Tuwakatae viongozi wa dini wanaotanguliza ushabiki kwenye siasa

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,976
Mmarekani aitwaye George Carlin once said, "I'm completely in favour of the separation of Church and State. My idea is that these two institutions screw us up enough on their own, so both of them together is certain death."

Haijawahi kutokea katika historia ya Tanzania kusikia vyama vyote vya siasa kwa pamoja vikihubiri Mabadiliko kama vitachaguliwa katika uchaguzi mkuu 2015. Hii inaonyesha wananchi wengi walikuwa wanataka mabadiliko bora.

Uchaguzi umemalizika na Watanzania wengi wamemchagua Dk. Magufuli kuwa Rais wa Tanzania. Huyu ndiye atakuwa kiongozi mkuu wa Mabadiliko hata kama unapenda au hupendi.

Mabadiliko ninayotaka kuyaona kwa sasa ni kuhakikisha viongozi wa dini wanaojiingiza kwenye siasa za kishabiki wanapigwa vita kwa nguvu zote. Kiongozi kujiingiza kwenye ushabiki wa kisiasa ni kuwagawa waumini wake na pia kuligawa taifa.

Hutuwezi kuwa Taifa endelevu kama kuna viongozi wa kisiasa au baadhi ya vyama vitakuwa vikiendesha siasa kwa matakwa ya baadhi ya viongozi wakuu wa dini. Kuchanganya Siasa na dini kwenye taifa lenye wananchi wengi wenye imani za dini tofauti ni kama kuchezea moto kwenye mafuta ya petroli.

Tumewaona viongozi wa dini kama Sheikh Rajab Katimba, Askofu Josephat Gwajima na Askofu Zachary Kakobe wakijiingiza kwenye ushabiki wa kisiasa kwa kutanguliza ubinafsi bila kuangalia madhara kwa waumini wao achilia mbali taifa letu. Tumeyaona matendo yao na kuzisikia kauli zao za kishabiki. Kwa kujiingiza kwenye ushabiki wa kisiasa wamewagawa kifikra na kimtazamo wafuasi wao na watanzania kwa ujumla. Mbaya zaidi, wamewalazimisha kimantiki wafuasi wao wakubaliane na matakwa yao yaliyojengeka katika msingi wa ubinafsi.

Kama hakutakuwa na Mabadiliko ya kupiga vita aina ya viongozi kama hawa, taifa litakuwa linajichimbia kaburi. This is a recipe for disaster.

Amani, Umoja na Upendo havinunuliwi bali vinajengwa kwa gharama kubwa lakini pia vinabomolewa kwa gharama ndogo kama inayofanywa na baadhi ya viongozi wa dini wa aina ya Sheikh Rajab Katimba, Askofu Josephat Gwajima na Askofu Zachary Kakobe.

Tusiruhusu religious belief kuwa political identity nchini. Tusiruhusu viongozi wakuu wa madhehebu ya dini kuwa political identity nchini. Chama cha siasa lazima kiwe cha wananchi wote bila kujali imani zao za dini. Viongozi wa kisiasa lazima wawe ni viongozi wa wananchi wote. Makanisa na Misikiti isiwe ni sehemu ya kueneza itikadi za vyama. Taifa letu liwe zaidi ya nafsi na ubinafsi wetu.

Tuendelee kuwakataa viongozi wa dini wa aina hii na wanasiasa wao wanaowatumia viongozi wa aina hii kama tulivyofanya kwenye Uchaguzi Mkuu uliopita.

Haya ndiyo mabadiliko bora ninayotumaini kuyapata katika utawala wa Rais Magufuli.
8Qe8ujNA.jpg

Bendera za vyama mpaka kwenye nyumba za ibada! tuzikatae siasa za aina hii.

P%2B2.JPG

Baadhi ya Viongozi wa dini, wakiwa katika mkutano mkuu wa Chadema jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Sheikh Rajab Katimba, Askofu Josephat Gwajima (wa pili kulia) na Askofu Zachary Kakobe.
 
Sheikh Ponda wa kwanza.
Sheikh Ponda kumjadili kwa sasa itakuwa ninamuonea kwa sababu nitakuwa ninaingilia haki yake kisheria kwa sababu ana kesi mahakamani inayohusu msingi wa thread yangu.

Tumuache kwanza amalizane na serikali!
 
Anaejiita Askofu Gwajima.......

Askofu askofu askofu na siasa wapi na wapi....Hata aibu haoni...!!!

Mtu anawasema waumini wake kanisani kwake eti kisa ni wanachama wa chama fulani

I hate this Askofu.

Halafu kuna maneno fulanifulani jinsi anavyoyatamka inaonesha hana hata chembe ya hekima.

Nawaskitikia waumini wake.
 
Kardinal Pengo anastahili kukataliwa mapema anapenda kujiingiza katika masuala ya dini.
 
kwani viongozi hawaruhusiwi kuwa wanachama?

Hawa ni matapeli na wenye njaa mtu kama Gwajima hata wanaomwamini ninaona hawako sahihi kifikra Hapo ndio utambue dini nikinvuli cha biashara Fulani ila hata viongozi wengi wadini hawajalitambua hilo wanaburuzwa tu kisa wana njaa
 
Nani kakudanganya kuwa hata hao unaowajua hawashanikii siasa ?!. Gusa taasisi au chama chenye masilahi nao utawasikia wakidai mnachezea amani. Na ni huko wanakokaribishwa kwenye majukwaa.

Viongozi hawa ambao hata serikali inapokandamiza katiba na watu wake huwezi kusikia wakikemea. Viongozi wote wa dini nchi hii hawako sawa , hawatetei wanyonge bali watawala na viongozi
 
Nadhani hujaelewa msingi wa thread yangu.

Tafadhari soma vizuri thread yangu na uielewe vizuri!

Kuna aina fulani ambayo wanaccm wengi mmejijenga nayo kwa muda mrefu, aidha kwa bahati mbaya ama kwa makusudi. sio mara moja au mbili tuliwaona viongozi wa dini wakitumika na chama cha ccm kwa mgongo wa serekali, na hili limefanyika kwa kificho ama hadharani. Siku za nyuma tuliona viongozi wa dini wakiwa mtaji wa ccm katika kupata madaraka, nongwa ilianza pale viongozi wa dini walipojitambua na kuamua kuchukua jukumu lao. Leo hii viongozi wa dini wamekigomea chama cha mapinduzi ndio maana unaona ngonjera kama hizo zako. Naomba nikuulize kuna kosa kiongozi wa dini kuwa mfuasi wa chama fulani cha siasa? Kuna sheria inayokataza hilo?

Leo hii tunaoana wasanii wanatumika katika majukwaa ya siasa, na ccm ndio imekuwa mtaji wao, je wanamuziki hawana wafuasi na huoni kama wanawagawa wafuasi wao? Leo hii mnakaa kimya lakini nadhani huko mbeleni iwapo wasanii nao watakawatolea nje nadhani mtakuja na vitisho na sheria hizi za hisia ili kuhakikisha mnabaki tu madarakani. Kama suala ni wafuasi hata wanamuziki wana wapenzi wao ambao wakati mwingine watakuwa hawakubaliani na mitazamo yao kisiasa. Kama Hamkubaliki si wakati wa kuzuia watu kufuata kile kipendacho roho ili mradi hawavunji sheria za nchi. Lakini kutujia na hisia za kiccm na vitisho vya kizee sio kitu kizuri, ama wewe ndio mlikuwa mnaonyesha sinema za mauji ya Rwanda mwaka 95 mkidanganya wananchi kwamba wapinzani wataleta vita iwapo watachaguliwa? Jiheshimu tafadhali acha kila raia ajiunge na chama apendacho, waliokatazwa kisheria kujiunga na siasa ni askari wa nchi hii na watumishi wa umma.
 
Anaejiita Askofu Gwajima.......

Askofu askofu askofu na siasa wapi na wapi....Hata aibu haoni...!!!

Mtu anawasema waumini wake kanisani kwake eti kisa ni wanachama wa chama fulani

I hate this Askofu.

Halafu kuna maneno fulanifulani jinsi anavyoyatamka inaonesha hana hata chembe ya hekima.

Nawaskitikia waumini wake.
Huyu anachojaribu kukifanya ni kujenga chama cha siasa ndani ya kanisa.

Kama ataendelea kuachwa, kuna uwezekano wa kuanza kupiga marufuku waumini wake ambao hawakifuati chama ambacho anakijenga ndani ya kanisa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom