Siku Zote Serikali ya CCM imekuwa ikijivunia AMANI na Utulivu. Sasa hiyo Amani na Utulivu imetusaidia nini katika uchumi. Katika Hiyo Miaka tumeona maisha ya kila siku ya watanzania zaidi ya asilimia 90 yakiwa taabani. Shilingi imeshuka thamani na mfumuko wa bei umeongezeka. Pia ni vigumu kupata hiyo shillingi. Vigogo wamejenga nyumba dubai, USA, South Africa,Mbezi Dar.
Inakuwaje uchumi wa Marekani uyumbe halafu dola yao iwe imara kuliko Shillingi ya Tanzania.
UWT/TISS wanasaidia nini?? Mbona hawakuweza kuzuia Kashfa ya EPA, CIS, Majengo Pacha, Richmond, IPTL?? Mbona TISS wasizuie mauaji ya albino.
TISS/UWT ni kwa ajili ya usalama wa nini,??
Angola na Rwanda wamekuwa kwenye vita zaidi ya miaka 16, wametulia kwa miaka michache iliyopita, lakini angalia uchumi wao unavyokuwa kwa kasi, Thamani ya pesa zao inaongezeka, Sisi amani na utulivu imetusaidia nini??
Pia hali mbaya ya uchumi ikiendelea kuwa mbaya, halafu Mambo ya UFISADI yakiendelea ujue kuwa Wananchi watakosa uvumilivu. Dalili zimeanza kuonekana, Zomea zomea viongozi, Kupiga mawe misafara ya Raisi, Maandamano....Bado huku mitaani wananchi wanalaani sana, Wanasema Hii NChi itakuwa ya Michakato mpaka lini au uchunguzi unaendelea mpaka lini. Wanataka mafisadi waadhibiwe, ufisadi ukomeshwe na uchumi uimarike.
Nawaomba hao usalama wa Taifa, wafanye utafiti. Wapande dala dala, waingie madukani kusubiri watu wanaokuja kununua bidhaa, foleni za wagonjwa hospitalini na sehemu mbalimbali zenye mikusanyiko ya watu wa kawaida, maisha ya kawaida . wasikilize mazungumzo na mijadala. Hali ni mbaya, taifa linaelekea pabaya.
UWT/TISS acheni mzaha, fanyeni utafiti na mumshauri RAiS.
PIa ccm yenyewe si moja, si chama kimoja tena. Kuna makundi au umoja fulani fulani au mtandao wenye masilahi tofauti. Hivyo kuna Chama ndani ya Chama. ENzi za MZee Mwinyi haikuwa hivi. Chama ndani ya chama imeanza kujijenga wakati wa mkapa. Na sasa wakati wa Kikwete kuna vyama ndani ya Chama.
Wakulima na wafugaji ni ugomvi. Pia ugomvi kati ya wafanyabiashara upo, mfano mafuta ya diesel.
Natamani kuanzisha mjadala wa kitaifa ili Vyama vyote vya kisiasa vijadili mustakabadhi wa taifa. Angalia Marekani, kuna demokrasia ya kweli na Wamarekani wanapendana mno. Sisi watanzania vipi??
Wamarekani wakimaliza uchaguzi wanarudi mezani wanaanza kujenga nchi.
Pia angalia WAarabu, Warusi (USSR) na Waisraeli. Wanauzalendo na nchi zao. Popote pale walipo wanatetea nchi zao, hata wakenya wapo mbele yetu. Angalia wanavyovutia kamba upande wao masuala ya EAC.
Sisi inabidi tutume wasome nchi za nje wakatuletee Teknologia nchini kwetu.
Pia watu walioko kwenye sekta nyeti na za maamuzi mazito wapewe mishahara mizuri na wawekewe Life insurance. Sasa hapo atakuwa mzalendo. Na kama ataamua kuwa fisadi, ni kuwa ameisaliti nchi na anastahili kunyongwa.