Tunataka rais aliyesoma shule za kata

Tunataka rais aliyesoma shule za kata

kaka MOLEMO wapiga kura walio wengi wamesoma shule za kata fanya upembuzi yakinifu, halafu umesahau mimi CDM si kufukuzwa nilijivua uanachama kwa maana mna poka demokrasia.
kweli nccr kuna demokrasia,yaani umeenda tu nakupewa cheo, nadhani watakuruhusu pia ugombee urais kupitia nccr 2015.
 
Kwa hiyo wengine hawana haki ya kugombea urais,kisa hawajasoma shule za kata. Kaka hapo umechemsha yaleyale ya kina zitto na january rais anayefaa ni aliyezaliwa baada ya uhuru,dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana!
 
Ndio maana mimi napenda kusema Rais ajaye lazima awe amesoma shule za kata huyu ndiye anajua machungu ya watanzania na lazima awe amesoma vyuo vya hapahapa bongo anajua machungu ya bodi ya mikopo, migomo ya vyuoni, ujinga unaoendeshwa na baadhi ya wahadhiri kuchelewesha watu kupata shahada za Uzamivu.

MTAZAMO WA KIZALENDO

Deogratius Kisandu hivi kweli kabisa unamaanisha ulichoandika hapa? #
 
Ndio maana mimi napenda kusema Rais ajaye lazima awe amesoma shule za kata huyu ndiye anajua machungu ya watanzania na lazima awe amesoma vyuo vya hapahapa bongo anajua machungu ya bodi ya mikopo, migomo ya vyuoni, ujinga unaoendeshwa na baadhi ya wahadhiri kuchelewesha watu kupata shahada za Uzamivu.

MTAZAMO WA KIZALENDO

Mkuu nasikia una shahada tena ya elimu (ualimu); hongera kwa kujikomboa na kuwa miongoni mwa "wasomi" wa inji hii ila hapo kwenye red Mkuu wangu, mimi sio mtaalamu wa lugha bali kwa uelewa wangu mdogo sijawahi kuona au kusikia mada ikianza na hayo maneno; "Ndio maana ...". Dah! una-conclude kabla hujaanza. Ulikuwa unaongea na nani kabla ya ku-post huu uzi?
 
  • Thanks
Reactions: SG8
kaka MOLEMO wapiga kura walio wengi wamesoma shule za kata fanya upembuzi yakinifu, halafu umesahau mimi CDM si kufukuzwa nilijivua uanachama kwa maana mna poka demokrasia.


Hivi ndg una uwezo gani wa kufikiri? japo umepewa cheo ambacho hakipo kikatiba jaribu kuwa na fikira ambazo zinaakisi taswira ya chama na kuacha mawazo ya kitoto kama haya. Shule za kata unazozungumzia wewe ni zipi? Mbona unashusha sana hadhi ya graduate wa chuo kikuu? mbaya zaidi umesoma Political science hapo sekuco ndo nini hiki? Jaribu kuficha mawazo mabovu, maana hata waliokuwa wanakutetea watakujua ulivyo. JIPANGE UPYA.
 
Ngoja nimpeleke back stage kidogo huyu bwana mdogo!
Bebe ngwana jisandu,oyaga ugubeha injemu jikamalaga amasala!
 
Shule za kata na hata kusoma vyuo vya ndani sio kigezo au sifa ya mtu kuwa rais wa taifa hili. Jipange vizuri kaka. Nenda bagamoyo chuo cha uongozi ukajifunze siasa kwanza then ndo ujipange upya kwa safari yako ya kisiasa coz bado una mapungufu mengi sanaaaaaaaaaaaaaaa. Kufukuzwa kwako CDM kutakugarimu sana katika ulingo wa siasa coz CDM ni chama makini na chama pekee chenye democrasia ya kweli. Kwakua ulikubali kutumika hayo ni matunda ya haki za watanzania ulizotaka kuziuza kwa uroho wa hela. Pole kaka ni ajalie?
 
Ndio maana mimi napenda kusema Rais ajaye lazima awe amesoma shule za kata huyu ndiye anajua machungu ya watanzania na lazima awe amesoma vyuo vya hapahapa bongo anajua machungu ya bodi ya mikopo, migomo ya vyuoni, ujinga unaoendeshwa na baadhi ya wahadhiri kuchelewesha watu kupata shahada za Uzamivu.

MTAZAMO WA KIZALENDO
Halafu wewe ndio mgombea Urais ajaye na Katibu mwenezi NCCR Manunuzi. JK amefanya Uaris ionekane kazi rahisi hata kwa wahuni kwa kweli. Wewe umesoma Shule hgani ya Kata? Baadae utaongeza awe amesoma Chuo Kikuu cha SEKUCO. Vijana wa siku hizi bhana, hasara tupu
 
ndio maana mimi napenda kusema rais ajaye lazima awe amesoma shule za kata huyu ndiye anajua machungu ya watanzania na lazima awe amesoma vyuo vya hapahapa bongo anajua machungu ya bodi ya mikopo, migomo ya vyuoni, ujinga unaoendeshwa na baadhi ya wahadhiri kuchelewesha watu kupata shahada za uzamivu.

Mtazamo wa kizalendo

pm 7.....
 
Back
Top Bottom