BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,009
Tutaacha lini kuwekeza katika anasa badala ya maendeleo? Thursday, 01 July 2010 10:29
Florence Majani
Mwananchi
NILIALIKWA katika kikao cha harusi. Wajumbe wakawa wanatoa michango kwa mashindano. Kila mmoja akijitahidi kutaja kiwango cha juu cha fedha ili aonekane naye amechangia kiasi kikubwa.
Lakini katika hali ambayo iliwashangaza wajumbe wengi katika kikao hicho, nikiwemo, mama wa bibi harusi alisimama na kutangaza kwamba atatoa Sh60milioni kuchangia harusi hiyo. Nilipigwa butwaa. Nikajiuliza, hiyo ni sherehe tu au kuna la ziada?
Nikatafakari na kugundua kuwa si huyu pekee anayetapanya fedha kwa ajili ya anasa ya siku moja. Wapo wengi na wanafanya hivyo kwa makusudi. Kwa ajili ya ufahari na starehe za muda mfupi tu.
Ni dhahiri kuwa, umaskini wa Watanzania unachangiwa kwa asilimia kubwa na ujinga na uzembe na uendekezaji wa starehe zisizo na msingi. Kwa nchi kama Tanzania, ambayo ni wachache wenye uwezo wa kifedha idadi kubwa wakiwa na maisha duni, haiingii akilini watu kutumbua fedha kwa kiasi kikubwa wakati watoto wanakosa hata madawati ya kukalia katika shule na wengine kujifungulia sakafuni.
Moyo wa uzalendo na kujitoa unahitajika katika kulijenga taifa hili. Umefika wakati wananchi tunapaswa kuachana na fikra za kuitegemea serikali kwa asilimia 100, huku wenyewe tukiwa tunachangia kulididimiza taifa katika lindi la umaskini kila kukicha. Kila mmoja wetu anayo dhamana ya kuangalia ni wapi anaweza kujitolea na kusaidia kwa uwezo alioanao.
Ni vyema Watanzania kufikiria upya kuhusu matumizi yetu, tuepuke kutapana fedha katika mambo ya anasa. Tuangalie vipaumbele vya wengi kama afya na elimu. Hii itasaidia kuinua kwa kiasi fulani hali ya maisha ya Watanzania. Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.
Wananchi wakishirikiana kufanya mambo ya maendeleo, tutapiga hatua na kadri siku zinvyokwenda tutajikuta tunafanya mambo makubwa katika nchi yetu. Huyu akichangia kujenga nyumba za walimu na huyu akatoa madawati katika shule fulani, mwingine akatoa vitanda hospitalini itasaidia kwa kiwango fulani kunyanyua maisha ya Watanzania.
Uwepo wa uzalendo katika vichwa vya Watanzania ni jambo lisilotiliwa mantiki kabisa, badala yake kila mmoja anajali nafsi yake. Wahenga wanasema hata ubuyu ulianza kama mchicha, hivyo Watanzania wakianza kuwa na moyo wa uzalendo wa kuchangia maendeleo, tutafikia walipo wenzetu wenye maendeleo.
Kwa mfano, badala ya kutumia zaidi ya Sh70milioni kwa ajili ya sherehe ya kumuaga binti, fedha hizo, zingejenga hospitali vijijini au kununua vifaa vya hospital au madawati kwa ajili ya wanafunzi wanaoketi chini au vitanda kwa ajili ya wajawazito wanaolala mzungu wa wanne hospitalini.
Hivi karibuni mkereketwa mmoja wa masuala ya mpira wa miguu alitoa tiketi za Sh30,000 kila moja kwa mashabiki zaidi ya 100 kwa ajili ya kutazama mechi kati ya timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) na Brazil kwa mahesabu ya harakaharaka zilitolewa kama Sh90milioni. Ni fedha nyingi, watu wamekwenda kutazama mpira tu na kurudi nyumbani.
Wakati watu hao wakitazama mpira na kukenua, kuna wagonjwa wanaokosa huduma kwa kukosa Sh 10,000 tu za kumuona daktari, wengine wakifariki dunia kwa kukosa fedha za operesheni, walemavu wakichubuka miguu kwa kukosa baiskeli.
Mpaka sasa bajeti ya nchi yetu inategemea zaidi misaada na mikopo kutoka kwa wafadhili. Mpaka lini tutaendelea kutegemea wafadhili? Msaada kwa taifa uanzie nyumbani siyo kwa wageni ambao baadaye hutupa masharti magumu na kutufanya watumwa katika nchi yetu.
Masuala ya burudani yawepo lakini wakati mwingine yafanywe katika namna ya kuchangia huduma za maendeleo ya jamii.
Kwa mfano, wakati tetemeko la ardhi lilipoikumba Haiti, wanamuziki wengi wa Marekani walifanya matamasha, waliimba na fedha zilizopatikana zilipelekwa Haiti, kusaidia walioathirika.
Je, nasi hatuwezi kufanya matamasha ya muziki na michezo ili kupata fedha ambazo zitawekezwa katika maendeleo au huduma za jamii? Ni mamilioni ya fedha kiasi gani, hupatikana wakati wa mechi za mpira wa miguu? Fedha kiasi gani hupatikana wakati mashindano ya ulimbwende au tuzo za muziki? Ni mara ngapi umewahi kusikia msanii amefanya onyesho kisha akaagiza mapato yake yaende kwa watoto yatima au vinunuliwe vitanda hospitalini?
Hakika hayo hufanyika mara chache hapa Tanzania kila mtu anajali maisha yake tu. Sina maana kwamba tusifanye starehe na lakini zifanywe kwa kuangalia mustakabali wa hali zetu na za wenzetu. Kila mmoja ajali maisha ya wenzake pia.
Watanzania wenye uwezo wa kifedha, wanamuziki, wasanii wa fani nyingine na wanamichezo wajipange kuandaa matamasha au burudani za aina yeyote mara kwa mara kwa ajili ya kuchangia huduma za jamii badala ya kusubiri wakati wa maafa pekee.
Kila mtanzania awe na moyo wa kufanya kila awezalo ili naye achangie katika huduma za jamii. Wale wenye uwezo kiasi wawafikirie wale waliokosa kabisa huduma na wanaohitaji msaada.
Florence Majani
Mwananchi
NILIALIKWA katika kikao cha harusi. Wajumbe wakawa wanatoa michango kwa mashindano. Kila mmoja akijitahidi kutaja kiwango cha juu cha fedha ili aonekane naye amechangia kiasi kikubwa.
Lakini katika hali ambayo iliwashangaza wajumbe wengi katika kikao hicho, nikiwemo, mama wa bibi harusi alisimama na kutangaza kwamba atatoa Sh60milioni kuchangia harusi hiyo. Nilipigwa butwaa. Nikajiuliza, hiyo ni sherehe tu au kuna la ziada?
Nikatafakari na kugundua kuwa si huyu pekee anayetapanya fedha kwa ajili ya anasa ya siku moja. Wapo wengi na wanafanya hivyo kwa makusudi. Kwa ajili ya ufahari na starehe za muda mfupi tu.
Ni dhahiri kuwa, umaskini wa Watanzania unachangiwa kwa asilimia kubwa na ujinga na uzembe na uendekezaji wa starehe zisizo na msingi. Kwa nchi kama Tanzania, ambayo ni wachache wenye uwezo wa kifedha idadi kubwa wakiwa na maisha duni, haiingii akilini watu kutumbua fedha kwa kiasi kikubwa wakati watoto wanakosa hata madawati ya kukalia katika shule na wengine kujifungulia sakafuni.
Moyo wa uzalendo na kujitoa unahitajika katika kulijenga taifa hili. Umefika wakati wananchi tunapaswa kuachana na fikra za kuitegemea serikali kwa asilimia 100, huku wenyewe tukiwa tunachangia kulididimiza taifa katika lindi la umaskini kila kukicha. Kila mmoja wetu anayo dhamana ya kuangalia ni wapi anaweza kujitolea na kusaidia kwa uwezo alioanao.
Ni vyema Watanzania kufikiria upya kuhusu matumizi yetu, tuepuke kutapana fedha katika mambo ya anasa. Tuangalie vipaumbele vya wengi kama afya na elimu. Hii itasaidia kuinua kwa kiasi fulani hali ya maisha ya Watanzania. Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.
Wananchi wakishirikiana kufanya mambo ya maendeleo, tutapiga hatua na kadri siku zinvyokwenda tutajikuta tunafanya mambo makubwa katika nchi yetu. Huyu akichangia kujenga nyumba za walimu na huyu akatoa madawati katika shule fulani, mwingine akatoa vitanda hospitalini itasaidia kwa kiwango fulani kunyanyua maisha ya Watanzania.
Uwepo wa uzalendo katika vichwa vya Watanzania ni jambo lisilotiliwa mantiki kabisa, badala yake kila mmoja anajali nafsi yake. Wahenga wanasema hata ubuyu ulianza kama mchicha, hivyo Watanzania wakianza kuwa na moyo wa uzalendo wa kuchangia maendeleo, tutafikia walipo wenzetu wenye maendeleo.
Kwa mfano, badala ya kutumia zaidi ya Sh70milioni kwa ajili ya sherehe ya kumuaga binti, fedha hizo, zingejenga hospitali vijijini au kununua vifaa vya hospital au madawati kwa ajili ya wanafunzi wanaoketi chini au vitanda kwa ajili ya wajawazito wanaolala mzungu wa wanne hospitalini.
Hivi karibuni mkereketwa mmoja wa masuala ya mpira wa miguu alitoa tiketi za Sh30,000 kila moja kwa mashabiki zaidi ya 100 kwa ajili ya kutazama mechi kati ya timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) na Brazil kwa mahesabu ya harakaharaka zilitolewa kama Sh90milioni. Ni fedha nyingi, watu wamekwenda kutazama mpira tu na kurudi nyumbani.
Wakati watu hao wakitazama mpira na kukenua, kuna wagonjwa wanaokosa huduma kwa kukosa Sh 10,000 tu za kumuona daktari, wengine wakifariki dunia kwa kukosa fedha za operesheni, walemavu wakichubuka miguu kwa kukosa baiskeli.
Mpaka sasa bajeti ya nchi yetu inategemea zaidi misaada na mikopo kutoka kwa wafadhili. Mpaka lini tutaendelea kutegemea wafadhili? Msaada kwa taifa uanzie nyumbani siyo kwa wageni ambao baadaye hutupa masharti magumu na kutufanya watumwa katika nchi yetu.
Masuala ya burudani yawepo lakini wakati mwingine yafanywe katika namna ya kuchangia huduma za maendeleo ya jamii.
Kwa mfano, wakati tetemeko la ardhi lilipoikumba Haiti, wanamuziki wengi wa Marekani walifanya matamasha, waliimba na fedha zilizopatikana zilipelekwa Haiti, kusaidia walioathirika.
Je, nasi hatuwezi kufanya matamasha ya muziki na michezo ili kupata fedha ambazo zitawekezwa katika maendeleo au huduma za jamii? Ni mamilioni ya fedha kiasi gani, hupatikana wakati wa mechi za mpira wa miguu? Fedha kiasi gani hupatikana wakati mashindano ya ulimbwende au tuzo za muziki? Ni mara ngapi umewahi kusikia msanii amefanya onyesho kisha akaagiza mapato yake yaende kwa watoto yatima au vinunuliwe vitanda hospitalini?
Hakika hayo hufanyika mara chache hapa Tanzania kila mtu anajali maisha yake tu. Sina maana kwamba tusifanye starehe na lakini zifanywe kwa kuangalia mustakabali wa hali zetu na za wenzetu. Kila mmoja ajali maisha ya wenzake pia.
Watanzania wenye uwezo wa kifedha, wanamuziki, wasanii wa fani nyingine na wanamichezo wajipange kuandaa matamasha au burudani za aina yeyote mara kwa mara kwa ajili ya kuchangia huduma za jamii badala ya kusubiri wakati wa maafa pekee.
Kila mtanzania awe na moyo wa kufanya kila awezalo ili naye achangie katika huduma za jamii. Wale wenye uwezo kiasi wawafikirie wale waliokosa kabisa huduma na wanaohitaji msaada.