Tusifurahie anguko la CUF, hasa Zanzibar

Tusifurahie anguko la CUF, hasa Zanzibar

Kashaijabutege

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2010
Posts
2,696
Reaction score
740
Ndugu wana JF

Mimi binafsi si mwanachama wa chama cha CUF, lakini nimekuwa nafarijika sana jinsi chama hicho kilivyoibana CCM visiwani Zanzibar mpaka kufikia hatua ya kugawana madaraka. Tukubali au tukatae, ukweli unabaki kuwa CUF kimejenga historia katika visiwa hivyo.

Kwangu mimi, adui namba 1, 2 na 3 wa Tanzania kwa sasa ni CCM. Mgawanyiko wa CUF ni furaha zaidi kwa CCM; ikiwezekana, CCM kiko tayari kufadhili mgawanyiko huo. Nguvu ya CUF Zanzibar imekuwa ni kero kwa CCM; kama nguvu ya CHADEMA inavyoanza kuwa kero kwa CCM huku bara. Mgawanyiko unaoendelea CUF baadhi yetu tunaufurahia kana kwamba utaishia CUF tu. Ni mkakati thabiti. Umepangwa. Baada ya CUF kufa au kupungua nguvu Zanzibar, nani atafuata?

Kila mpenda maendeleo na demokrasia, asifurahie kifo cha CUF, hasa Zanzibar, na zaidi Pemba.

Mimi nasema ukweli, sipendi CUF ikose nguvu Zanzibar.
 
kianguke tu....
kama kiongozi anaweza sema wameshindwa uzini kwa sababu kuna wakristo wengi?
hakifai.................
 
CUF ina wanasiasa wanaotia shaka kuhusu uwepo wa Tanzania. Ni kama wanafagilia kuona Tanzania inapotea. Why do we have to trust them? Na kama kuanguka sababu imekuwa nini? Let them rest in peace
 
Hapana mkuu.From my heart kuliko CUF its much better CCM.Haiwezekani kiongozi mkuu wa chama anasema waziwazi wameshindwa uchaguzi kwa sababu ya Ukristo.Mtu huyo ukimpa mamlaka atawanyonga hao wakristo asiowapenda na anaodhani ni adui wa chama chake.CUF is disaster in our country
 
Ndugu wana JF

Mimi binafsi si mwanachama wa chama cha CUF, lakini nimekuwa nafarijika sana jinsi chama hicho kilivyoibana CCM visiwani Zanzibar mpaka kufikia hatua ya kugawana madaraka. Tukubali au tukatae, ukweli unabaki kuwa CUF kimejenga historia katika visiwa hivyo.

Kwangu mimi, adui namba 1, 2 na 3 wa Tanzania kwa sasa ni CCM. Mgawanyiko wa CUF ni furaha zaidi kwa CCM; ikiwezekana, CCM kiko tayari kufadhili mgawanyiko huo. Nguvu ya CUF Zanzibar imekuwa ni kero kwa CCM; kama nguvu ya CHADEMA inavyoanza kuwa kero kwa CCM huku bara. Mgawanyiko unaoendelea CUF baadhi yetu tunaufurahia kana kwamba utaishia CUF tu. Ni mkakati thabiti. Umepangwa. Baada ya CUF kufa au kupungua nguvu Zanzibar, nani atafuata?

Kila mpenda maendeleo na demokrasia, asifurahie kifo cha CUF, hasa Zanzibar, na zaidi Pemba.

Mimi nasema ukweli, sipendi CUF ikose nguvu Zanzibar.

Tatizo la CUF ni UBAGUZI, ukitaja kujenga historia visiwani hilo halipingiki lakini lazima ujue hiyohiyo historia ndio imewabeba kuweza kudumisha upinzani Zanzibar. Siasa za visiwa vya Zanzibar na Pemba ni za KIHISTORIA na hadi sasa zipo lakini majina ya washikadau yamebadilika. HIZBU na AFROSHIRAZ = CUF na CCM respectively.
 
Hayo ni mawazo ya mtu mmoja.
Ndugu yangu Idd Amini! wewe huijui Cuf. Anaijua ni Jussa aliyesema ukiristo ni tatizo kwa wao kushinda!siku akishindwa jimbo lenye waislamu wengi atasema ni kwa sababu kuna weusi wengi, kama alivyosema msemaji mmoja hapo juu. Hiki chama hakitaki tanzania hata kilipoanzishwa kiliitwa Zanzibar United Front walibadili jina wakaita cuf kwa sababu sheria hairuhusu chama cha upande mmoja. Nakuasa utoke huko kama wewe si sultani!!cuf ni chama cha masultani!!!!!watakuvua gamba kama walivyofanya kwa wamatumbi wakina Hamad na Doyo, shauri yako.
 
acha cuf ife, lipumba anakuja kuhitimisha mazishi
 
CUf itakufa huku bara siyo Zanzibar. HR hana wafuasi wa kuitishia CUF ktk ngome yake Pemba na baadhi ya maeneo ya Unguja.
 
Nadhani hii thread inawahusu zaidi waislamu.
Source: Ismail Jusa na Shaweji Keto.
 
CUF ipo na itaendelea kuwepo! Uhai wa CUF hautegemei Molemo, VINEGA, au CHADEMA! Hili kundi halijawahi kuitakia mema CUF hata siku moja kwenye uhai wake! Hawa ndio waliomleta KIKWETE madarakani kwa kudai chaguo la mungu. Sasa wameamua kumleta padre kabisa! Hilo nalo litashindwa! Wanao hubiri CUF kufa ni maadui wa jadi wa CUF ambao tunawajua! Amini naawambia CDM itakufa kwanza kabla ya CUF! I can bet my life on it'
 
CUF ipo na itaendelea kuwepo! Uhai wa CUF hautegemei Molemo, VINEGA, au CHADEMA! Hili kundi halijawahi kuitakia mema CUF hata siku moja kwenye uhai wake! Hawa ndio waliomleta KIKWETE madarakani kwa kudai chaguo la mungu. Sasa wameamua kumleta padre kabisa! Hilo nalo litashindwa! Wanao hubiri CUF kufa ni maadui wa jadi wa CUF ambao tunawajua! Amini naawambia CDM itakufa kwanza kabla ya CUF! I can bet my life on it'

dalili ya mvua ni...............................................
 
CUF ipo na itaendelea kuwepo! Uhai wa CUF hautegemei Molemo, VINEGA, au CHADEMA! Hili kundi halijawahi kuitakia mema CUF hata siku moja kwenye uhai wake! Hawa ndio waliomleta KIKWETE madarakani kwa kudai chaguo la mungu. Sasa wameamua kumleta padre kabisa! Hilo nalo litashindwa! Wanao hubiri CUF kufa ni maadui wa jadi wa CUF ambao tunawajua! Amini naawambia CDM itakufa kwanza kabla ya CUF! I can bet my life on it'

Jussa: CUF imeshindwa uzini kwa sababu ya Ukristo.
 
CUF ipo na itaendelea kuwepo! Uhai wa CUF hautegemei Molemo, VINEGA, au CHADEMA! Hili kundi halijawahi kuitakia mema CUF hata siku moja kwenye uhai wake! Hawa ndio waliomleta KIKWETE madarakani kwa kudai chaguo la mungu. Sasa wameamua kumleta padre kabisa! Hilo nalo litashindwa! Wanao hubiri CUF kufa ni maadui wa jadi wa CUF ambao tunawajua! Amini naawambia CDM itakufa kwanza kabla ya CUF! I can bet my life on it'

abdalah unanifurahishaga na ndoto zako?

kujua maehemu anaepelekwa makaburini atafufuka na mtu mzima afe huo ni unabii.
 
CUF ina wanasiasa wanaotia shaka kuhusu uwepo wa Tanzania. Ni kama wanafagilia kuona TANZANIA inapotea. Why do we have to trust them? Na kama kuanguka sababu imekuwa nini? Let them rest in peace

Kwanini hili neno TANZANIA munalipenda sana nyinyi Watanganyika na munakosa amani pindi mukilisikia linahatarishiwa amani!! Kwa nini musiwe na ndoto ya kuiona Jamhuri ya Watu wa Tanganyika kama wanavyotamani Wazanzibari siku moja waishuhudie Jamhuri ya watu wa Zanzibar. Nini kimewasibu wenzetu?
 
Kwanini hili neno TANZANIA munalipenda sana nyinyi Watanganyika na munakosa amani pindi mukilisikia linahatarishiwa amani!! Kwa nini musiwe na ndoto ya kuiona Jamhuri ya Watu wa Tanganyika kama wanavyotamani Wazanzibari siku moja waishuhudie Jamhuri ya watu wa Zanzibar. Nini kimewasibu wenzetu?

Ndugu Mpemba Mbishi kwa kweli hata mimi huwa nawashangaa sana hawa watanganyika wenzangu wanaokerwa kuona wazanzibari wakidai haki za taifa lao la Zanzibar.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom