Tusiokuwa na Ajira Soma Hapa

Tusiokuwa na Ajira Soma Hapa

mwanazuoni2

Member
Joined
Mar 29, 2014
Posts
13
Reaction score
10
Ndugu zangu tatizo la ajira tanzania sasa hivi limekuwa kubwa sana inaeza tangazwa nafasi moja waka-apply watu alfu mbili. Sasa mimi nilikuwa na wazo kwa nini tusianzishe maandamano ya wasiokuwa na ajira especially sie tuliopo Dar-es-salaam ili serikali na sector binafsi zipate pressure ya kutusikiliza na tuone tunatatua vp ili suala.

Tukikaa kimya umri unaenda huo. Ili bomu la ajira ndio muda muafaka kulipuka.

Nawasilisha
 
unaamini katika malcolm X badala ya Martine Luther king..?

mimi nakataa hoja kwa kuangalia side effects za maandamano.

jambo la msingi hasa ambalo litakiwa kufanywa hapa nchini ni kuunda bodi maalum hasa ambayo ingeweza kusimamia tatizo la ajira kwa vijana.

mifumo ningi ni mibovu sana, kwanini uwekewe kigezo cha working experience wakati ndio kwanza unatoka chuoni? hili nalo ni jambo la msingi hasa la kuwekewa mjadala kupitia vyombo mbali mbali vya habari, kwa njia ya amani tu na si maandamano!

halafu tukija katika masomo mbali mbali ya ngazi ya vyuo vikuu, kuna masomo yakisomwa inakuwa ngumu sana ajira kupatikana, si serikalini wala kwa sekta zisizo za serikali, je huko nako tulazimishe kuajiriwa wakati tumelazimisha kusoma wenyewe? tena wengine walipewa ushauri kabisa.. bado wakaenda huko??

siamini katika maandamano, utengenezaji wa ajira utawezekana tu endapo serikali yetu itatatua kwanza mfumo wa elmu nchini, endapo masomo ya kujitegemea nayo yatarudishwa, tatizo litapunguzwa kwa kiasi chake..
 
mimi nadhani ipo haja ya kuanzishwa kwa mjadala mkubwa wa kitaifa kujadili tatizo la ajira! mjadala huu uhusishe watu wa kada mbali mbali
 
Bwana Excel nakusalimu Sir. Vp tpdc?
 
Last edited by a moderator:
dah mkuu bom ndio unataka kuli-detonate?,hii serikali si ifanye hivi hii nchi si ina ardhi kubwa kwanini sasa vijana tusiandikishwe pale wizanarani au kwa wakuu wa wilaya halafu tukapewe ardhi huko tukalime kama enzi za ujamaa miaka ile ya vijiji vya ujamaa!
(In 1973, a policy of forced villagisation was pursued under Operation Vijiji in order to promote collective farming.[5])
 
Bwana Excel nakusalimu Sir. Vp tpdc?
salama mkuu.. kunani tena huko? lols!

mkuu mi mwenyewe muhanga wa tatizo la ajira! usione naandika hapa ukadhani niko control room benki kuu, NO!

niko street nasaka ajira kama wewe ndugu!
 
Nayaheshimu mawazo yako,japo tunaweza tukawa tunatofautiana kimtazamo for some extent,siamini katika kuandamana maana nadhani haitasaidia sana,solution ni hii hapa: Ili serikali iweze kutatua tatizo la ajira kwa kiasi fulani(si chote) lazima iweke mazingira mazuri ya FOREIGN DIRECT INVESTMENT,hii ni concept ya kiuchumi,lakini naweza nikaielezea kwa mfano rahisi kama ifuatavyo: Watu kutoka may be Sweden wanakuja kuwekeza katika nchi yetu mradi flani kama ni benki n.k,hii itasaidia kuwapa watu ajira japo sio wote,kwani nafasi na uwezo wa serikali kuajiri ni mdogo tofauti na wanaohtaji hizo ajira,tazama mashirika na benki za wawekezaji toka nje jinsi zinavyosaidia kupunguza tatizo la ajira kwa nchi zinazoendelea ikiwemo na TZ,japo tatizo halijaisha lakini kwa kiasi fulani inasaidia...............so kwa maoni yangu kuandamana sio sahihi sana!
 
Mie natamani tuungane tujikite kwenye kilimo na hapo ndipo serikali itatusikia,tuwe na mbinu mbadala kujiajiri kuliko kulia na ajira na waliopo kwenye ajira hawataki kutoka.
Hakika nawaambia bila kuwa na umoja miaka itakatika bila kufanya lolote. Kwanini tusiungane?
Mie binafsi sijawahi kuajiriwa na sifikirii kwa maana najua hawataweza kunilipa zaidi ya nipatacho sasa ila nataka kuunganisha nguvu kujitanua zaidi na kuwapa wengine ujasiri na fursa kuangalia mbadala zaidi ya ajira rasmi
 
Maandamano ndio solution ya kutupa huo mjadala mpana
kwani lazima Dar-es-salaam?
Mlisoama ili muje kuajiriwa na iwapo Serikali ikishindwa kuwaajiri ndiomuigome kwa maandamano.
tafuteni ajira Binafsi huko Magole -Dakawa kulikovunjika daraja la Dodoma - Moro ipo ajira ya kupigilia Mahema
kuna mashamba ya kulima vitunguu Lumuma
Sisi tulisoma Mwl akakimbia kufika mwisho wa ubao sasa hivi tumejiajiri kuuza karanga mradi mkono uende kinywani
MY TAKE
Hakuna haja ya Mgomo tena kuufanyia DSM kwa wenzenu waliobahatika kuendesha ma-Vogue hizo ni Godfather
ninyi ingieni kivingine MUNGU ataonesha njia.
 
kwani lazima Dar-es-salaam?
Mlisoama ili muje kuajiriwa na iwapo Serikali ikishindwa kuwaajiri ndiomuigome kwa maandamano.
tafuteni ajira Binafsi huko Magole -Dakawa kulikovunjika daraja la Dodoma - Moro ipo ajira ya kupigilia Mahema
kuna mashamba ya kulima vitunguu Lumuma
Sisi tulisoma Mwl akakimbia kufika mwisho wa ubao sasa hivi tumejiajiri kuuza karanga mradi mkono uende kinywani
MY TAKE
Hakuna haja ya Mgomo tena kuufanyia DSM kwa wenzenu waliobahatika kuendesha ma-Vogue hizo ni Godfather
ninyi ingieni kivingine MUNGU ataonesha njia.
Mkuu saruti kwako nakuunga mkono 100%
 
Mie natamani tuungane tujikite kwenye kilimo na hapo ndipo serikali itatusikia,tuwe na mbinu mbadala kujiajiri kuliko kulia na ajira na waliopo kwenye ajira hawataki kutoka.
Hakika nawaambia bila kuwa na umoja miaka itakatika bila kufanya lolote. Kwanini tusiungane?
Mie binafsi sijawahi kuajiriwa na sifikirii kwa maana najua hawataweza kunilipa zaidi ya nipatacho sasa ila nataka kuunganisha nguvu kujitanua zaidi na kuwapa wengine ujasiri na fursa kuangalia mbadala zaidi ya ajira rasmi

you sound wise mkuu,tujielekeze huko!
 
Nyie mnaosema kilimo mnakijua au mnasema tu,kwa kilimo chetu hiki cha kutegemea mvua ambazo hazieleweki zitanyesha lini si utalia.Mi sina hamu na hicho kilimo nimepoteza 1.5m kuandaa shamba,kununua mbegu matokeo yake mvua zimekataa ikawa imekula kwangu.
 
chagua ccm utapata ajira ya kugawa T-shirt, kanga na KAPELO. Over. Hadi miaka mitano ajira inajirudia tena. mwakani watawapa kazi kisimamia kura. over.
 
Mkuu saruti kwako nakuunga mkono 100%
Nashukuru Mkuu Mimi yalinipata hayo ya kuisubiri Serikali inipe kazi
na leo nimekutana na hii thread tuwape na wenzetu
https://www.jamiiforums.com/habari-...osa-hili-kubwa-linalogharimu-maisha-yako.html
Kama hujafanikiwa kama wenzako walivyofanikiwa huenda hujajua ni kitu gani unachofanya kwenye maisha yako. Huenda hujajua ni kitu gani cha kipekee unachoweza kufanya na ukafanikiwa sana. Na kwa asilimia kubwa huenda unaiga maisha ya watu wengine.
Jilinganishe na wewe mwenyewe
.
 
Vijana wajiajiri' unajiajiri kivip kwanza ndo unashindwa hata kununua sabuni. Hawa wazee ambao wa ajira huko serikali miaka zaidi ya 20 wameshindwa kujiari kwa mishahara yao ila aliyetoka juz chuo ajiajiri hii kweli. Au wanaongea bz wanauhuru wa kuongea. Kama tanzania ingekuwa na watu wenye destur ya kujiajira serikali ingetafuta wafanya kazi. Sasa wazee wanatakakufia ofisin alaf kijana ajiajiri. Waache kaz wajiajiri kama wanaona ndio furusa. Hawez kujiajir kama huna mtaji la sivyo utaishia kuwa na presha.
 
Mie natamani tuungane tujikite kwenye kilimo na hapo ndipo serikali itatusikia,tuwe na mbinu mbadala kujiajiri kuliko kulia na ajira na waliopo kwenye ajira hawataki kutoka.
Hakika nawaambia bila kuwa na umoja miaka itakatika bila kufanya lolote. Kwanini tusiungane?
Mie binafsi sijawahi kuajiriwa na sifikirii kwa maana najua hawataweza kunilipa zaidi ya nipatacho sasa ila nataka kuunganisha nguvu kujitanua zaidi na kuwapa wengine ujasiri na fursa kuangalia mbadala zaidi ya ajira rasmi

Mkuu unalima wapi,au umeanza mchakato huo tayari ......
 
Back
Top Bottom