Tundu Lissu apambana dakika 125

Tundu Lissu apambana dakika 125

Kibo10

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
11,278
Reaction score
8,868
Tundu Lissu juzi alitumia dakika 125 kupinga muswada wa Sheria ya Usimamizi wa Maafa wakati Bunge lilipokaa kama kamati kupitisha vipengele.

Lissu, ambaye kitaaluma ni mwanasheria, alikuwa na kazi ngumu ya kupambana na Naibu Waziri wa Sheria, Mwanasheria Mkuu na baadhi ya wabunge wa CCM waliokuwa wakijaribu kusaidia kupitishwa kwa muswada ambao hata hivyo ulikwama kutokana na idadi ndogo ya wabunge waliokuwa ukumbini.

amoja na uwingi huo wa wapinzani wake, Lissu hakuonekana kukata tamaa wala kuingia hasira zaidi ya kumwambia Mwanasheria Mkuu, George Masaju, “stoop!” kutokana na kuchukua jukumu la kulishauri Bunge, kitendo ambacho Lissu alisema kinamkera kwa kuwa AG ni mshauri wa Serikali na si Bunge.

Lissu, ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chadema na kaimu kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, alipinga vifungu vyote 44 vya muswada huo, akisema kuwa unamuondolea mamlaka Rais ya kutangaza hali ya hatari, sheria mpya kudurufishwa bila ya kuwa na upya wowote na kwamba inavunja Katiba ya nchi.

Mvutano huo ulianza saa 12:00 jioni, lakini ulishika kasi kuanzia saa 1:25 hadi 3:25 usiku baada ya Bunge zima kukaa kama kamati kwa ajili ya kupitisha kufungu kimoja kimoja cha muswada huo, huku Lissu akisimama mara 19 kupinga kupitishwa kwa vifungu hivyo, akieleza kasoro zake na kushauri jinsi vinavyotakiwa kuwekwa, huku vingine akitaka vifutwe kabisa.

Kutokana na kuibuka kwa ubishani mkali na mrefu kati ya mbunge huyo, Masaju, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu wa Bunge), Jenister Mhagama, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki na Waziri wa Tamisemi, Hawa Ghasia na kusababisha muda kuyoyoma jambo lililomfanya mwenyekiti wa Bunge, Musa Azzan Zungu kulazimika kulihoji Bunge ili kupitisha vifungu husika.

Hata baadhi ya wabunge waliosimama kupinga hoja za Lissu, akiwamo mbunge wa Kilwa Kaskazini (CCM), Murtaza Mangungu, Henry Shekifu (Lushoto, CCM) na kutoa ufafanuzi wa kisheria, hawakuweza kuzipangua hoja za mbunge huyo wa Singida Mashariki.

Wakati Lissu akianza kutoa ufafanuzi wa vifungu hivyo, mbunge wa Muhambwe (NCCR-Mageuzi), Felix Mkosamali naye alikuwa ama akiunga mkono hoja za Lissu au kuja na hoja zake za kupinga muswada huo.

Hata hivyo, mbunge huyo baadaye alikata tamaa na kusema kuwa hana sababu ya kupoteza nguvu zake kutoa maoni ya msingi, mwisho wa siku yanapuuzwa na Serikali ambayo ilikataa kila pendekezo la wabunge hao.

“Nashangaa Mkosamali unakata tamaa,” alisema Lissu baada ya mbunge huyo kusema hawezi kuendelea kutoa hoja zaidi za kupinga muswada huo.

Wakati Mhagama akieleza kuwa sheria hiyo itasaidia wanaokumbwa na maafa na kukosa msaada, kutofautisha maafa na hatari ambazo kwa mujibu wa Katiba na Sheria ya Kudhibiti Maafa ya Mwaka 1990, zinatakiwa kushughulikiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano, Lissu alisema muswada huo hauna jipya.
 
Hadi raha, yaani mnyiramba huyu we acha tu.
 
Mwambieni Masaju vingine ni zaidi ya Elimu na kipaji. Lissu 1000kph
 
Hongera sna Lisu maana bla wwe huo muswada ungepita...mungu akupe maisha marefu ili uendelee kulitetea taifa letu
 
Lisu hawezi zuia serikali kufanya yake. Lisu hawezi mzuia AG kunywa maji, kwanza mwenye mamlaka ya kutafsiri na kutoa maelekezo ya kusheria na katiba kwa ujumla ni Mahakama na AGC, Lisu akatafsir katiba ya chadema. Tupa kule. Na bado changa la macho la october linaandaliwa. Wataisoma namba.
 
Back
Top Bottom