Haiingii akilini wimbo uliotoka mwezi Novemba na kutamba miezi miwili,ushindanishwe na wimbo uliotoka mwezi Machi na kutamba miezi kumi ktk mwaka husika.Ndio maana wasanii wapenda tuzo wanatumia udhaifu huu kwa kutoa nyimbo mpya miezi ya mwisho wa mwaka,maana wanajua wakati wa upigaji kura wimbo unaopigiwa kura ni ule ulio masikioni mwa wapiga kura.Ushauri ni kwamba zoezi la kutafuta kazi bora lianze Januari hadi Desemba kujua kazi iliyofanya vyema kwa mwaka mzima.Hii itaondoa manung'uniko