Tuwatumie wageni kwa manufaa yetu; Diplomasia ya kiuchumi baina ya China na Afrika

Philipo Mwakibinga

Senior Member
May 13, 2013
111
175
DIPLOMASIA YA KIUCHUMI BAINA YA CHINA NA AFRIKA

Tarehe 14/12/2020.

Mahusiano ya China na Nchi za Kiafrika yanarejewa kwanzia karne ya 7 bk (baada ya Kristu) hadi sasa. Kwasasa China imekua na uhitaji mkubwa wa malighafi na masoko kwaajili ya kukidhi mahitaji ya viwanda na masoko yake. Wakati huo Afrika imekua na mahitaji makubwa ya fedha za kuendeleza na kujenga miundombinu mbalimbali.

China inatoa kipaombele cha utoaji mikopo yenye masharti nafuu, China wanafanya Uwekezaji wa miradi mikubwa kwa kutoa mikopo nafuu kwa nchi za Afrika ambazo zinautajiri mkubwa wa malighafi na eneo kubwa lenye soko kwaajili ya bidhaa za viwandani kwa maana ya eneo lenye idadi kubwa ya Watu kupewa kipaombele zaidi. Pamoja na unafuu huo China kama nchi nyingine kubwa Duniani imekua ikinyonya nchi za Afrika kwa kusaini mikataba mibovu hasa pale ambapo VIONGOZI wa TAIFA HILO NI LEGELEGE.

Wakati mwingi China wamejikita kwenye ujenzi wa miundombinu mikubwa katika nchi za Afrika kwa kubadilishana na madini, mafuta kwa mikataba ya ujenzi wa miundombinu.

Mahusiano haya yamekuwa ya kichagizwa na kuimarishwa kwa mahusiano ya kidiplomasia, biashara, misaada ya kijeshi kama vile silaha na vifaa vingine.

Ndani ya Bara la Afrika China amekua na ushindani mkubwa na mataifa mbalimbali ya Ulaya na Amerika kama vile Uingereza, Ufaransa na Amerika.

Kwa Mwaka 2009 pekee China alikuwa mdau mkubwa wa Biashara baina yake na Nchi za Afrika huku akimuacha Amerika mbali zaidi kwani alisaini mikataba na mataifa takribani arobaini (40) ya Afrika.

Taarifa zinaonesha kuwa Mwaka 2000 Biashara ya China na Afrika ilikuwa kwa thamani ya dolla za kimarekani Bilioni kumi ($10 Bilioni) ambapo kufikia Mwaka 2014 ilikuwa hadi kufikia dolla za Kimarekani miambili ishirini bilioni ($ 220 Bilioni).

Nilazima tuendelee kuwa na Rais Dkt Magufuli ili Tanzania iendelee kunufaika na Diplomasia ya Kiuchumi kuliko kuwa Miongoni mwa mataifa yanayoibiwa. Uwekezaji huu wa miundombinu ya barabara, umeme, Afya, Elimu, Usafiri wa Aga na mengine mengi unaofanywa na Serikali hii ya Awamu ya Tano ni wazi kuwa tunaenda kuwa Taifa kubwa litakaolo weza kuvuka mipaka katika Duru za kiuchumi Afrika na Duniani kwa Ujuma. Tujenge uzalendo.

Philipo Mwakibinga.
0758-910403.
 
Nyingi ya bidhaa toka China ni substandard, na kwenye mikataba yao mingi huingiza 10% za viongozi.
 
Kupambana katika biashara ya kimataifa unahitaji sekta binafsi yanye nguvu na kazi ya serikali ni kutunga Sera na sheria za kuimarisha na kulinda raia wake kiuchumi.
Utekelezaji wa mikataba ya kidiplomasia ya uchumi huhitaji watu binafsi kwa asilimia kubwa kwa kuwa serikali ni kikundi kidogo tu cha watu wa usimamizi.
 
Theme nzima ya uzi wako iko hapa.

'Nilazima tuendelee kuwa na Rais Dkt Magufuli ili Tanzania iendelee kunufaika na Diplomasia ya Kiuchumi'.
 
Ok ingawa kwenye mada yako kuna kitu ndani yake “Why China”
Ina maana kule kwingine hakuko poa ok!
Mfano mdogo tuuu kulingana na mada zako!
Watu wengi ukiwaambiwa unatak kuajiriwa kwenye kampunibya Mchina au Mzungu?
Atakuambia bora Mzungu hata kama anakunyonya lakini atakulipa vema na Utaishi kesho utakuja tena ila Mchina duuuu hawa jamaa wana Ubaguzi balaaa,Hawa na wahindi hawaachani aiseee.... Roho zao mbaya tuu za Kimaskini!
Wanapenda ujanja ujanja tuuu!
Any way mafa yako Nzuri inataka tupate angalau ahueni.....
 
"Masharti nafuu" yanayoongelewa hapa ni China kutojali haki za binadamu kukiukwa, ufisadi, demokrasia kuvunjwa, na uozo wa aina yoyote ile. Sasa mikopo ya aina hii inamsaidia nani? Kingine ni kwamba benki na kampuni za ujenzi nyingi za China zinamilikiwa na serikali ya China na huwa zinatumika kuzinasa nchi masikini kwenye madeni kama mtumwa. Debt-trap diplomacy. Unapewa mikopo ambayo huwezi kuilipa kwa hiyo inabidi kuwapa tuu malighafi wanazotaka Wachina mpaka wazimalize ndiyo wanafuta deni. Soma hapa kuhusu debt-trap diplomacy

 
Back
Top Bottom