Tunaomba ushauri: Miaka 37 ana Mchumba wa miaka 19

Tunaomba ushauri: Miaka 37 ana Mchumba wa miaka 19

The Businessman

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2014
Posts
7,397
Reaction score
9,263
Wana MMU,

Kwa niaba ya familia yetu, nimekuja kuomba ushauri wa kumahauri huyu ndugu yetu Kaka Mkubwa.
Kwa kifupi ni kaka yetu mkubwa ana miaka 37 bado hajaoa na wala hana mtoto, kiuchumi anajiweza kwa kiasi fulani.
Tatizo linakuja ana mchumba "mpenzi" wa miaka 19 na yupo kidato cha 5 na yeye ndio anasema chaguo lake ni hilo.
Kama familia tunaona hilo ni tatizo kwani Msichana alishamwambia asubiri mpaka amalize chuo kikuu ndio waanze mipango ya ndoa kisha kutengeneza Familia.
Kaka yetu kwa wazazi wa bint hajulikani "rasmi" ila bint kwetu familia inamfahamu. Tumejaribu kumshauri atafute bint ambaye yupo tayari kuanza maisha hata sasa kuliko kumsubiria huyu mwanafunzi amalize chuo ndio amuoe lakini imeshindikana yeye amesimamia msimamo wake ule ule anamsubiri bint amalize chuo.
Familia tunaona hilo ni tatizo hasa ukiangalia umri wake ni mkubwa ambao kwa mwingine angekuwa tayari ana familia anayoiendesha.
Wawo kupishana huo umri sisi hatuoni tatizo, tatizo tunaloliona ni kaka kupoteza muda wa kumsubiria bint, na mnajua wachumba wa siku hizi akishafika chuo tu.....kosa.
Bado tunaendelea kumshauri.
Nawe unamshauri nini?
 
Huyo anatafuta majanga, kama ni mhehe aandae kamba
 
Mmmh inamaana kama dada atachukua kozi ya miaka mitatu tuhesabie miaka mitano mbele na kaka ako atakuwa na miaka 44 ndio ndoa, endeleeni kumshauli
 
Kwa umri aliofikia na maamuzi aliyoyachukua inaonekana kwamba huyo kaka yenu hana haraka ya ndoa wala kujenga familia..Uwenda nyie ndugu ndo mnaitaka sana familia kuliko yy..
 
Wana MMU,

Kwa niaba ya familia yetu, nimekuja kuomba ushauri wa kumahauri huyu ndugu yetu Kaka Mkubwa.
Kwa kifupi ni kaka yetu mkubwa ana miaka 37 bado hajaoa na wala hana mtoto, kiuchumi anajiweza kwa kiasi fulani.
Tatizo linakuja ana mchumba "mpenzi" wa miaka 19 na yupo kidato cha 5 na yeye ndio anasema chaguo lake ni hilo.
Kama familia tunaona hilo ni tatizo kwani Msichana alishamwambia asubiri mpaka amalize chuo kikuu ndio waanze mipango ya ndoa kisha kutengeneza Familia.
Kaka yetu kwa wazazi wa bint hajulikani "rasmi" ila bint kwetu familia inamfahamu. Tumejaribu kumshauri atafute bint ambaye yupo tayari kuanza maisha hata sasa kuliko kumsubiria huyu mwanafunzi amalize chuo ndio amuoe lakini imeshindikana yeye amesimamia msimamo wake ule ule anamsubiri bint amalize chuo.
Familia tunaona hilo ni tatizo hasa ukiangalia umri wake ni mkubwa ambao kwa mwingine angekuwa tayari ana familia anayoiendesha.
Wawo kupishana huo umri sisi hatuoni tatizo, tatizo tunaloliona ni kaka kupoteza muda wa kumsubiria bint, na mnajua wachumba wa siku hizi akishafika chuo tu.....kosa.
Bado tunaendelea kumshauri.
Nawe unamshauri nini?

Sio tatizo j3 ya wiki hii daily mail ya UK iliripoti mchungaji mmoja wa Marekani Ohio miaka 60 amemuoa girlfriend wake ambaye ana miaka 19 cha msingi makubaliano.
 
Mugabe 91 years Mke wake ni 49years Kuna Variance ya 42 years binafsi huwa sion tofauti ya umri kama ni kigezo!
 
Kama Jamaa anaona anaweza kusubiri, then mwacheni asubiri. Hamna haki ya kuingilia maamuzi yake.

ahaaaa ebu fikiria na upande mwingine. Akifika chuo tuu, totoz wanamdaka. At that tym kaka atakua 42. Yangu macho nasubiri uzi wa kulizwa kwa kaka huyo. Naona hujui makontena mpya ya first year yanavyodakwa vyuoni.
 
fikiri na upande mwingine akifika chuo tu mtotoz wanamdaka ahaaaaa nasubiri uzi wa kulizwa kwa huyo kaka at that time atakua na 42. Ahaaaa atachunwa weeeee mpaka basi mwisho atamwambia staki mzee.

Unataka kusema kuwa hakuna wanawake waaminifu na wanaojielewa?
 
Duh majanga maana yake Binti akimaliza BA Kaka yako atakuwa na miaka 41.Ikiwa Binti ataamua kusomea uDr maana yake Kaka yako atakuwa na miaka 43 - 44 hivi.Huo umri kama ni kuoa labda mjane si kipusa kibichi aisee hii si haki.Tunaendelea tuseme baada ya mwaka mmoja watajaliwa mtoto wa kwanza mtoto akimaliza darasa la saba Kaka yako atakuwa na miaka 57 kama kaajiriwa atakuwa kabakiza miaka 3 atastaafu kazi yaani mtoto akiwa form 3 Kaka yako atakuwa anakula pensheni binti atakuwa bado mbichi mbichi vijana wa mtaani itabidi wamsaidie.
 
Mbona hiyo haina shida? Namfahamu mtu ako na miaka 40 nae hana hata mtoto wa kusingiziwa na hana haraka na maisha!
 
Back
Top Bottom