Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,842
- 31,073
Kutokana na taarifa iliyotolewa asubuhi hii na shirika la utangazaji la BBC, amenukuliwa mwanasiasa maarufu wa Chama cha Chadema, Tundu Lissu, akisema kuwa hivi sasa ameshatoka hospitalini na anatarajia kurejea nchini wakati wowote kuanzia sasa
Ikumbukwe kuwa Tundu Lissu alinusurika kifo baada ya kushambuliwa kwa risasi zisizopungua 30, mwezi September mwaka jana huko jijini Dodoma na watu wasiojulikana
Amekuwa akitibiwa nje ya nchi jijini Nairobi na baadaye nchini Ubelgiji kwa takribani miezi 11 hivi sasa
Alipoulizwa na mtangazaji Zuhura Yunus, kuhusu usalama wake akirejea nchini Tanzania kwa sasa, mwanasiasa huyo alijibu kuwa ni kweli analazimika kuchukua tahadhari kubwa sana ya usalama wake atakaporejea nchini kwa kuwa wale waliotaka kumwua hadi leo hawajapatikana
Akiongelea hali ya kisiasa hapa nchini, alijibu kuwa wapinzani nchini Tanzania, hususani wa chama kikuu cha upinzani nchni cha Chadema, kwa sasa wanafanya kazi zao katika mazingira magumu sana ambayo hayajawahi kutokea tangu turejee katika mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, kwa kuwa viongozi wakuu wote wa Chadema wanasumbuliwa na kesi zisizo kuwa na mwisho karibu kila siku katika Mahakama zetu nchini, ambapo inawapa wakati mgumu sana kuwatumikia wananchi wao waliowachagua katika majimbo yao
Mwenyezi Mungu mjalie na umkinge na watesi wake Tundu Lissu, ambaye ndiye shujaa wa kisiasa nchini Tanzania hivi sasa
Ikumbukwe kuwa Tundu Lissu alinusurika kifo baada ya kushambuliwa kwa risasi zisizopungua 30, mwezi September mwaka jana huko jijini Dodoma na watu wasiojulikana
Amekuwa akitibiwa nje ya nchi jijini Nairobi na baadaye nchini Ubelgiji kwa takribani miezi 11 hivi sasa
Alipoulizwa na mtangazaji Zuhura Yunus, kuhusu usalama wake akirejea nchini Tanzania kwa sasa, mwanasiasa huyo alijibu kuwa ni kweli analazimika kuchukua tahadhari kubwa sana ya usalama wake atakaporejea nchini kwa kuwa wale waliotaka kumwua hadi leo hawajapatikana
Akiongelea hali ya kisiasa hapa nchini, alijibu kuwa wapinzani nchini Tanzania, hususani wa chama kikuu cha upinzani nchni cha Chadema, kwa sasa wanafanya kazi zao katika mazingira magumu sana ambayo hayajawahi kutokea tangu turejee katika mfumo wa vyama vingi mwaka 1992, kwa kuwa viongozi wakuu wote wa Chadema wanasumbuliwa na kesi zisizo kuwa na mwisho karibu kila siku katika Mahakama zetu nchini, ambapo inawapa wakati mgumu sana kuwatumikia wananchi wao waliowachagua katika majimbo yao
Mwenyezi Mungu mjalie na umkinge na watesi wake Tundu Lissu, ambaye ndiye shujaa wa kisiasa nchini Tanzania hivi sasa