Tuwe na tabia ya kusifia wake zetu

Tuwe na tabia ya kusifia wake zetu

Wapendwa habari za jioni,

Poleni na kazi za mchana kutwa,

Utakuta mtu anaishi na mume au mkewe hajawahi msifia mwenzi wake kuwa amependeza,mfano mke ametoka salon amejipamba vizuri anarudi nyumbani mume hamsifii hata kidogo,anaona kawaida tu.

Ila mwanamke yule akienda kazini kila mtu anamsifia kuwa umependeza sana,mumewe hajamsifia na hana hulka ya kumsifia mkewe.Utakuta mkewe huwa anamsifia sana mfano eee mume wangu umenyoa ndevu vizuri,

Hilo tisheti limekupendeza sana mme wangu,watu mlio na wapenzi wenu muwe na tabia ya kuwasifia kwa mambo mazuri wanayo watendea,usiku mwema🙂

Hata kushukuru tu ni dawa ya mapendo, ndoa zingine kitu SHUKRANI haipo...!
 
kusifiwa kuna ongeza kujiamini kwawatu jamani, utashangaa nje wanakusifu nyumbani umetoka hata ujaambiwa umependeza
Tatizo siku hizi mnajipamba kupendezesha watu wengine, sio waume zenu. Unavaa ukiwaza "watu watanionaje," na sio "mume wangu atanionaje "
 
Mkuu unajisikiaje umetoka nyumbani hujasifiwa,unafika office unakutana na mtu anakwambia waaaaao umependeza sana🙂
Kwa sababu hao ndio uliowalenga, hakika watakusifia. Kabla Mumeo hajakuoa ulijipamba kuulenga moyo wake. Mumeo alikuoa kwa sababu kuna mambo yalimvutia kwako, ulipoingia ndani, ukaachana nayo, ukaanza kutumikia matakwa ya wengine ili wakusifie. Hii ndio namna nyepesi kabisa ya kuua moyo wa mumeo. Kila akikutazama hakuoni wewe, anaona mwanamke mgeni maishani mwake. Atabaki kujiuliza, yuko wapi mke wangu mpenzi niliyempenda? Na kama hutakuwa na busara, utatekwa kirahisi tu huko nje, ukijidanganya kuwa unatafuta faraja ya moyo wako.

Enyi wanawake, mjipambe kwa ajili ya kuwavutia waume zenu siku zote, na si kutaka sifa za mtaani. Maisha yako yawe kwa ajili ya kuuteka moyo wa mumeo. Jitahidi kuishi maisha ya uchumba kwenye ndoa yako.
 
Wanawake wa siku hizi mnaingia kwenye ndoa kwa ajili ya "security " tu. Ukiwekwa ndani, unaanza unaendelea kutafuta aina ya wanaume wanaoufurahisha moyo wako. Mumeo unamweka kando kwa sababu utalala naye tu, unawinda hao walio mbali nawe. Kwa hiyo :
1. Unaishi na mumeo kwa sababu ya sheria ya ndoa tu (kimwili)
2. Moyo wako uko kwingine kabisa.
3. Kwa hiyo huwezi kuona jema lolote toka kwa mumeo, na hakika atakuwa kero maishani mwako
4. Tarajia ndoa yenye migogoro isiyo isha, ambayo haina kichwa wala miguu
5. Jiandae kupambana na moyo wako, Kwani utakuwa ukisaka mwanamume ambaye unadhani ndiye alistahili haswa kuwa mumeo.
6. Daima utajiona sawasawa na mfungwa gerezani.

Jiulize leo : kama kweli huyo unayemdhania kuwa ndiye akufaaye angekupenda hivyo, ni kwa nini basi hakukuoa wewe tangu awali? Mwenzako alimchagua mwingine dhidi yako, halafu wewe kakugeuza kipozeo kwa sababu unajirahisi kwake. Wakati wewe ukijidanganya upo kwa ajili yake, mwenzio yupo kwa ajili ya yule aliyemweka ndani. Ukishikwa, shikamana.

Nb:

ISAYA 32:6

MTU AZINIYE NA MWANAMKE HANA AKILI KABISA;AFANYA JAMBO LITAKALOMWANGAMIZA NAFSI YAKE
ATAPATA JERAHA NA KUVUNJIWA HESHIMA WALA FEDHEHA YAKE HAITAFUTIKA
 
Wapendwa habari za jioni,

Poleni na kazi za mchana kutwa,

Utakuta mtu anaishi na mume au mkewe hajawahi msifia mwenzi wake kuwa amependeza,mfano mke ametoka salon amejipamba vizuri anarudi nyumbani mume hamsifii hata kidogo,anaona kawaida tu.

Ila mwanamke yule akienda kazini kila mtu anamsifia kuwa umependeza sana,mumewe hajamsifia na hana hulka ya kumsifia mkewe.Utakuta mkewe huwa anamsifia sana mfano eee mume wangu umenyoa ndevu vizuri,

Hilo tisheti limekupendeza sana mme wangu,watu mlio na wapenzi wenu muwe na tabia ya kuwasifia kwa mambo mazuri wanayo watendea,usiku mwema🙂
Sifa zikizidii ni kerooo...
...
 
Back
Top Bottom