Interest
JF-Expert Member
- Apr 11, 2015
- 3,434
- 7,055
Nimekumbuka mbali. Tusichekane.
Nikiwa na umri mdogo, nilikuwa nasikiliza sana vipindi vya redio kabla ya ujio wa televisheni na mapinduzi yake. Huko nikadevelep interest na media lakini zaidi nikavutiwa na kuwa DJ.
Mbele mbele kidogo, interest ikabadilika. Nikaongeza na kusoma sana magazeti, hivyo nikawa mtu wa redio na magazeti. TV haikuwahi kuniteka sana hata ilipokuja.
Nikaachana na kupenda U-DJ nikahamia kutamani kuwa Mwandishi kwa sababu nilikuwa nikisoma sana makala na kufuatilia habari zote.
Siku hazigandi, masomoni kuelekea Chuo Kikuu machaguo yakaongezeka kiasi cha kunivuruga kidogo. Nikawa mtumiaji sana wa internet ambako nikakutana na vitu vingi sana sana. Ilifikia hatua nikawa sijui kipi naweza kufanya kwa sababu sikupataga nafasi ya kupractise chochote kati ya vile ambavyo niliona vinanivutia.
Nikajikagua, kwenye uchaguzi wa kozi nikajikuta nimeangukia Masscom with Public Relations. Huko nikaelewa vizuri ni kitu gani naweza kufanya na ndicho nafanya mpaka sasa.
Stadi nzuri za kuwasiliana na kushawishi zimenipa nafasi ya kufanya kazi kwa ubora na utofauti kila ninapokuwepo. Zaidi ya yote nafurahia kufanya hivyo. Nachukulia ni kipaji na taaluma.
Wewe una kipaji gani? Unakitumia?
Nikiwa na umri mdogo, nilikuwa nasikiliza sana vipindi vya redio kabla ya ujio wa televisheni na mapinduzi yake. Huko nikadevelep interest na media lakini zaidi nikavutiwa na kuwa DJ.
Mbele mbele kidogo, interest ikabadilika. Nikaongeza na kusoma sana magazeti, hivyo nikawa mtu wa redio na magazeti. TV haikuwahi kuniteka sana hata ilipokuja.
Nikaachana na kupenda U-DJ nikahamia kutamani kuwa Mwandishi kwa sababu nilikuwa nikisoma sana makala na kufuatilia habari zote.
Siku hazigandi, masomoni kuelekea Chuo Kikuu machaguo yakaongezeka kiasi cha kunivuruga kidogo. Nikawa mtumiaji sana wa internet ambako nikakutana na vitu vingi sana sana. Ilifikia hatua nikawa sijui kipi naweza kufanya kwa sababu sikupataga nafasi ya kupractise chochote kati ya vile ambavyo niliona vinanivutia.
Nikajikagua, kwenye uchaguzi wa kozi nikajikuta nimeangukia Masscom with Public Relations. Huko nikaelewa vizuri ni kitu gani naweza kufanya na ndicho nafanya mpaka sasa.
Stadi nzuri za kuwasiliana na kushawishi zimenipa nafasi ya kufanya kazi kwa ubora na utofauti kila ninapokuwepo. Zaidi ya yote nafurahia kufanya hivyo. Nachukulia ni kipaji na taaluma.
Wewe una kipaji gani? Unakitumia?