NJOGHOMILE
JF-Expert Member
- Jun 11, 2017
- 657
- 1,868
Mtu yupo kwenye utumishi wa umma kwa miaka 13, wenzake walioingia kwenye utumishi pamoja naye, tayari wana maisha yao. Huyu ndugu hamna alilolifanya, yaani hamna jambo lolote la maendeleo. Sijui salary anapelekaga wapi hata kama anaishi mjini, wenzio nao wanaishi humo mjini kama yeye ila wao wana nyumba, usafiri, familia(ingawa na huyu ndugu naye ana Familia lakini kwa 99% ni mke tu ndio kama Baba wa Familia)
Jamaa sasa hivi anakimbizana na namba(yrs) kuelekea 40 kwenye umri ambao huwa tunaambiwa ndio umri unatakiwa uwe ushaanza maisha!
Tabia yake inayokera ni kuomba pesa(sio kukopa, ni kuomba labda tuseme Chawa, maana Chawa ananyonya, huku anamuacha aliyemnyonya akiathirika) kutoka kwa ndugu, asipopewa anakasirika na kuzua ugomvi anaona ndugu hawamtendei haki, huyu ni mtu mzima ndio yuko hivi.
Ana mambo mengi ya hovyo kabisa ambayo hayafai kuwa kwa mtu mzima kama yeye, ila anasikitisha.
Kwa mtu wa namna hii mnadili naye vipi...
Jamaa sasa hivi anakimbizana na namba(yrs) kuelekea 40 kwenye umri ambao huwa tunaambiwa ndio umri unatakiwa uwe ushaanza maisha!
Tabia yake inayokera ni kuomba pesa(sio kukopa, ni kuomba labda tuseme Chawa, maana Chawa ananyonya, huku anamuacha aliyemnyonya akiathirika) kutoka kwa ndugu, asipopewa anakasirika na kuzua ugomvi anaona ndugu hawamtendei haki, huyu ni mtu mzima ndio yuko hivi.
Ana mambo mengi ya hovyo kabisa ambayo hayafai kuwa kwa mtu mzima kama yeye, ila anasikitisha.
Kwa mtu wa namna hii mnadili naye vipi...