Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Ninaapa kwa mababu, na mizimu ya kikwetu,
Natoa leo sababu, roho yangu iwe kwatu,
Ni hili lilonisibu, kunifedhehesha utu,
Walilokula wengine, tunda hili mimi sili!
Nimepewa tunda hili, la bure sikununua,
Ni moja siyo mawili, hilo nililichukua,
Nina hamu kwelikweli, alonipa kang'amua,
Walilokula wengine, tunda hili mimi sili!
Alonipa kasifia, kasema tunda ni tamu,
Kanipa kaniambia, wengine wanalo hamu,
Hakuna alowahia, kulila tunda adhimu,
Walilokula wengine, tunda hili mimi sili!
Ndipo nikashangilia, wakijiji nina ngeke,
Tunda nililoshikia, kama vile libeneke,
Hamu nikalishakia, nyumba hima nifike,
Walilokula wengine, tunda hili mimi sili.
Kufika pale nyumbani, sahani nikaandaa,
Kulitoa mfukoni, na kisu kukiandaa,
Nikapigwa tafurani, nikabaki kushangaa,
Walilokula wengine, tunda hili mimi sili!
Tayari limeshang'atwa, upande huu na ule,
Kwa kisu lilishakatwa, ati na miye nilile,
Wanadhani wa kuletwa, kumbe nami yule yule,
Walilokula wengine, tunda hili mimi sili!
Tunda hili sasa chungu, kuonja miye sitaki,
Nataka lililolangu, si tunda la kinafiki,
La kwangu la peke yangu, lenye utamu wa haki,
Walilokula wengine tunda hili mimi sili!
Natoa leo sababu, roho yangu iwe kwatu,
Ni hili lilonisibu, kunifedhehesha utu,
Walilokula wengine, tunda hili mimi sili!
Nimepewa tunda hili, la bure sikununua,
Ni moja siyo mawili, hilo nililichukua,
Nina hamu kwelikweli, alonipa kang'amua,
Walilokula wengine, tunda hili mimi sili!
Alonipa kasifia, kasema tunda ni tamu,
Kanipa kaniambia, wengine wanalo hamu,
Hakuna alowahia, kulila tunda adhimu,
Walilokula wengine, tunda hili mimi sili!
Ndipo nikashangilia, wakijiji nina ngeke,
Tunda nililoshikia, kama vile libeneke,
Hamu nikalishakia, nyumba hima nifike,
Walilokula wengine, tunda hili mimi sili.
Kufika pale nyumbani, sahani nikaandaa,
Kulitoa mfukoni, na kisu kukiandaa,
Nikapigwa tafurani, nikabaki kushangaa,
Walilokula wengine, tunda hili mimi sili!
Tayari limeshang'atwa, upande huu na ule,
Kwa kisu lilishakatwa, ati na miye nilile,
Wanadhani wa kuletwa, kumbe nami yule yule,
Walilokula wengine, tunda hili mimi sili!
Tunda hili sasa chungu, kuonja miye sitaki,
Nataka lililolangu, si tunda la kinafiki,
La kwangu la peke yangu, lenye utamu wa haki,
Walilokula wengine tunda hili mimi sili!