Wa Nyumbani
JF-Expert Member
- Mar 31, 2011
- 438
- 67
Padri mmoja mzee alistaafu na wanaparokia walimfanyia sherehe kubwa. Katika sherehe hiyo, mbunge wa eneo hilo alipangwa kutoa hotuba ya shukurani ya kumuaga padri huyo kwa niaba ya wanaparokia wote. Bahati mbaya, mbunge alichelewa kufika, Mc akamwomba padri aseme machache wakati wanamsubiri mweshimiwa mbunge. Padri hakujipanga kusema kitu lakini kwa kujitahidi, aliongea. "Wapendwa, naikumbuka sana siku nilipofika katika kanisa hili kwa mara ya kwanza, ila nilipata mshangao siku nilipoanza kuungamisha. Mtu wa kwanza kabisa kumuungamisha alinishangaza sana. kwani alisema amemwibia bosi wake TV, amemwibia ndugu yake pesa za urithi, amezini na jirani yake, na pia katembea na house girl wake. Nilidhani watu wote wa kanisa hili wanatabia kama hizi, kumbe baadaye nikakuta kumbe watu wa hapa ni wazuri sana na hawana dhambi za ajabu ajabu". Mara mheshimiwa mbunge akawasili, padri akakatisha maongezi na mbunge akaanza kuhutubia. "Ndugu wapendwa, ninayo furaha kubwa kwa kunipa nafasi hii kuhutubia kwa niaba yenu. Mimi nina bahati sana kwani padri huyu alipokuja hapa, mimi nilikuwa mtu wa kwanza kwenda na kuungama kwake... (Fundisho-tuwe tunawahi)