engmtolera
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 5,150
- 1,437
Tunaomba ushauri ipi unadhani ina unafuu ktk unywaji wa mafuta,upatikanaji wa spare part kwa Tanzania na ipi inafaa kwa off road? mzee kastahafu inabidi apate moja ya gari hizi
1. Honda HR-V
2. Honda CR-V
======
1. Honda HR-V
2. Honda CR-V
======
Kwa asiyejua Honda basi atakwambia ni gari bomu. Honda ni kati ya magari bora na yenye uimara kushinda toyota. Naaema hivyo kutokana na uzoefu wangu maana ninaendesha CRV 2009. Nimeshawahi kuendesha CRV 2003 na 2005.
Kwa mazingira ya TZ inahitaji gari yenye nguvu. Pia salama na siyo chambo la wezi kung'oa vifaa. Honda haing'olewi vifaa.
Upande wa mafuta inatumia vizuri sana. Unaweka full tank na kuendwaha toka Dar hadi dodoma bila kupngeza mafuta njiani. Kama matumizi yako ya kawaida kwa mfano mimi ninakaa less than 3km kwenda kazini na watoto wanasoma upande mwingine nayo ni kama 2km. Basi kwa safari za wiki 2 na nusu nqtumia full tank na kipindi kingine huwa inanifikisha wiki 3 kama sina safari za kijinga na watoto wakipanda basi.
Kuhusu HRV siwezi semea ila brand ya honda inaaminika duniani kote hasa nchi za magharibi kama marekani.
Kuhusu spare hapa TZ zinapatikana ila kusema ukweli hizi gari zote nilizoendesha za honda sijawahi kununua spare hata moja. Zaidi zaidi nafanya service on time.
Ushauri mwingine kama ni gari ya kustaafu basi ni gari nzuri sana. Ila kumbuka lazima anunue gari nzuri na siyo iliyotembea kms nyingi. Picha ulizoweka ni gari za lizamani na zimechoka sana.
All the best