chakii
JF-Expert Member
- Sep 15, 2013
- 19,666
- 22,674
Habari wanaJamvi.
Tatizo la ajira limekuwa likishika kasi kila kukicha huku jitihada za Serikali zikionekana waziwazi kugonga mwamba.
Wasomi wanaongezeka kila siku huku hakuna mfumo ambao utawasaidia kupata ajira ya Uhakika, inafikia kufanya kazi ambayo huna ujuzi nayo ilimradi mkono uende kinywani maana umri nao unakwenda.
Miaka michache ijayo nchi yetu tutakuwa na idadi kubwa ya watu wasiokuwa na ajira na hii itarudisha sana maendeleo ya nchi nyuma sana maana nguvu kazi kubwa itakuwa vijiweni na katika shughuli za kiuhalifu.
Naomba kupitia huu uzi tujadiliane namna ya kutatua tatizo hili ambalo hata viongozi wetu wa kisiasa wamediriki kuliita BOMU linalosubiria kulipuka.
Naamini wapo wengi watakaofaidika na michango itakayotolewa hapa na hatimaye tutakuwa tumeisaidia jamii yetu.
Karibuni.
Tatizo la ajira limekuwa likishika kasi kila kukicha huku jitihada za Serikali zikionekana waziwazi kugonga mwamba.
Wasomi wanaongezeka kila siku huku hakuna mfumo ambao utawasaidia kupata ajira ya Uhakika, inafikia kufanya kazi ambayo huna ujuzi nayo ilimradi mkono uende kinywani maana umri nao unakwenda.
Miaka michache ijayo nchi yetu tutakuwa na idadi kubwa ya watu wasiokuwa na ajira na hii itarudisha sana maendeleo ya nchi nyuma sana maana nguvu kazi kubwa itakuwa vijiweni na katika shughuli za kiuhalifu.
Naomba kupitia huu uzi tujadiliane namna ya kutatua tatizo hili ambalo hata viongozi wetu wa kisiasa wamediriki kuliita BOMU linalosubiria kulipuka.
Naamini wapo wengi watakaofaidika na michango itakayotolewa hapa na hatimaye tutakuwa tumeisaidia jamii yetu.
Karibuni.