Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,179
- 7,298
Nimekuwa nikifuatilia maoni ya wanaCHADEMA, humu Jf na hata mitaani, na wengi wanalaani kushindwa uchaguzi wa mwaka huu na kusema tusubiri 2015, CCM itaanguka.
Ninachotaka kuwaasa ndugu zangu, tukisubiri 2015 bila kujipanga vyema, tutakuja kuumbuka hata zaidi ya mwaka huu. Sote tunajua kuwa pamoja na kazi kubwa tuliyoifanya mwaka huu, lakini tumeishia kuibiwa kizembe mno. Ni sawa na mkulima aliyejituma sana kulima, alipovuna akaweka mazao yake stoo asifunge mlango, then akapita kibaka akachukua kiulaini, sasa mkulima analalamika.
Kusemma kweli naweza sema kuwa mwaka huu tulijiandaa kushindwa, sio kushinda. Naweza kutoa mfano wa jimbo nililopo; kwanza hadi wiki 1 kabla ya uchaguzi, hatukuwa na mawakala katika vituo vyote. Tunaenda kwenye kupiga kura, zaidi ya 25% ya vituo hatukuwa na mawakala. nilijaribu kutembelea vituo kadhaa wakati wa zoezi la kupiga kura, nikagundua kuwa mawakala walikuwa wamelkaa mita kadhaa kutoka kwa anayehakiki majina ya wanaopiga kura; wakala hana karatasi wala orodha ya waliotakiwa kupiga kura pale. Hali kadhalika, katika vituo vingi nilona mpangilio ni kuwa tokea mtu angeweza kupewa karatasi ya kupigia kura, akapiga na kuweka kwenye box, akiwa amemgeuzia wakala mgongo wakati wote,kwa maana kwamba hata angekuwa anapiga kura zaidi ya moja asingeonwa.
Jioni ilipofika, zoezi lakuhesabu kura lilipoingia ndio lilikuwa kichekesho. Kwanza, bila sababu za maana masanduku yalikuwa yanahamishwa kutoka kituo kimoja hadi kingine kabla hayajahesabiwa, eti kwenda sehemu zenye taa! Hakuna wakala aliyekuwa anahoji. Baada ya zoezi lakuhesabu mawakala walikuwa wanatia saini kwenye karatasi za matokeo ambayo yalikuwa yameandikwa loosely kiasi kwamba nakala waliyokuwa wanapewa baadhi ya mawakala ilikuwa haionyeshi chochote, na hakuna aliyegoma kupokea! Mbaya zaidi ni kuwa mawakala baada ya kuhesabu kura katika vituo vingi walitimua zao home, wakiacha mabox ya kura na wasimamizi wa vituo wakisubiri magari ya halmashauri yaje kupitia.
Mawakala wengi waliondoka na nakala za matokeo walizopewa kwenda nazo makwao, hivyo kumfanya mgombea ubunge na wasaidizi wake wategemee zile zilizokuwa zinatoka kwa wasimamizi peke yake wakati wa kujumlisha. Cha kusikitisha zaidi ni kuwa kwa vile vituoa ambavyo CHADEMA haikuwa na mawakala na walitegemea wa CUF, hawakupewa nakala za matokeo kutoka vituoni (hadi leo)
Katika mazingira kama hayo jamani wanaCHADEMA, tunaweza kweli kuilaumu CCM kwa kutuibia? Na hapa nilipo ni mjini, ambapo pamoja na mapungufu yote hayo Dr Slaa aliibuka na zaidi ya 35% ya kura zilizotangazwa na NEC! Ni katika eneo ambalo CHADEMA tulifanikiwa kuwa na wagombea udiwani kweye zaidi ya 60% ya kata zake. Imagine kuwa yapo majimbo mengi ambayo kwanza ni remote, pili hatukuwa na wagombea ubunge na hata kwingine walikuweko lakini wagombea udiwani hawakuweko.
Kwa maoni yangu naamini hata hizi 26% CCM wametuachia, nadhani hawakuamua tu kuzipunguza, wangeweza kuzipunguza sana tu bila ya yeyote kuwapinga kwa ushahidi.
Mi nadhani huu ndio wakati wa CHADEMA kujipanga. CHADEMA wamepata kura (kwa mujibu wa NEC) zaidi ya mil 2. Hii ina maana kuwa kulikuwa na wapiga kura zaidi ya mil 2 ambao wanaiunga mkono CHADEMA. Hivi kweli kutoka kwa hawa watu wote tutashindwa kupata watu 52,000 kuwa mawakala katika vituo vya kupigia kura. Mi naamini wapo watanzania wengi sana ambao wapo tayari kujitolea kwa hiari yao wenyewe, kulinda kura zao, na naamini tunaweza kujipanga na kuwa na mawakala zaidi ya hata watano katika kila kitu (kwa kutumia vyama vingine), kuwa na waratibu zaidi ya hata 10 katika kila jimbo watakaokuwa wanafuatilia kwa karibu zoezi la kupiga kura na baadae watakaoshirikiana kupata jumla ya kura na kuwa na matokeo ya jumla moja kwa moja kutoka vituoni, kabla ya kusubiri kwenda kwa mkurugenzi.
Tatizo ni pale tutakapoamini kuwa wapo watu waliopo kwa ajili ya kufanya hizi organisation. Ki ukweli ndugu zangu, hakuna mtu wa kufanya haya. Sio Slaa, wala Mnyika wa Zito wala Mbowe. Ni sisi wenyewe. Kuna kila umuhimu wa kila mmoja wetu kujisikia yupo responsible na kuhakikisha mambo yanakuwa sawa katika eneo lake alilopo, kama sio jimbo basi hata katika kata yake. Mi nadhani makao makuu wanatakiwa tu kuagiza ongozi za wilaya, ziandae mipango mikakati thabiti ya kila jimbo, ikionyesha mipanglio ya nini kitafanyika kusuka na kuimarisha mitandao ya ushindi katika kila jimbo na kila kata.
Tunafahamu kuwa katika baadhi ya maeneo CHADEMA haina uongozi kabisa au ina uongozi dhaifu (baadhi ya wilaya, hata mikoa). Kwa yale maeneo ambayo hamna uongozi kabisa inaweza kuwa rahisi kwa watu kujitolea na kuwasiliana na makao makuu. Ugumu kidigo upo yale maeneo ambayo yana uongozi dhaifu. Hapa busara inatakiwa itumike sana kwa sababu hatua zozote inabidi zichukuliwe chini au kwa kushirikisha na uongozi uliopo. Sometimes baadhi ya viongozi wanakuwa wazito kiutendaji na ukiwaandama sana wanahisi kuwa unataka kuwanyang'anya madaraka yao. Kwenyemaeneo kama hayo tuwe makini...
Ninachotaka kuwaasa ndugu zangu, tukisubiri 2015 bila kujipanga vyema, tutakuja kuumbuka hata zaidi ya mwaka huu. Sote tunajua kuwa pamoja na kazi kubwa tuliyoifanya mwaka huu, lakini tumeishia kuibiwa kizembe mno. Ni sawa na mkulima aliyejituma sana kulima, alipovuna akaweka mazao yake stoo asifunge mlango, then akapita kibaka akachukua kiulaini, sasa mkulima analalamika.
Kusemma kweli naweza sema kuwa mwaka huu tulijiandaa kushindwa, sio kushinda. Naweza kutoa mfano wa jimbo nililopo; kwanza hadi wiki 1 kabla ya uchaguzi, hatukuwa na mawakala katika vituo vyote. Tunaenda kwenye kupiga kura, zaidi ya 25% ya vituo hatukuwa na mawakala. nilijaribu kutembelea vituo kadhaa wakati wa zoezi la kupiga kura, nikagundua kuwa mawakala walikuwa wamelkaa mita kadhaa kutoka kwa anayehakiki majina ya wanaopiga kura; wakala hana karatasi wala orodha ya waliotakiwa kupiga kura pale. Hali kadhalika, katika vituo vingi nilona mpangilio ni kuwa tokea mtu angeweza kupewa karatasi ya kupigia kura, akapiga na kuweka kwenye box, akiwa amemgeuzia wakala mgongo wakati wote,kwa maana kwamba hata angekuwa anapiga kura zaidi ya moja asingeonwa.
Jioni ilipofika, zoezi lakuhesabu kura lilipoingia ndio lilikuwa kichekesho. Kwanza, bila sababu za maana masanduku yalikuwa yanahamishwa kutoka kituo kimoja hadi kingine kabla hayajahesabiwa, eti kwenda sehemu zenye taa! Hakuna wakala aliyekuwa anahoji. Baada ya zoezi lakuhesabu mawakala walikuwa wanatia saini kwenye karatasi za matokeo ambayo yalikuwa yameandikwa loosely kiasi kwamba nakala waliyokuwa wanapewa baadhi ya mawakala ilikuwa haionyeshi chochote, na hakuna aliyegoma kupokea! Mbaya zaidi ni kuwa mawakala baada ya kuhesabu kura katika vituo vingi walitimua zao home, wakiacha mabox ya kura na wasimamizi wa vituo wakisubiri magari ya halmashauri yaje kupitia.
Mawakala wengi waliondoka na nakala za matokeo walizopewa kwenda nazo makwao, hivyo kumfanya mgombea ubunge na wasaidizi wake wategemee zile zilizokuwa zinatoka kwa wasimamizi peke yake wakati wa kujumlisha. Cha kusikitisha zaidi ni kuwa kwa vile vituoa ambavyo CHADEMA haikuwa na mawakala na walitegemea wa CUF, hawakupewa nakala za matokeo kutoka vituoni (hadi leo)
Katika mazingira kama hayo jamani wanaCHADEMA, tunaweza kweli kuilaumu CCM kwa kutuibia? Na hapa nilipo ni mjini, ambapo pamoja na mapungufu yote hayo Dr Slaa aliibuka na zaidi ya 35% ya kura zilizotangazwa na NEC! Ni katika eneo ambalo CHADEMA tulifanikiwa kuwa na wagombea udiwani kweye zaidi ya 60% ya kata zake. Imagine kuwa yapo majimbo mengi ambayo kwanza ni remote, pili hatukuwa na wagombea ubunge na hata kwingine walikuweko lakini wagombea udiwani hawakuweko.
Kwa maoni yangu naamini hata hizi 26% CCM wametuachia, nadhani hawakuamua tu kuzipunguza, wangeweza kuzipunguza sana tu bila ya yeyote kuwapinga kwa ushahidi.
Mi nadhani huu ndio wakati wa CHADEMA kujipanga. CHADEMA wamepata kura (kwa mujibu wa NEC) zaidi ya mil 2. Hii ina maana kuwa kulikuwa na wapiga kura zaidi ya mil 2 ambao wanaiunga mkono CHADEMA. Hivi kweli kutoka kwa hawa watu wote tutashindwa kupata watu 52,000 kuwa mawakala katika vituo vya kupigia kura. Mi naamini wapo watanzania wengi sana ambao wapo tayari kujitolea kwa hiari yao wenyewe, kulinda kura zao, na naamini tunaweza kujipanga na kuwa na mawakala zaidi ya hata watano katika kila kitu (kwa kutumia vyama vingine), kuwa na waratibu zaidi ya hata 10 katika kila jimbo watakaokuwa wanafuatilia kwa karibu zoezi la kupiga kura na baadae watakaoshirikiana kupata jumla ya kura na kuwa na matokeo ya jumla moja kwa moja kutoka vituoni, kabla ya kusubiri kwenda kwa mkurugenzi.
Tatizo ni pale tutakapoamini kuwa wapo watu waliopo kwa ajili ya kufanya hizi organisation. Ki ukweli ndugu zangu, hakuna mtu wa kufanya haya. Sio Slaa, wala Mnyika wa Zito wala Mbowe. Ni sisi wenyewe. Kuna kila umuhimu wa kila mmoja wetu kujisikia yupo responsible na kuhakikisha mambo yanakuwa sawa katika eneo lake alilopo, kama sio jimbo basi hata katika kata yake. Mi nadhani makao makuu wanatakiwa tu kuagiza ongozi za wilaya, ziandae mipango mikakati thabiti ya kila jimbo, ikionyesha mipanglio ya nini kitafanyika kusuka na kuimarisha mitandao ya ushindi katika kila jimbo na kila kata.
Tunafahamu kuwa katika baadhi ya maeneo CHADEMA haina uongozi kabisa au ina uongozi dhaifu (baadhi ya wilaya, hata mikoa). Kwa yale maeneo ambayo hamna uongozi kabisa inaweza kuwa rahisi kwa watu kujitolea na kuwasiliana na makao makuu. Ugumu kidigo upo yale maeneo ambayo yana uongozi dhaifu. Hapa busara inatakiwa itumike sana kwa sababu hatua zozote inabidi zichukuliwe chini au kwa kushirikisha na uongozi uliopo. Sometimes baadhi ya viongozi wanakuwa wazito kiutendaji na ukiwaandama sana wanahisi kuwa unataka kuwanyang'anya madaraka yao. Kwenyemaeneo kama hayo tuwe makini...