Tutailipa ACACIA, Ila tuing'oe CCM kwanza

Tutailipa ACACIA, Ila tuing'oe CCM kwanza

kitu ambacho bado sijafahamu ni kwamba tumeibiwa kiasi gani?

maana kimkataba tulipaswa kulipwa 4percent of the value. hivyo kama wali under estimate kwa billion 885 tumepunjwa around 45billion plus may be a penalt. sasa ukizidisha mara miaka 18 hata haifiki trillion moja.

lakini hasara tutakayokuja kuifidia itazidi trillion moja kama tukishindwa kesi huko mbeleni. Kwa niini serikali ya Magufuli isiwaite kwanza uongozi wa kampuni husika ipande opinion yao na hata kuwaruhusu kufanya their independent analysis hata kupitia maabara zile zile walizofanyia serikali kuona je wamefikia same conclussion?
♪♪♪ Nataka nitokee kwenye gazeti ,niuze sura ♪♪♪
♪♪♪ ndundundu ndundundu ♪♪♪
 
You are in deed right Kiongozi Kichokoro. Hilo kwa kweli ndilo ambalo tulitskiwa kulifanya. Siyo kamwe kutumia mabavu tutaumia. Angalia Mugabe hajapona hadi leo. Mambo haya hayataki mihemko ya kisiasa! Tunapotoa ushauri huu sie siyo wahaini. Leo wewe unawezaje kutumia ubabe kwa wenye migodi hii Waingereza na Wamarikani na Wakanada? Isitoshe bado hatujajitoa katika mahakama za usuluhishi ambako tutabondwa na kutakiwa kulipa fidia kubwa kama tulolipa meli ya samaki. Wapinzani siyo wageni ni watanzania. Maoni yao yachukuliwe yafanyiwe kazi. Wasiojua wanashangilia lakini tutaumia, na kwa hilo CCM mtajibu kama mtakavyotakiwa kujibu wizi wa IPTL, MEREMETA, ASCROW n.k. tumechoka kila kitu kinaendeshwa kisiasa. Nchi hii sasa hatuendi mbele tunalimbana tu kisiasa, mpaka lini ?
 
Historia imetusogeza katika ukingo wa haki. Mahali ambapo tunapaswa kutoa haki kwa wenye haki, na kupokea haki tunayostahili.
Ikiwa nguvu itahitajika ni sawa, maana historia itakuwa imetusogeza kwenye ukingo wa machafuko na hatuwezi kukwepa!

CCM imetuletea majanga yasiyomithilika.Ndio iliyopitisha sheria za uwekezaji kimuhemuhe. Ndio waliosign mikataba na wazungu kwa siri.
Na kama rasilimali zetu zimeibiwa basi CCM ni mshiriki namba moja kwenye huo wizi.

Tutamlipa Acacia, sio kwasababu ni halali, ila ni haki yake kisheria.
Na CCM hatuwezi kuwaacha hivi hivi hivi, itageuka ni mazoea.Tutamtendea kama mwizi anavyotendewa.
1. Tuitoe madarakani kabla ya kuidhinisha shilingi yoyote kumlipa Acacia.
2. Wahusika wakuu, Mzee Mkapa & co. Tuwafanyie mahakama ya wazi pale uwanja wa taifa.
TUWAHUKUMU WATU KUTOKANA NA MATENDO YAO.

Ndugu zangu, nyakati kama hizi ni adimu sana katika historia.
Ni nyakati za kipekee na zisizofananishwa na nyingine kwa vijana kuonyesha uwepo na uhai wao katika taifa. Vijana lazima waache alama ya kizazi chao katika historia.

Tumekusanya matatizo mengi kama taifa na hii ni fursa ya kuyatatua.
Nyakati kama hizi zinahitaji maamuzi magumu, roho na mioyo iliyo tayari ambayo hutokea mara chache sana katika historia. Lakini zinapotokea huleta mafanikio makubwa sana kutoka katika uwezo wa juu kabisa wa mtu!

CCM OUT!
Tupo pamoja
 
Historia imetusogeza katika ukingo wa haki. Mahali ambapo tunapaswa kutoa haki kwa wenye haki, na kupokea haki tunayostahili.
Ikiwa nguvu itahitajika ni sawa, maana historia itakuwa imetusogeza kwenye ukingo wa machafuko na hatuwezi kukwepa!

CCM imetuletea majanga yasiyomithilika.Ndio iliyopitisha sheria za uwekezaji kimuhemuhe. Ndio waliosign mikataba na wazungu kwa siri.
Na kama rasilimali zetu zimeibiwa basi CCM ni mshiriki namba moja kwenye huo wizi.

Tutamlipa Acacia, sio kwasababu ni halali, ila ni haki yake kisheria.
Na CCM hatuwezi kuwaacha hivi hivi hivi, itageuka ni mazoea.Tutamtendea kama mwizi anavyotendewa.
1. Tuitoe madarakani kabla ya kuidhinisha shilingi yoyote kumlipa Acacia.
2. Wahusika wakuu, Mzee Mkapa & co. Tuwafanyie mahakama ya wazi pale uwanja wa taifa.
TUWAHUKUMU WATU KUTOKANA NA MATENDO YAO.

Ndugu zangu, nyakati kama hizi ni adimu sana katika historia.
Ni nyakati za kipekee na zisizofananishwa na nyingine kwa vijana kuonyesha uwepo na uhai wao katika taifa. Vijana lazima waache alama ya kizazi chao katika historia.

Tumekusanya matatizo mengi kama taifa na hii ni fursa ya kuyatatua.
Nyakati kama hizi zinahitaji maamuzi magumu, roho na mioyo iliyo tayari ambayo hutokea mara chache sana katika historia. Lakini zinapotokea huleta mafanikio makubwa sana kutoka katika uwezo wa juu kabisa wa mtu!

CCM OUT!

unaitoaje ccm na kumuweka huyo ambaye mkataba wa buzwagi unasainiwa alikuwepo kama waziri mkuu! na mwanahalisi lilidokeza kwamba alikuwepo huko london siku ya kusaini huo mkataba???

msitufanye wajinga bhana! rais tulienaye tuliusikia msimamo wake juu ya usafirishaji wa mchanga hata kabla hajawa rais
27b86d9bf63395cc271248e9e768e5af.jpg
 
Hivi aliyewaambia ACACIA watashinda kesi ni nani? Mbona watanzania hamjiamini, kesi kufunguliwa London au sehemu nyingine yoyote ile duniani haimaanishi Tanzania lazima ishindwe.
Alafu kesi yenyewe ni ya kuomba kuruhusu third party kufanya uchunguzi hata sio kuomba fidia. Watu mnaogopa sana companies za nje, ACACIA wana pesa ndiyo ila a $1 billion dollar company kwa hii age sio scary at all.
Labda mwenzetu ni jaji.
Yaani hata kesi yenyewe bado anahukumu.
 
Acacia iwe chachu ya kumtoa CCM
Nadhani kabla ya hapo mwanze kuwafukuza Lowasa na Sumayi huko UKAWA kwani hao ndo wahusika wakuu, ni vema mkawauliza wakawaeleza kwa kina nn kilitokea-unaposema CCM nashindwa kuelewa kuwa CCM ni kitu gani, kwako wakibadili na kuwa CCF utaendelea kuwachagua co?
 
Hivi aliyewaambia ACACIA watashinda kesi ni nani? Mbona watanzania hamjiamini, kesi kufunguliwa London au sehemu nyingine yoyote ile duniani haimaanishi Tanzania lazima ishindwe.
Alafu kesi yenyewe ni ya kuomba kuruhusu third party kufanya uchunguzi hata sio kuomba fidia. Watu mnaogopa sana companies za nje, ACACIA wana pesa ndiyo ila a $1 billion dollar company kwa hii age sio scary at all.

Mkuu, hebu tupe clue. Kwa mfano tutawashinda kwa kutumia hoja gani?
 
Wewe una uhakika ACACIA watashinda hiyo kesi? Na je umeiona hiyo mikataba? Kufungua kesi mapema ni lazima maana wameguswa sehemu ya maisha yao.lakini cha pili hiyo CCM tutaitoa kwa namna ipi? Ya kuchukua makapi yanayotemwa huko CCM halafu sisi tunayapokea na kuyapatia bendera kugombea kwetu? Hapo ni sawasawa na kutoa CCM A kuja CCM B,,yaani mtu ahamie Chadema leo na kesho apewe kugombea uraisi tena bila utaratibu maalumu? Bado una ndoto ya kwamba tutaitoa ccm? Na haohao pia walikwepo wakati hiyo mikataba ya unyonyaji inapitishwa ioa walinyamaza kimya,wametukwamisha kwenye katiba mpya,ila kukatwa tu uraisi wakakimbilia huku we bado unaamini watatusaidia kuitoa Ccm?amka mkuu,wanasiasa wasikupelekeshe

Mkuu, yaani unataka tuwang'oe ACACIA kwa sababu wanatuibia mali zetu za matrilion. Na unasema wizi huo unafanyika kwa sababu watu fulani walisaini Mikataba ya ovyo na ya Kimangungo. Lakini unataka watu hao hao waendelee kutawala! Mbona sasa sikusomi kabisa. Unataka nini hasa??? Maana kumbe hakuna cha maana unachokisimamia bali unatuchezea akili tu...
 
Ili tumuingize Lowassa ikulu. Mmelogwa nyie sio Bure.

Basi acheni kutusumbua na kelele zenu kuhusu hii mikataba mibovu ya madini. Mnalalamika kisha mnakuja humu kutwambia you want to keep the same status quo? Kama mnataka waliosaini Mikataba ya Kimangungo na wanaopitisha Sheria za ovyo waendelee kutawala, na mnasema hawana mbadala, why are you complaining then???? Acheni kujichanganya.
 
Hebu fikiria siku ambayopo uchunguzi huru ukafanyika alafu ikaonekana huu uchunguzi wa kwanza wa mruma ni sawa na project ya research propasal ya saint joseph kwamba haukuwa na vigezi kozi kwingine ni assumption zao tu katika kufanya ukadiriaji. What will be next na huku hisa zao zinashuka katika soko.

Mkuu ikitokea hivyo then ni lazima tulipe, hadi Rais kufikia kukubali report inamaanisha anawaamini hawa jamaa, na itakua ajabu kama amewapa watu wa ovyo kufanya research haraka haraka wala hawajui calculation zozote, nategemea watakua wamefanya na kurudiarudia mara kadhaa kuhakikisha kua hawajafanya kosa. Na ndiyo maana nilisema waweke data online ili na wengine tufanye statistical analysis, maana njia wanazotumia sio kwamba hakuna anayejua, mtu yeyote aliyesoma statistics anaweza fanya estimate tu na kuona kama wote tutafikia conclusion moja.
 
Back
Top Bottom