Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Taifa, Antiphas Mughwai Lissu Mahakamani leo Julai 11, 2025.
==
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Tundu Lissu amefikishwa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam leo Ijumaa Julai 11, 2025 ambapo Mahakama kuu inatarajia kutoa uamuzi wa maombi yake.
Lissu amefungua shauri la maombi mahakamani hapo akipinga uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Dar es Salaam, Kisutu kuahirisha usikilizwaji wa kesi ya kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni, ulioyotolewa Juni 2,2025.
Uamuzi huo unatarajiwa kutolewa na Jaji Elizabeth Mkwizu anayesikiliza shauri hilo, baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili yaani mawakili wa Serikali na mawakili wa Lissu.
==
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Tundu Lissu amefikishwa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam leo Ijumaa Julai 11, 2025 ambapo Mahakama kuu inatarajia kutoa uamuzi wa maombi yake.
Lissu amefungua shauri la maombi mahakamani hapo akipinga uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Dar es Salaam, Kisutu kuahirisha usikilizwaji wa kesi ya kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni, ulioyotolewa Juni 2,2025.
Uamuzi huo unatarajiwa kutolewa na Jaji Elizabeth Mkwizu anayesikiliza shauri hilo, baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili yaani mawakili wa Serikali na mawakili wa Lissu.