa, wanajituma ubora wao unaonekana, kwa kweli inasikitisha sana.
Ni aibu kumpambanisha Riyama Ally na akina Wolper, Lulu na Wema, eti kwa kuwa tu Lulu anapendwa sana Instagram jinsi anavyovaa na kujipiga ma selfies basi wampe tuzo yeye na kumuacha Odama, huu ni uonevu na tunawavunja moyo sana wasanii wenye vipaji halisi. Ni bora mkawatoa kabisa akina Riyama ili muwaweke wale mnaoona wanastahili.
Hao akina Lulu na Wema wana tuzo zao uko kwa Shigongo zinaitwa IJUMAA SEXIEST GIRL kila mwaka wanashindanishwa makalio na kukaa uchi, ila kwenye vipaji kwa kweli hamuwatendei haki. Mwaka jana Wema sepetu alichukua tuzo ya Ijumaa sexiest girl, pale alistahili kabisa kwa kuwa Wema ni sex kabisaa, tuzo ambayo ilichukuliwa pia na jJck kabla ya kuitwaa Wema.
Kama kweli mmeamua kutoa tuzo za heshima kwa wasanii wenye vipaji basi zingatieni vipaji na sio vinginevyo.
Unapompa tuzo Wema au Lulu kuwa msanii bora wa kike, kwa kazi gani? Kwa filamu ipi? Na kwa kiwango gani? Mnawaacha akina Thea, Mainda, Wellu sengo, Odama, Nisha, Johari wanaohangaika kwa ajili ya sanaa, wanajituma ubora wao unaonekana, kwa kweli inasikitisha sana.