Tunawashukuru watu waliojitokeza katika uzinduzi wetu

Tunawashukuru watu waliojitokeza katika uzinduzi wetu

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2014
Posts
643
Reaction score
1,603
Nawasalimu kwa salamu ya kizalendo.

Jana chama chetu cha ACT-Wazalendo kilizindua kampeni za urais, ubunge na udiwani katika Viwanja vya Zakhem, Mbagala. Tunawashukuru Watanzania wote walijiotokeza katika mkutano wetu, waliofuatilia katika vyombo vya habari na hata kwenye mitandao ya kijamii. Hatuna cha kuwalipa zaidi ya kuwaahidi kuwatumikia kwa nguvu zote na kwa maarifa yote na kwa ushirikiano mkubwa kati ya viongozi na wananchi.

Viongozi wamesema mengi, ila kwa ufupi Watanzania wameombwa kuchagua moja miongoni mwa mambo yafuatayo; mbwembwe zinazofanywa na CCM, ulaghai unaofanywa na UKAWA, na Utu, uadilifu na Uzalendo unaohubiriwa na ACT-Wazalendo.

CCM wanachofanya sasa ni mbwembwe ambazo kimsingi hazitamsaidia Mtanzania yeyote zaidi ya kuendelea kumdidimiza, CCM ni chama ambacho kimetufikisha hapa tulipo baada ya kuacha misingi iliyoasisiwa na waanzilishi wa Taifa hili, Mwalimu Nyerere na Sheikh Karume. Mgombea wake hafai kuaminiwa hata kidogo sababu hakerwi na RUSHWA wala UFISADI unaoendelea kulitafuna taifa hili. Hakusema lolote katika kashfa ya ESCROW na hata ile ya EPA. Sasa wanatulitea mbwembwe, Watanzania tuwakatae.

UKAWA ni walaghai kwa sababu kama wapinzani waliutangazia umma orodha ya mafisadi katika viwanja vya Mwembe Yanga, Temeke. Katika orodha ya watu 11 namba tisa alikuwa Lowassa, na waliendelea kumtangaza hivyo kwa jina la ufisadi kwa miaka yote, ni mwezi uliopita tu ndipo walipoanza kumsafisha. Huu ni ulaghai kwa Watanzania na huku ni kucheza na tumaini la watanzania waliloliweka kwa vyama vya upinzani.

Imeshakua dhahiri sasa kuwa ndani ya CCM, UFISADI umekua mkubwa na sasa umezaa mtoto, na huyo ni UKAWA. Hotuba za viongozi wa UKAWA sasa zimebadilika, hawazungumzii UFISADI wala RUSHWA, na kwa kuwa huo ufisadi na rushwa ni matokeo ya uongozi mbovu wa CCM, na kwa kuwa mtuhumiwa mkubwa ufisadi ndiye mgombea wa UKAWA, hivyo basi si UKAWA na si CCM ambao wanaweza kuzungumzia na kuukemea UFISADI. Watanzania wanahitaji chama ambacho hakitauonea haya ufisadi na RUSHWA, chama ambacho kitaendeleza vita hii pale walipoishia CHADEMA, chama hicho si kingine isipokuwa ni ACT-Wazalendo.

Pamoja na kwamba chama chetu ndiyo chama pekee ambacho kina ubavu wa kuendeleza vita dhidi ya ufisadi na rushwa, lakini pia chama chetu kina ILANI, sera na misingi yake ambayo yote haya kwa pamoja yanatoa majawabu kwa matatizo yanayolikabili taifa letu. Hifadhi ya jamii, uchumi shirikishi, afya na elimu ndiyo vipaumbele vyetu. Hivyo basi na kwa sababu hiyo tunakuomba ukichague chama cha ACT-Wazalendo.

ilani.jpg

Tunaomba Watanzania mtuunge mkono.
 
Dhambi ya usaliti Haito waacha mtamficha mwanadamu Ila mungu atawaumbua sun tukutane tar 25 ucku
 
vipi mbona Zitto hajakabidhi ukuu wa chama/nuru ya chama kwa mgombea urais wa ACT kama alivyotuahidi??cc to MOTOCHINI
Nimekua na siku kama 3 singii kwa kina ktk mitandao hii ya kijamii, naingia kwa muda tu, jana nduguyangu uliuliza hili, leo pia ndio umetofautisha kidogo maana jana ulisema "mlituaminisha..." leo umesema "alivyo.." jana rafiki yangu sikuweza kuelewa nani alie kuambia ndio maana sikujibu kitu kwakuwa nasiku 3 sipo kivile mitandaoni, leo umemsema ila napata shaka kweli alisema au porojo zenu zilezile sasa nipe ukweli alisemea jf,fb,twttr,au live ktk tv, ili niingie chimbo mkuu maana hatutaki ukanjanja hapa ulaghai. TEAM WAZALENDO
 
Last edited by a moderator:
ACT wakipata hata 0.1% ya kura za urais wataingia Kwenye kitabu cha Guiness
 
Mgombea urais ambae alishindwa kwenye kura za maoni za viti maalum tena akiwa CHADEMA!!! This is an insult to Tanzanians. Do do guys really expect any sensible man would vote for her!?

In fact, huo urais wenyewe anagombea kwa kukurupushwa. Msitufanyie mzaha.
 
Jipangeni kwa msimu mwingine ujao, kwa sasa ushiriki wenu ni kama sehemu ya demokrasia. Jana bahati mbaya sana Campaign Manager wenu (sikumbuki jina lake) alianza kwa matusi sana. Watu wenye akili zetu hatuhitaji kusikiliza matusi, tunahitaji kusikia vitu vya maana pamoja na sera. ZZK Ulifanya kitu cha maana to clear it out kwa kuomba msamaha. It should be a lesson kwake, hopefully hatarudia.
 
Do not be afraid a group of lion led by a sheep.But rather be afraid a group of sheep led by a lion.
MOTOCHINI safi sana hii makitu hapo juu
 
Last edited by a moderator:
Nimekua na siku kama 3 singii kwa kina ktk mitandao hii ya kijamii, naingia kwa muda tu, jana nduguyangu uliuliza hili, leo pia ndio umetofautisha kidogo maana jana ulisema "mlituaminisha..." leo umesema "alivyo.." jana rafiki yangu sikuweza kuelewa nani alie kuambia ndio maana sikujibu kitu kwakuwa nasiku 3 sipo kivile mitandaoni, leo umemsema ila napata shaka kweli alisema au porojo zenu zilezile sasa nipe ukweli alisemea jf,fb,twttr,au live ktk tv, ili niingie chimbo mkuu maana hatutaki ukanjanja hapa ulaghai. TEAM WAZALENDO

wewe ingia chimbo muulize @Zitto au Mwigamba ulete majibu hapa.
 
Hamna kitu hapo,mnaacha kunadi sera zenu kazi kuponda wapinzani wenzenu,sijui kama mtapata hata diwani nyie,Watanzania wamewadharau sana!
 
Chama cha usaliti - alliance for cowards and traitors
 
Fanyeni siasa bila ku attack vyama vingine
hilo tu......

Mkuu siasa za Bongo (sina uzoefu na za nje) haziwezi kufanyika bila kuattack vyama hasimu!

Hatuna chama cha namna hiyo hapa Bongo.
 
Mkuu siasa za Bongo (sina uzoefu na za nje) haziwezi kufanyika bila kuattack vyama hasimu!

Hatuna chama cha namna hiyo hapa Bongo.

Siasa za Zitto zinaleta maswali mengi
anakataa posho halafu anaomba kuchangiwa
hili la posho kama atapata wabunge basi kuwaambia wakatae posho litazua bonge la mgogoro

na haijulikani hasa source ya pesa zao iko wapi
 
Back
Top Bottom