Tunazo sababu nyingi kwanini tunakopa kama Nchi

Tunazo sababu nyingi kwanini tunakopa kama Nchi

Fahami Matsawili

Senior Member
Joined
Mar 8, 2018
Posts
172
Reaction score
153
Takwimu zetu zinaonesha ndani ya miaka 6 kati ya Mwaka 2014 - 2019, kama nchi tuliagiza nje bidhaa za vyakula zinatokana na sekta ya kilimo zenye thamani ya Shilingi Trilioni 7.7.

Sawa na Wastani wa shilingi Trilioni 1.3 kwa mwaka mmoja ndani ya miaka 6, bidhaa hizo kwa asilimia ni (1)Ngano 53.3% (2)Mafuta ya Kula 22.6 % (3) Sukari 16.2 % (4) Mbegu za Mahindi.

Hii ni fursa kwa Sekta binafsi katika maeneo muhimu sana kwao kuweka nguvu zaidi kuanzia mwaka huu 2022, serikali yetu ikiongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan inawekeza kwenye kujenga mazingira rafiki kwa wawekezaji kuazia sera rafiki na zinazotabirika, suala la Amani (political stability) na ujenzi wa Miundombinu kama sekta wezeshi kwa Sekta ya Viwanda ili uchumi wetu uzalishe na Ukue zaidi.

Tanzania tumesaini mkataba wa eneo huru la biashara kwa nchi za Afrika [Agreement Establishing African Continental Free Trade Area -Afcfta]

Lazima tukope pesa tumalize miradi ya kimkakati, tuweke mazingira rafiki kwa wawekezaji wa ndani na nje ili Tanzania tunufaike zaidi na soko hili la eneo huru la biashara Afrika kwa kuwa tunakwenda kupanua soko la biashara na kuhitaji wawekezaji na Wafanyabiashara.

hakuna namna tunaweza kutumia pesa za makusanyo ya ndani pekee tutawaumiza wananchi wetu na kodi zisizo rafiki na kuchelewa kufikia malengo yetu kwa wakati tuliopanga, tunahitaji kukopa pesa ili kujenga miundombinu wezeshi kwa ajili ya Uzalishaji ili kukuza Uchumi wetu.

Rais wetu Samia Suluhu Hassan anafanya kazi kubwa, ya kuhakimisha nchi yetu inakwenda mbele kimaendeleo, jukumu letu ni kumpa moyo katika jitihada kubwa anazofanya kwa ajili ya Maendeleo ya Nchi yetu.

2db41221-e837-4853-a8b0-88c3393bf351.jpg

47cd4579-726e-4e37-8860-f8bb3c9662c0.jpg
 
Ningependa kumpa unsolicited advice Rais Samia kuhusu kukopa nchi za jie. Nchi yetu ina rasilimali nyingi ambazo zinaweza kutumika kama dhamana na sisi tukakopa kutoka nchi za nje kwa masharti nafuu.

Ningekushauri kama unaweza kwa ushawishi wako uendelee kutafuta mikopo mingine yenye masharti nafuu hasa ile yenye riba SIFURI na muda mrefu wa kurejesha ; ukiipata uitumie tulipa madeni ya Kikwete aliyokopa kutoka private banks kwa riba kubwa na kutakiwa kurejeshwa Kwa muda mfupi!

Ukiweza kufanya hivyo utapunguzia mzigo kwa wananchi kutokana na madeni hayo na hakutakuwa na sababu ya kuongeza TOZO kiholela zinazowaumiza wananchi!!
 
Takwimu zetu zinaonesha ndani ya miaka 6 kati ya Mwaka 2014 - 2019, kama nchi tuliagiza nje bidhaa za vyakula zinatokana na sekta ya kilimo zenye thamani ya Shilingi Trilioni 7.7...
Mpigania tumbo katika ubora wako, akija Rais mwingine akisema kukopa sio sahihi, unaitikia hiyo verse na kuanza porojo upya. Mlichosimamia wakati wa Magufuli na mnachoongea sasa kimefanya tuwadharau ile mbaya. Yaani hapa tunaona ni kama mnajaza tu server.
 
Mie naona mapicha picha tu kilichopo kwenye kichwa changu mkopo ni mkopo ukikosea unapigwa mnada maasilimia yenu hayo ni kutoka nje ya lengo
 
Takwimu zetu zinaonesha ndani ya miaka 6 kati ya Mwaka 2014 - 2019, kama nchi tuliagiza nje bidhaa za vyakula zinatokana na sekta ya kilimo zenye thamani ya Shilingi Trilioni 7.7...
Msitudanganye mnazo kopa hazina riba.

Pesa yetu ya madafu hushuka thamani kila siku. Ukikopa usd 500m hata kama haina riba baada ya one yr sio sawa na uliyo kopa. Hizo story waambie Ccm Lumumba
 
Msitudanganye mnazo kopa hazina riba.
Pesa yetu ya madafu hushuka thamani kila siku. Ukikopa usd 500m hata kama haina riba baada ya one yr sio sawa na uliyo kopa. Hizo story waambie Ccm Lumumba

Daaaah
 
Mpigania tumbo katika ubora wako, akija Rais mwingine akisema kukopa sio sahihi, unaitikia hiyo verse na kuanza porojo upya. Mlichosimamia wakati wa Magufuli na mnachoongea sasa kimefanya tuwadharau ile mbaya. Yaani hapa tunaona ni kama mnajaza tu server.

Haaaa haaa sawa wewe mpigania nchi Kwani kipindi kilichopita tulipinga mikopo???
 
Ningependa kumpa unsolicited advice Rais Samia kuhusu kukopa nchi za jie. Nchi yetu ina rasilimali nyingi ambazo zinaweza kutumika kama dhamana na sisi tukakopa kutoka nchi za nje kwa masharti nafuu...

Umeongea Vizuri Sana Comrade, Ushauri mzuri ubarikiwe Sana, Tanzania ni yetu
 
Kwakua tozo inawaumiza wananchi tuifute kabisa tubakie na mikopo tu.

Kuifuta kabisa haiwezekani, serikali zote duniani hata Marekani na China zinaendeshwa kwa kodi, ila kodi rafiki ndiyo maana serikali inaamua kukopa na kuweka kodi za kawaida au rafiki
 
Kuifuta kabisa haiwezekani, serikali zote duniani hata Marekani na China zinaendeshwa kwa kodi, ila kodi rafiki ndiyo maana serikali inaamua kukopa na kuweka kodi za kawaida au rafiki
Kodi kwenye miamala ilikuwepo na bado ipo.

Kuweka Tozo huoni ni double Taxation??
 
Sir pls try and attend a course on development economics , and you will see what is really wrong with Tanzania, thanks
 
Back
Top Bottom