Uchaguzi 2020 Tundu Lissu na mwamko mpya kiushawishi

MTAZAMO

JF-Expert Member
Feb 8, 2011
19,643
33,432
Wakuu,

Kampeni za uchaguzi zinaendelea na kwasababu ya mabadiliko makubwa ya kiushawishi ya Tundu Lissu yanayomfanya ajipatie mashabiki kwa kasi ambayo wengi (ikiwemo mimi) hatukutegemea, nimeona niandike machache kwanini anafanikiwa;

1) Lissu alianza vibaya kampeni kwa hotuba zake kujaa hoja za kiharakati ambazo haziongezi kura. Mashambulizi binafsi kwa mgombea wa CCM yalijaa jeuri isiyojenga wala kuongeza kura hivyo kuonekana na umma kama mwanaharakati zaidi ya amri jeshi mkuu mtarajiwa.

2) Hoja namba moja ndio kiini cha Lissu kujirekebisha na kubadili upepo wa kampeni. Lissu akaanza kuacha kumzungumzia sana mgombea wa CCM na kujikita kwenye shida za watu.

3) Chadema wametafiti na kutambua maeneo ambayo hayajafanyiwa kazi na kujikita huko kuliko kuponda tu miradi ambayo hoja yao imekuwa haieleweki na wananchi wengi. Sasa Lissu anazungumza habari za bei ya Cement, kupandisha mishahara, Fao la kujitoa n.k

4) Lissu ameanza kuheshimu vyombo vya dola na hata leo amewasifia. Hii ni mbinu ya kuwachota kisaikolojia askari na watumishi wengine ili wapate ushirikiano wao kikamilifu. Nafikiri hii itazidi kumuongezea wafuasi maana anajipambanua kama Amri Jeshi mkuu mtarajiwa.

5) Pamoja na ukubwa wa CCM lakini uchaguzi huu wana tatizo kubwa kupangua hoja kwenye maeneo ambayo hawakufanya vizuri. Kwanza wanaonesha hawajui vision ya mgombea wao toka alipoingia madarakani. JPM amefanya kazi nzuri sana lakini kuna maeneo hakufanya vizuri na lazima wajipange kutoa majibu ya wazi maana Chadema wamejikita huko.

6) Kwa ujumla tulitegemea kampeni zitazotawaliwa na CCM kutokana na upinzani kuwa nusu kaputi kwa muda mrefu lakini Lissu amebadili upepo na kufanya tushuhudie moja ya uchaguzi ambao hoja ndio zitazotawala na kutoa fursa kwa wananchi kuamua yupi atawafaa.

7) Pia mnyonge mnyongeni haki yake apewe. JPM anakwenda kuandika historia ya kuendesha uchaguzi kistaarabu bila vurugu tulizoshuhudia chaguzi zilizopita. Kwasababu wengi tunasahau lakini chaguzi zilizopita ziligubikwa na mengi. Pamoja na mapungufu machache lakini kampeni zinakwenda vyema na tuendelee kuomba hali ibaki hivi hadi mwisho.

Hakika Tundu A. Lissu amebadili upepo na kuleta ladha halisi ya kampeni za ushindani kihoja.

Asanteni,
MTAZAMO.
 
Uchaguzi wa kistaarabu kivipi na haujafanyika? Ndiyo kampeni sasa hivi na CCM na Magufuli wamepigwa na upepo wa kisulisuli na hawakutegemea kuwa Magufuli anachukiwa kiasi hiki mpaka kanda ya Ziwa ambayo ndiyo ilimwokoa uchaguzi uliopita?

Huu uchaguzi unaweza kuwa ndiyo wenye vurugu kuliko nyingine zote kwa sababu Magufuli anajua kabisa yuko kwenye hali mbaya na hawezi kushinda kwa kura huku wananchi wakiwa wameamua kuwa liwalo na liwe lakini kipindi hiki CCM ifikie mwisho.
 
Uchaguzi wa kistaarabu kivipi na haujafanyika? Ndiyo kampeni sasa hivi na CCM na Magufuli wamepigwa na upepo wa kisulisuli na hawakutegemea kuwa Magufuli anachukiwa kiasi hiki mpaka kanda ya Ziwa ambayo ndiyo ilimwokoa uchaguzi uliopita? Huu uchaguzi unaweza kuwa ndiyo wenye vurugu kuliko nyingine zote kwa sababu Magufuli anajua kabisa yuko kwenye hali mbaya na hawezi kushinda kwa kura huku wananchi wakiwa wameamua kuwa liwalo na liwe lakini kipindi hiki CCM ifikie mwisho.

Hakuna cha vurugu wala nini maana Magufuli atashinda tu
 
Uchaguzi wa kistaarabu kivipi na haujafanyika? Ndiyo kampeni sasa hivi na CCM na Magufuli wamepigwa na upepo wa kisulisuli na hawakutegemea kuwa Magufuli anachukiwa kiasi hiki mpaka kanda ya Ziwa ambayo ndiyo ilimwokoa uchaguzi uliopita? Huu uchaguzi unaweza kuwa ndiyo wenye vurugu kuliko nyingine zote kwa sababu Magufuli anajua kabisa yuko kwenye hali mbaya na hawezi kushinda kwa kura huku wananchi wakiwa wameamua kuwa liwalo na liwe lakini kipindi hiki CCM ifikie mwisho.
Magufuli hana hali mbaya bali ushindani umeongezeka kitu ambacho ni afya kwa Taifa letu.
 
Vyombo vya dola sasa rasmi vimepewa commitment ya Raisi Mtarajiwa wa Tanzania 2020- 2025 kuwa hawatapoteza kazi zao wala vyeo vyao

Kwa hili namshauri ndugu Magufuli apaki tu vitu vyake kujiandaa kurudi chato baada ya Uchaguzi

Lissu is another level🙌
 
Hakuna cha vurugu wala nini maana Magufuli atashinda tuuu
120277806_724486211614343_7270274407021162463_n.jpg

Hiiiiiiiiii
 
Kura zikipigwa leo atashinda ila kasi ya Lissu ni tishio na hasa angle ya hoja zake za hivi karibuni. Mambo kama fao la kujitoa, nyongeza za mishahara, bei ya Cement n.k inagusa wananchi moja kwa moja.
Hoja za Lissu zimejikita ktk kutoa elimu tena kwa mifano inayowazunguka wananchi eneo lao wanaloishi, ukimsikia anazungumza mpaka unamasika, binafsi namuona kupitia social media like youtube ila ninamasika sana, hoja zinaniamsha toka usingizini, sasa sipati picha kwa wananchi walio live ktk mkutano hamasa wanayopata
 
Huna lolote mtoa mada. Kwa hiyo wewe ulitaka aongee kila kitu siku moja? Au siku ya kwanza?

Mambo ya kuongelea Ni mengi Sana asingeweza kuyaeleza yote. Mambo yanaenda kwa mpango, nabado ataongea mambo mazuri na makubwa huko mbele.

Sema naona unajiandaa kisaikolojia tu. Baada ya kuona mtu wako anawekwa uchi,na Nini kitamfika.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom