Tunapenda pombe lakini pombe hii itatutia ukichaa

Tunapenda pombe lakini pombe hii itatutia ukichaa

Zero IQ

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2016
Posts
13,985
Reaction score
25,200
Pombe sio Chai tuliipenda wenyewe wacha tuinywe,

Leo pombe ile tuliyoichagua imetulewesha inatupeleka inavyotaka,

ikisema pita huku unapita ,kojoa hapa unakojoa ukijaribu kuipinga ata kidogo inakuyumbisha na kukudondosha,

Pombe ya kwanza kuinywa ilikuwa togwa tuliinywa lakini hatukulewa .

ikaja ya pili tukanywa ulanzi hii tukawa tunalewa huku tunakulana bila kujari tofauti zetu

Pombe ya tatu tukanywa safari hii tukawa tunagonga grass na mashemeji zetu japo kinafiki,

pombe ya nne ilikuwa wine hapo hatukuona aibu kuitoa nje kuinywa ata na majirani zetu huku nyimbo laini ya kusindikiza unywaji wetu zikiendelea kuburudisha nyoyo zetu

Hii pombe ya tano sasa ni Ngumu kumeza inaitwa Gongo ,pombe isiyo na staha ata kwa mashemeji,pombe isiyojua heshima ya wakwe ,

Yenyewe ukishapiga fundo moja inakupeleka inavyotaka

Pombe hii tumeiagiza ndio kwanza tupo grass ya kwanza na imejaa ndoo lakini imeshatulewesha tuko chakali hatuoni mbele wala nyuma tuko hoe hae.

Majirani zetu hawataki kusikia chochote kutuhusu wanatuona maboya kuendelea kuinywa pombe hii inayotuendesha ,

Kuna wanaosema tuiache, wengine wanajifariji kwa kusema uwenda ikapunguza makali kadri tunavyoendelea kuinywa,

na wengine wanasema tuendelee mbona kama inazoeleweka.

Tatizo la pombe hii haitabiliki unaweza kudhani kama imepoa lakini ikiamua kupanda ni kama ina kichaa lazima uwake.


IMG_20180809_155530_035.JPG
 
Hii pombe haipendi wanao 'dilute' kwa ndimu ndani ya chungu..
Na wale ambao wako nje wakijitahidi kuwakataza walevi kwa kuwapa juice ..basi pombe hii inageuka sumu na kuua wakatazaji pamoja na wanywaji kwa kutumia nguvu ya alcohol na Amira.
 
Hii pombe haipendi wanao 'dilute' ndimu ndani ya chungu..
Na wale ambao wako nje wakijitahidi kuwakataza walevi kwa kuwapa juice ..basi pombe hii inageuka sumu na kuua wakatazaji pamoja na wanywaji kwa kutumia nguvu ya alcohol na Amira.
 
Pombe sio Chai tuliipenda wenyewe wacha tuinywe,

Leo pombe ile tuliyoichagua imetulewesha inatupeleka inavyotaka,

ikisema pita huku unapita ,kojoa hapa unakojoa ukijaribu kuipinga ata kidogo inakuyumbisha na kukudondosha,

Pombe ya kwanza kuinywa ilikuwa togwa tuliinywa lakini hatukulewa .

ikaja ya pili tukanywa ulanzi hii tukawa tunalewa huku tunakulana bila kujari tofauti zetu

Pombe ya tatu tukanywa safari hii tukawa tunagonga grass na mashemeji zetu japo kinafiki,

pombe ya nne ilikuwa wine hapo hatukuona aibu kuitoa nje kuinywa ata na majirani zetu huku nyimbo laini ya kusindikiza unywaji wetu zikiendelea kuburudisha nyoyo zetu

Hii pombe ya tano sasa ni Ngumu kumeza inaitwa Gongo ,pombe isiyo na staha ata kwa mashemeji,pombe isiyojua heshima ya wakwe ,

Yenyewe ukishapiga fundo moja inakupeleka inavyotaka

Pombe hii tumeiagiza ndio kwanza tupo grass ya kwanza na imejaa ndoo lakini imeshatulewesha tuko chakali hatuoni mbele wala nyuma tuko hoe hae.

Majirani zetu hawataki kusikia chochote kutuhusu wanatuona maboya kuendelea kuinywa pombe hii inayotuendesha ,

Kuna wanaosema tuiache, wengine wanajifariji kwa kusema uwenda ikapunguza makali kadri tunavyoendelea kuinywa,

na wengine wanasema tuendelee mbona kama inazoeleweka.

Tatizo la pombe hii haitabiliki unaweza kudhani kama imepoa lakini ikiamua kupanda ni kama ina kichaa lazima uwake.


View attachment 831105

Ubunifu mzuri japo yatakayokujia sina hakika nayo sana....
 
Unajua ukishazoea kunywa wine kwenye muziki mororo inakuwa ngumu sana kuhimili gongo. Kwa sisi tulioishi maisha ya unywaji gongo miaka yote hatupati shida kabsaa kwenye hii pombe ya tano. Sana sana tunafurai kwelikweli kuona wale ambao waliokuwa wanakunywa wine kiujanja ujanja wakilalamika huku wapo nasi gongoni.
Tabu halisi hamjapata, iko njia kuja
 
Tuliamua wenyewe kunywa gongo baada ya kuona wine inachelewa kupanda kichwani
 
Naaam tumeipenda wenyewe ! Tujipange tu kuanza kufunga suruali zetu na kamba kwenye miguu... maana pombe inazidi ukali tu... inageuka Pingu
 
Ndio tatizo la pombe... mwanzoni tulikuwa tunakunywa na kufurahi, sasa hapa wengine wamezima, wengine Sana'a gums tu, yaani kiufupi tunashuhudia vituko tu. Hii Gongo hatari sana, wengine imekimbilia machoni hatuoni vizuri kama zamani, Dah!! aliyetuuzia hii Gongo sijui katuroga hapa kilabuni kuna kajamaa kananunua walevi waliokuwa chakari sijui kanataka nini mana watu wamezima hawajielewi, anyway tuombe kukuche salama, wengine mning'iniko ziada ukiisha, basi na pombe itakuwa basi. Angalizo kuna uharibifu mkubwa hapa kilabuni na uhakika kesho tutarukana wakati tulikunywa na kukesha pamoja...." Ehh mhudumu ongeza glass" kazi na dawa....
 
Halafu kuna wenzetu kila uchao wanaimba, "Nataka kulewa, lewax2, zikipanda nimwage radhi!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom