Makamu Mwenyekiti wa Chadema Tundu Lissu akiwa Mkoani Kagera, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika leo, amemjibu Kinana aliyewatuhumu Viongozi waandamizi wa CHADEMA kukosa shukrani kwa Rais Samia Suluhu Hasani aliyewafutia kesi.
Lissu amesema, hawawezi kushukuru kwa kufutiwa kesi za uwongo ambazo Rais mwenyewe amewahi kukiri hadharani kuwa zilikuwa za uwongo.
"Nakufungulia kesi ya uwongo, nakutesa, nakuweka gerezani, Mwenyekiti amekaa gerezani miezi minane, ameachiwa bure mlitaka apige magoti kushukuru?.."
“Sisi ukitufunga bure TUTAKUSEMA, ukituachia baada ya kutufunga bure TUTAKUSEMA, ukiiba TUTAKUSEMA, ukigawa nchi yetu kwa wageni TUTAKUSEMA, na tutakusema mchana kweupe, sisi hatuhongeki, kama mlifikiri mnatuachia kama hongo, hiyo haipo..." Tundu Lissu.
Huyo ndiye Lissu ‘White is White, Black is Black’.
Lissu amesema, hawawezi kushukuru kwa kufutiwa kesi za uwongo ambazo Rais mwenyewe amewahi kukiri hadharani kuwa zilikuwa za uwongo.
"Nakufungulia kesi ya uwongo, nakutesa, nakuweka gerezani, Mwenyekiti amekaa gerezani miezi minane, ameachiwa bure mlitaka apige magoti kushukuru?.."
“Sisi ukitufunga bure TUTAKUSEMA, ukituachia baada ya kutufunga bure TUTAKUSEMA, ukiiba TUTAKUSEMA, ukigawa nchi yetu kwa wageni TUTAKUSEMA, na tutakusema mchana kweupe, sisi hatuhongeki, kama mlifikiri mnatuachia kama hongo, hiyo haipo..." Tundu Lissu.
Huyo ndiye Lissu ‘White is White, Black is Black’.