Lord Denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 23,494
- 57,869
Wiki chache zilizopita Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Tulia Ackson akihojiwa na television ya Wasafi alitetea kitendo chake cha kuvunja Katiba kwa kuruhusu Wabunge 19 waliofukuzwa na Chadema kuendelea kuwa wabunge bila kuwa na Chama bungeni huku wakilipwa mamilioni ya fedha za walipakodi masikini wa Tanzania kwa kisingizio cha kijinga na kipumbavu eti kwa sababu walikata rufaa juu ya maamuzi ya Chama chao.
Msimamo ule uliotolewa na Tulia Ackson Mwansasu sio kinyume tu na Katiba bali umethibitisha kuwa hastahili kuchukuliwa kama mtu mwenye PhD ya Sheria maana anapotosha kwa makusudi masuala ya kisheria jambo linalodhalilisha tasnia na taaluma ya Uanasheria.
Someni hapa maneno aliyowahi kutamka Jaji Mkuu wa Kenya mwaka 2022 kuhusu mtu anapokata rufaa na status ya suala lake kisheria anapokuwa amekata rufaa. Ukisoma utagundua tu kuwa Tanzania sio masikini kwa bahati mbaya ila umaskini wetu unatokana na kuwa na Viongozi wapuuzi wanaofinyanga Katiba na kujifanyia wanavyopenda bila kuwa na hofu ya kufanywa chochote na yeyote yule.
Nazidi kusikitika sana kwa Tanzania kuwa na Jeshi la Wananchi lisilojitambua ambalo limeapa kuilinda Katiba huku likiacha viongozi wapuuzi wa CCM na Serikali yao wakiisigina Katiba hiyo na kuichezea wapendavyo bila kuwa na hofu ya kufanywa chochote huku wao wakiwa wanakodoa macho tu.
Msimamo ule uliotolewa na Tulia Ackson Mwansasu sio kinyume tu na Katiba bali umethibitisha kuwa hastahili kuchukuliwa kama mtu mwenye PhD ya Sheria maana anapotosha kwa makusudi masuala ya kisheria jambo linalodhalilisha tasnia na taaluma ya Uanasheria.
Someni hapa maneno aliyowahi kutamka Jaji Mkuu wa Kenya mwaka 2022 kuhusu mtu anapokata rufaa na status ya suala lake kisheria anapokuwa amekata rufaa. Ukisoma utagundua tu kuwa Tanzania sio masikini kwa bahati mbaya ila umaskini wetu unatokana na kuwa na Viongozi wapuuzi wanaofinyanga Katiba na kujifanyia wanavyopenda bila kuwa na hofu ya kufanywa chochote na yeyote yule.
Nazidi kusikitika sana kwa Tanzania kuwa na Jeshi la Wananchi lisilojitambua ambalo limeapa kuilinda Katiba huku likiacha viongozi wapuuzi wa CCM na Serikali yao wakiisigina Katiba hiyo na kuichezea wapendavyo bila kuwa na hofu ya kufanywa chochote huku wao wakiwa wanakodoa macho tu.