Samatime Magari
Senior Member
- Feb 10, 2017
- 103
- 388
Nakujuza Ili siku nyingine ukiona hii usitoe macho kama Jamaa wa Masters aliyeapply kazi ya sensa na akakosa, kabla hatujafika mbali unatakiwa kujua unleaded petrol ni petrol isiyokuwa na kiambata [additive] cha lead...
.
Hiki ni kiambata ambacho kilikuwa kinaongezwa kwenye Petrol ili kuongeza rate ya uchomaji wa mafuta [boost octane] lengo likiwa ni kuipa engine ya gari yako ufanisi zaidi...
.
Baada ya Hichi kiambata cha lead kuonekana negative impact zake ni kubwa, Kubwa kwa afya ya binaadamu, uchafuzi wa mazingira na baadhi kwenye components za magari basi ikapigwa marufuku kutumika...
.
.
So nchi nyingi duniani zikaachana nacho ingawa inasemekana kuna baadhi waliendelea, Na hapa ndo Unleaded Petrol akazaliwa nafikiri ilikua miaka ya 1975..
.
So kwa lugha rahisi na nyepesi kabisa unleaded Petrol ni petrol isiyokuwa na kiambata cha Lead, Viambata vingine ndo vikaja mfano total wana excellium, Ushapata picha ya lead na Unleaded tuendelee...
.
.
Bongo tuna aina mbili common za Petrol tuna Unleaded na Super/Premium unleaded, Nasema 2 sababu ndo mara nyingi kwenye pump za vituo vya mafuta utakuta haya majina...
.
Yani ukifika Station utakuta wameandika "unleaded" au "super" au "premium" tuanze kwa kuzitofautisha..
.
Super/Premium unleaded petrol inakua na high octane rating ambayo ni 98, Hii high rating ya octane inasababisha engine performance kuwa nzuri na kupunguza matumizi ya mafuta...
.
.
Unleaded Petrol hii inakua na octane rating ya 95, na kwenye issue ya gharama hii iko cheap kidogo, Najua utakua umejiuliza Octane ni nini ? Octane ni chemical substance iliyo ndani ya Petrol[colorless flammable hydrocarbon of the alkane]..
.
Hii inapima ubora wa mafuta Nikukumbushe ubora wa mafuta hapa ni uwezo wa kuungua kirahisi, Sasa sometime hizi classes za mafuta zinaweza kuwa mpaka tatu...
.
Kuna sehemu unaweza kuta kuna Unleaded, Premium then Super na sehemu zingine ni Unleaded na Premium tu nk, Ukiona hivi jua kwamba tofauti Zake ni kiwango cha octane kilichoko ndani kwamba Super anakua na high number of octane kuliko wenzake..
.
Utajiuliza tena nitajuaje gari yangu inahitaji kutumia mafuta gani..
.
Kuna njia mbili za kulijua hili Kwanza ukisoma manual utapewa maelekezo ya mafuta ya kutumia, Pili ukifungua mfuniko wa Tank la mafuta kwa baadhi ya gari utaona number imeandikwa..
.
.
Ukikuta 98 Jua unatakiwa kutumia Super/Premium ikiwa chini hapo basi ni Unleaded, Inshort kila engine ina specific number ya mafuta inayotakiwa kutumia na hii number utaipata kwenye Mfuniko wa tenki au manual ya gari...
.
Kwa bongo binafsi huwa sioni application ya hii kitu though kwenye vituo naona haya majina kwenye pump/mabango, Ila ukifika kituoni unawekewa mafuta tu haya mambo ya super na premium engine huwa inajua yenyewe inachopata...
.
Halafu kwa bei super bei iko juu kuliko regular unleaded petrol lakini ukifika station sidhani kama kuna bei 2 za petrol, Binafsi huwa naona bei moja tu labda kama ni vituo tofauti..
.
Ni kama tunatumia mafuta ya aina moja tu, labda kama kuna ambaye yuko jikoni atujuze zaidi. Though kuna baadhi ya wadau wanakua sensitive na kituo cha mafuta ila sio aina ya mafuta [unleaded/premium]..
.
Utasikia mwamba anasema mi mafuta bila Total siweki sehemu nyingine, Nilishawahi kuweka kituo cha mabogini gari ikasumbua, ikawa ina miss miss baadaye ikaua pump..
.
Nakumbuka hata kipindi cha nyuma kulikua na sakata la kuchakachua mafuta binafsi huwa sijui linafanyikaje Ila najua ukikutana na mafuta ya dizaini hii lazima gari ikuletee mapicha picha...
.
.
Mwenye uelewe na hili atie neno kidogo Maana naamini uchakajua wa mafuta sio Kama kuongeza maji kwenye maziwa its a complex issue kidogo
.
Baada ya hiyo tafakuri hapo juu kikubwa ninachoweza kukwambia ni kwamba Super/Premium zimetengenezwa kwa ajli ya engine zenye performance kubwa
.
Engine sensitive na mafuta na ndo maana mafuta yana octane Kubwa ambayo ina act kama resistance ya engine knocking so kama una engine zenye performance kubwa [sports car]and the likes Premium ni muhimu
.
Hata Engine sensitive na mafuta kama hizi za D4 [direct injection] unashauriwa kutumia super/premium petrol ili kuepusha matatizo Ya uchafu unaotokana na mafuta yenye kiwango kidogo that means utumie super premium
.
Kama una performance engine, mfano sport cars and the likes basi weka premium, Kwa gari ya kawaida tu [ambazo ndo majority tunazo] weka hata unleaded tu hakutakua na issue yoyote...
.
Kubwa kuliko kama we ni mzee wa i know my car ukiwa unaweka mafuta zima gari, Najua utakuwa unawaza issue ya kuzima ni kuzuia ajali ya moto Yes uko sahihi...
.
.
Ila Pia lengo Lingine ni pump isivute uchafu maana najua toka umenunua hiyo gari hujawahi safisha tank na Unapokuwa unaweka mafuta yanaingia kwa pressure kubwa kwenye tank na kuvuruga uchafu...
.
Hili likifanyika kama gari bado inaaunguruma pump inavuta uchafu ambao kiasi utapenya mpaka kwenye nozzle na baadaye italeta shida, Hapa ndo unaweza wekewa mafuta kumbe Tank lilikua tupu Ile force ya mafuta ikatibua uchafu chini then pump ikauvuta...
.
Ukatoka Kituoni mbele kidogo gari ikaanza kuleta mapicha mapicha ukasema Umepewa mafuta yaliyochakachuliwa, Kumbe issue sio mafuta ni uchafu kwenye Tank ndo umeleta shida
.
Natumaini umejifunza kitu kama jibu ni ndio Mungu akubariki, Kama unahitaji kuagiza gari Japan, UK Singapore, etc au kununua hapa nchini [showroom au mkononi] Karibu Tutafanya mchakato wako wa kupata gari kuwa salama na unaojali muda wako...
.
.
Tunafanya kazi na dealers wa nje na nchini wanaotupa gari nzuri zenye ubora na bei nzuri, Simply bofya link [Samatime Cardealers] njoo WhatsApp au ofisini Kigamboni Kisiwani na hitaji lako utakua sorted na ushauri juu.. .
.
Hata kama uko mkoani unaweza wasiliana nasi ukaagiza gari yako kwa usalama kabisa, Malipo ukafanyia huko huko [at cost] yani unatumiwa invoice then unalipa with no extra cost, Mpaka gari itapofika [30-45 days] then utaletewa au utakuja kuichuk...
.
Asante
Samatime
Get a smart car like you
Mob 0714547598