MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,604
Mara nyingi tumekumbana na vitendo vya rushwa. Ingawaje kisheria "mla rushwa na mtoa rushwa wote ni wakosa, lakini mara nyingi tunalazimika kununua haki zetu kwa kutoa rushwa. Kuanzia kijijini kwa balozi hadi kufikia wizarani kwa waziri na walio chini yake, kumejaa wala rushwa na kunanuka. Tumefika pahala kutoa rushwa kumiekuwa mtindo wa maisha yetu na wametuweka kwenye ulingoni kwenye ringi hatuna pa kutokea.
Lakini bado nafasi tunayo, angalau kwa kupunguza hasira zetu kwa kuwataja hapa.
Umewahi kuombwa "kitu kidogo katika kudai haki yako au katika kufuatilia huduma? Polisi amekukamata na kosa, badala ya kukupeleka mahakamani akadai "chai"? Mdada, umelazimika kumridhisha bosi ili upate kazi au usitimuliwe kazini? Mzee wangu uliyekwisha staafu, hukupewa kiinua mgongo chako hadi ulipotoa chochote? Mwanafunzi, ilikubidi kuahidi na baadaye kutoa sehemu ya mkopo wako wa elimu, vyenginevyo usingelipata mkopo? Mwanakijiji, ulipotaka kujenga ilikulazimu kumgawia chai diwani ili upate kibali cha ujenzi? Mfukuza tonge, hukupewa leseni ya kuweka genge lako hadi ulipovaa "shati la mikono mirefu? Mifano ni visa ni vingi.
Ninakuombeni kutaja hapa kila adha uliyopata kwa kudai haki yako.
Nikianza kwa kutoa mfano, niliporejea toka masomoni, Wizara ya Fedha ilikuwa na wajibu wa kunirejeshea gharama za nauli. Nilipigwa tarehe siku nenda siku rudi, mpaka pale"msamaria mwema" mmoja pale wizarani aliponitonya kuwa ili nifanikiwe ingebidi "nile na watu". Kwa umasikini wangu, nilikubali na kutakiwa kutoa 25% ya pesa zile na kweli haikumaliza wiki nikafanikiwa. Siku ya makabidhiano, nilitakiwa kuweka saini kwenye vocha, baadaye "wakahukua chao mapema" kabla ya kuingia mikononi mwangu, yenginevyo tungelivutana mashati. Wewe je, ni mkasa gani wa rushwa uliokumbana nao?
Lakini bado nafasi tunayo, angalau kwa kupunguza hasira zetu kwa kuwataja hapa.
Umewahi kuombwa "kitu kidogo katika kudai haki yako au katika kufuatilia huduma? Polisi amekukamata na kosa, badala ya kukupeleka mahakamani akadai "chai"? Mdada, umelazimika kumridhisha bosi ili upate kazi au usitimuliwe kazini? Mzee wangu uliyekwisha staafu, hukupewa kiinua mgongo chako hadi ulipotoa chochote? Mwanafunzi, ilikubidi kuahidi na baadaye kutoa sehemu ya mkopo wako wa elimu, vyenginevyo usingelipata mkopo? Mwanakijiji, ulipotaka kujenga ilikulazimu kumgawia chai diwani ili upate kibali cha ujenzi? Mfukuza tonge, hukupewa leseni ya kuweka genge lako hadi ulipovaa "shati la mikono mirefu? Mifano ni visa ni vingi.
Ninakuombeni kutaja hapa kila adha uliyopata kwa kudai haki yako.
Nikianza kwa kutoa mfano, niliporejea toka masomoni, Wizara ya Fedha ilikuwa na wajibu wa kunirejeshea gharama za nauli. Nilipigwa tarehe siku nenda siku rudi, mpaka pale"msamaria mwema" mmoja pale wizarani aliponitonya kuwa ili nifanikiwe ingebidi "nile na watu". Kwa umasikini wangu, nilikubali na kutakiwa kutoa 25% ya pesa zile na kweli haikumaliza wiki nikafanikiwa. Siku ya makabidhiano, nilitakiwa kuweka saini kwenye vocha, baadaye "wakahukua chao mapema" kabla ya kuingia mikononi mwangu, yenginevyo tungelivutana mashati. Wewe je, ni mkasa gani wa rushwa uliokumbana nao?