Tunalazimika sasa kuifahamu SIMBA TRUST

Tunalazimika sasa kuifahamu SIMBA TRUST

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2010
Posts
17,018
Reaction score
20,489
Kampuni hii inayomiliki hisa 50% kwenye kampuni ya PAP iliyonunua hisa zote za IPTL iliyoliingiza taifa kwenye hasara ya trilioni moja nukta nane hilo ni sehemu ya sababu ya watz kulazimika kuifahamu.

Simba trust imesajiliwa nchini Australia chini ya uwakilishi wa mwanasheria mmoja wa Australia mwenye uswahiba na Tanzania.

Taarifa toka Afrika ya Kusini zinasema Simba Trust imetumiwa na Rais Jacob Zuma kuibia madini nchini Kongo katika kipindi cha vita vya kuwafukuza M23 mashariki mwa nchi ya Kongo, Ndani ya ANC kumeibuka msuguano mkubwa watu wakihoji utajiri wa ghafla wa Rais Zuma tangu kipindi kifupi cha Vitata ya M23,

Taarifa zinasema wizi huo wa madini katika mgongo wa vita vya kimataifa ulizihusisha mamlaka za urais wa nchi tatu ambazo ni Zuma, Kabila na Kikwete, na katika kipindi hicho mpaka sasa, kampuni hiyo haijawahi kulipa kodi kwa biashara hiyo mahali popote katika nchi hizo hali inayotafsiriwa kuwa walifanya hivyo kwa "wizi".

Hapa kwetu tunaona jinsi kampuni hii inavyonufaika kwa wizi huu wa Escrow kwa mabilioni ya umma na nguvu kubwa ya wabunge wa chama tawala kutetea wizi huu. Katika taarifa ya PAC Katibu wa Rais Prosper Mbena ameshiriki kuchota mabilioni ya pesa hizi za umma,

Ikiwa Prospet Mbena amesaini barua kuruhusu pesa zitoke kwa niaba ya raisi huu ni uhusika wa rais yeye binafsi na si kama taasisi, kwani huyu Prosper ni msaidizi wake private.

Kama ingekuwa ni taasisi ya urais tulitegemea Sefue ndiyo asaini, unaweza sasa kutofautisha na kupata picha nia ya ya serikali kuchukua hatua dhidi ya uovu huu ni chafu yenye kulinda maslahi binafsi zaidi.

Tutumie mda wetu kwa maslahi mapana ya taifa letu kuitafuta Simba Trust na umiliki wake na biashara zake hii ni baada ya wale niliowataja wiki juzi kukanusha umiliki huo, ili tujue tunayepambana nae ni nani? isije kuwa ndie tuliyemtanguliza vitani..
 
Kampuni hii inayomiliki hisa 50% kwenye kampuni ya PAP iliyonunua hisa zote za IPTL iliyoliingiza taifa kwenye hasara ya trilioni moja nukta nane hilo ni sehemu ya sababu ya watz kulazimika kuifahamu.

Simba trust imesajiliwa nchini Australia chini ya uwakilishi wa mwanasheria mmoja wa Australia mwenye uswahiba na Tanzania.

Taarifa toka Afrika ya Kusini zinasema Simba Trust imetumiwa na Rais Jacob Zuma kuibia madini nchini Kongo katika kipindi cha vita vya kuwafukuza M23 mashariki mwa nchi ya Kongo, Ndani ya ANC kumeibuka msuguano mkubwa watu wakihoji utajiri wa ghafla wa Rais Zuma tangu kipindi kifupi cha Vitata ya M23,

Taarifa zinasema wizi huo wa madini katika mgongo wa vita vya kimataifa ulizihusisha mamlaka za urais wa nchi tatu ambazo ni Zuma, Kabila na Kikwete, na katika kipindi hicho mpaka sasa, kampuni hiyo haijawahi kulipa kodi kwa biashara hiyo mahali popote katika nchi hizo hali inayotafsiriwa kuwa walifanya hivyo kwa "wizi".

Hapa kwetu tunaona jinsi kampuni hii inavyonufaika kwa wizi huu wa Escrow kwa mabilioni ya umma na nguvu kubwa ya wabunge wa chama tawala kutetea wizi huu.

Tutumie mda wetu kwa maslahi mapana ya taifa letu kuitafuta Simba Trust na umiliki wake na biashara zake ili tujue tunayepambana nae ni nani? Asije kuwa ndie tuliyemtanguliza vitani...!

Mkuu ndo hii hii uliyotuambia kua inamilikiwa na Miraji na dada yake Salama? au ni nyingine maana naona kama vile leo unataka kutupeleka kwingine.
 
Hahahahahaaaaaaa!mhekaya za Yeriko. Kwani si ulituambia kuwa Simba Trust inamilikiwa na Salama Kikwete na Miraji Kikwete?
 
Mkuu ndo hii hii uliyotuambia kua inamilikiwa na Miraji na dada yake Salama? au ni nyingine maana naona kama vile leo unataka kutupeleka kwingine.
Mkuu, Yeriko ameshasahau kuwa alitudanganya kuwa hiyo kampuni ni ya familia ya Kikwete
 
Yeriko umeanza kudharauliwa. Kama umefikia hatua ya kumnadi Kagame ndani ya ardhi ya Tanzania hakika umedharaulika sana
 
Uliposema inamilikiwa na Miraji Kikwete na SALAMA KIKWETE ulikuwa unataka kumfurahisha nani?
 
Yeriko tapeli huyu, akaja na mbwembwe nyingi kuhusu mmliliki wa Simba Trust , leo tena bila aibu anakuja na swaga zile zile. Anataka kufunika uongo wake
Yeriko ni mganga njaa tu pale Kinondoni mtaa wa Ufipa
 
Lizaboni na Thatha mnajaribu sana kuokota maji.... Yamesha mwagika

Tatizo lenu bawacha mlitaka nchi iingie kwenye matatizo baada ya mipango yenu kushindwa mmebaki kupotosha na kujenga umbea.
 
Lizaboni, thatha, na gsu nawaomba myakumbuke maneno haya ya Albert Einstein "Any fool can make things bigger, more complex,and more violent. It takes a touch of a genius-and a lot of courage- to move in the opposite direction."

Jichunguzeni, kwanini mwaamua kujifanya "wapumbavu".
 
Last edited by a moderator:
Lizaboni, thatha, na gsu nawaomba myakumbuke maneno haya ya Albert Einstein "Any fool can make things bigger, more complex,and more violent. It takes a touch of a genius-and a lot of courage- to move in the opposite direction."

Jichunguzeni, kwanini mwaamua kujifanya "wapumbavu".

Asante sana mkuu wangu kwakuwafunda hawa vijana
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom