Tunaosubiri Ajira za Maafisa Ugani

Tunaosubiri Ajira za Maafisa Ugani

Mkulima na Mfugaji

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2013
Posts
1,056
Reaction score
1,867
Jamani naomba kuuliza kama kuna mwenye tetesi zozote kwamba ni lini ajira za maafisa ugani wa kilimo na mifugo zitatoka kwani mpaka sasa hatujui hatma yetu na wengine washaanza kujuta kwa nini walipoteza muda kusomea fani hii.maana serikali imeahidi itaajiri maafisa ugani pindi watakapo maliza masomo lakini sasa ni mwaka wa tatu toka tuhitimu masomo tuko mitaani.
 
Tume haijawezeshwa fungu ndo maana wapo kimya toka itoe tangazo la ajira kupitia PSRS, tuendelee kusubiria mpaka wajapo ona vema wao ku2ajiri
 
nakumbuka September 2013 walisema wanasubiri kibali...ndo sijui waliishia wapi!! me mwenyewe nshachoka na hili wizara lililojaa kujuana na selfishness.....oh! MOLA wangu! !!! nijaalie kila wepesi............
 
Kama u mkweli kuna ajira binafsi ya kuanzisha na kusimamia shamba, kuna mtu nnamjuwa anatafuta meneja wa shamba, Mkuranga. Kama u tayari ni PM nikuunganishe nae.
 
ndugu siku hizi serikali imeacha kuajiri watu moja kwa moja kwenye wizara ya kilimo mpaka uombe utumishi, pia wapo kwenye mchakato wa kuacha kuajil watu moja kwa moja ualimu na kuacha nao wawe wanaomba utumishi kama wengine, ukiachilia wa sayansi ambao watakuwa wanaajiliwa moja kwa moja mpaka wafikie 18000 wanaohitajika.
 
Back
Top Bottom