Tunalaani uwanja Chato, nchi hii upendeleo ulianza zamani Wachaga mkiongoza

Hapa JF, uependeleo na ubaguzi unalaaniwa kwa nguvu zote. Kwa vyama vya upinzani, uwanja wa Chato unatumika kama ishara ya upendeleo usiotakiwa. Hakika upendeleo ni mbaya. Tuambizane ukweli.

Ukimuacha Nyerere ktk ugawaji wa raslimali, waliofuata wote hata mawaziri wa Nyerere, walijaa upendeleo wa wazi wa makabila na dini zao. Kelele zetu kwa sasa ni kujisikia kwamba wewe haumo kwenye kundi linalopendelewa. Hatusemi yaliyofanyika kupendelea makabila yetu na dini zetu.

Elinawinga alihamisha vijana wa Mkoa wa Kilimanjaro hasa Wachaga na kuwapeleka mikoa hadi Kigoma na Tabora ili kukwepa quarter system iliyokuwa imeanzishwa na Nyerere. Wakatumia majina ya makanisani bila kuweka yale ya ukoo hadi walipomaliza shule. Leo hii hatusemi. Msuya akahamisha pesa za maendeleo na kuzipeleka kuweka umeme mkoa wa Kilimanjaro Mwanga, ikapata umeme hadi kwenye migomba na palachichi.

Wale wa kanda hiyo munafurahia hadi leo eti, mumeendelea kuliko wengine. kuweni mashujaa kulaani tabia hiyo, hata kama ni ya zamani.

Baada ya Nyerere, alikuja Mwinyi. Yeye aliegemea dini yake kwa nguvu zote maeneo ya wazi yalivamiwa kujenga misikiti na miradi ya mafuta, kwa wale wa dini yake. Zanzibar alijichukulia eneo kubwaaaa na watu wakadeka. Waliofuta ikawa kama kawa! Awamu ya 4 ndo kabisaaa! Ilikuwa Dar na Pwani basi! Familia yake na marafiki ndo ilikuwa inatafutiwa maisha bora. Hata chama ikawa ni ni yeye mtoto na mkewe!

Tusisahau akina Sumayi na mikakati ya uwanja wa Arusha. Mwandosya na Songwe, Pinda na mkoa wa katavi wenye population chini kabisa! Sitta na ofisi ya spika Urambo. Tunajuana kwa ubaguzi wetu. Na sasa kuna uhakika kwamba kuna makabila yanayoongoza kwa ubaguzi; Wachaga, wahehe, wahaya, wengine wanafuata.
Umesema vizuri lakini hujalaani hii ya awamu ya tano. Hii iko wazi wazi
 
Hapa JF, uependeleo na ubaguzi unalaaniwa kwa nguvu zote. Kwa vyama vya upinzani, uwanja wa Chato unatumika kama ishara ya upendeleo usiotakiwa. Hakika upendeleo ni mbaya. Tuambizane ukweli.

Ukimuacha Nyerere ktk ugawaji wa raslimali, waliofuata wote hata mawaziri wa Nyerere, walijaa upendeleo wa wazi wa makabila na dini zao. Kelele zetu kwa sasa ni kujisikia kwamba wewe haumo kwenye kundi linalopendelewa. Hatusemi yaliyofanyika kupendelea makabila yetu na dini zetu.

Elinawinga alihamisha vijana wa Mkoa wa Kilimanjaro hasa Wachaga na kuwapeleka mikoa hadi Kigoma na Tabora ili kukwepa quarter system iliyokuwa imeanzishwa na Nyerere. Wakatumia majina ya makanisani bila kuweka yale ya ukoo hadi walipomaliza shule. Leo hii hatusemi. Msuya akahamisha pesa za maendeleo na kuzipeleka kuweka umeme mkoa wa Kilimanjaro Mwanga, ikapata umeme hadi kwenye migomba na palachichi.

Wale wa kanda hiyo munafurahia hadi leo eti, mumeendelea kuliko wengine. kuweni mashujaa kulaani tabia hiyo, hata kama ni ya zamani.

Baada ya Nyerere, alikuja Mwinyi. Yeye aliegemea dini yake kwa nguvu zote maeneo ya wazi yalivamiwa kujenga misikiti na miradi ya mafuta, kwa wale wa dini yake. Zanzibar alijichukulia eneo kubwaaaa na watu wakadeka. Waliofuta ikawa kama kawa! Awamu ya 4 ndo kabisaaa! Ilikuwa Dar na Pwani basi! Familia yake na marafiki ndo ilikuwa inatafutiwa maisha bora. Hata chama ikawa ni ni yeye mtoto na mkewe!

Tusisahau akina Sumayi na mikakati ya uwanja wa Arusha. Mwandosya na Songwe, Pinda na mkoa wa katavi wenye population chini kabisa! Sitta na ofisi ya spika Urambo. Tunajuana kwa ubaguzi wetu. Na sasa kuna uhakika kwamba kuna makabila yanayoongoza kwa ubaguzi; Wachaga, wahehe, wahaya, wengine wanafuata.

Huu umeonyesha unasumbuliwa na wivu. Ushauri wangu kamata kamba kajinyoge kama wafanyavyo wenye wivu kama wako.
 
Mkuu huo uwanja haukutengewa bajeti na Bunge. Kilichotengwa ni bilioni 2 tu kwa ajili ya feasibility study. Nduli akachota hazina zaidi ya bilioni 50 bila idhini ya Bunge kuhakikisha uwanja unajengwa na pia kupeleka wanyama huko ili kuvutia watalii hotel yake ipate wateja. Unadhani huyo nduli asingekuwepo Ikulu uwanja huo ungejengwa? Kwa kipaumbele gani kwa Watanzania Mkuu!?

..nakubaliana na wewe 100%.

..mradi huo ni " mauza-uza" ambayo hayana faida kwa nchi kama ulivyosema.

..lakini siyo upendeleo kwa wananchi wa chato.

..sanasana amewanyima fursa ya kutatua changamoto zao kwa kutumia fedha kwenye mradi ambao hawauhitaji.
 
Sio ujinga bali ni ukweli mtupu, ujinga ni kuyafumbia macho na kutoyakosoa.
Kwahiyo tusilaana kisa huko nyuma yalitokea.? Hivi tunaishi leo au tunaishi wakati uliyopita.? Kama yalitokea huko nyumba ayahalalishi kutokea na kushangiliwa leo.
 
Sio ujinga bali ni ukweli mtupu, ujinga ni kuyafumbia macho na kutoyakosoa.

Ukiona mtu anaanza visingizio kwa kuwa hajaendelea kwa kutoa lawama kwa upande fulani, jua kuna tatizo kubwa sana katika ubongo wake
 
Waasisi wa ukabila na upendeleo ni wachaga,hata mtoto mdogo ajua hivo,awamu hii wamekosa hiyo nafasi ndo maana wanaongoza kulalamika,hata baba wa taifa aliwasema,

Acha kukariri wachaga sijui waliwafanya nini, mbona wengi wao wametapakaa mikoani na wengi ni wafanyabishara sasa walalamike kwa kipi, usidhani kila Mchaga ni mwanasiasa ila imani yao kwenye siasa ni thabiti, poleni sana
 
Ujinga mtupu
Ipe akili yako utulivu, utaona huo ujinga uliouandika
Hivi unafikiri wamisionari walikuwa wajinga? Waliona hao wachaga wana hari ya mafanikio na wanabebeka! Sehemu nyingine watu wanawaza ngono tu na ujuaji mwingi kama huyo muhutu.
Mtoa mada hizi takwimu zinakuumuza sana na hata uko palipoendelea kama dar, njombe etc ukihesabu utakuta kina Manka na Mangii. Lia tuu ila papendeni kwenu

Mwanzilishi wa thrd!! Kwa kweli umewapata watu hawa. Kwa majibu kama haya ndo utaona jinsi gani wote hawa hawana uhalali wa kukemea upendeleo. Yaani wote hawako tayari kusema upendeleo walioupata ktk makabila yao ulikuwa mbaya. Naona hata takwimu zisizohusiana na majadiliano, zinaletwa!

Jamani! Tukubali nchi hii ina watu wabaguzi nawapendeleaji tangu tupate Uhuru.Hakuanza Magufuli kama tunavyoonesha. Kama tunaona imetosha, tuseme wote kwamba tulikosea na tuache. Ukianza kujidai eti tuko hivi kwa kuwa tumesoma, sijui tunaakili ya kazi kuliko wengine, hiyo inanonesha bado tunayo hamu ya kupendelewa. Mbona hatutaki kukubali kwamba tulisoma na tuna tabia ya kupendeleana?
 
Kusoma kwa miaka ile, usiwape pongezi wazee wa kichaga, toa pongezi kwa wamisionari, hata Ukerewe ni hilo!

..unajichanganya.

..mara unasema walipendelewa na Elinawinga.

..halafu unageuka unasema walielimishwa na Wamisionari.

..sasa msimamo wako ni upi?

..siri ya kwanza ya maendeleo ya Kilimanjaro ni zao la KAHAWA.

..siri ya pili ni biashara ya mpakani baina ya Tanzania na Kenya.

..katika majirani zetu wote, Kenya ndiyo stable kiuchumi na yenye viwanda kuzidi wote.

..kuhusu elimu, chama cha ushirika kncu kilikuwa kinatoa scholarships kwenda nchi za nje kama India na kwingineko kabla hata ya uhuru wa Tanganyika.

..baada ya uhuru kncu ikafutwa na mali zake ikiwemo mashule zikataifishwa.

..Jambo lingine ambalo hujalizungumzia ni uwepo wa PRIVATE SCHOOLS nyingi kulinganisha na maeneo mengine Tz. Je, private schools nazo ni upendeleo?

NB.

..jambo lingine linalopaswa kukufikirisha ni msisitizo kwa elimu kwa watoto wa kike.

..lingine ni elimu ya ufundi. Ndugu zetu hawa walianza zamani kwa ufundi magari, ufundi welding, etc. Hilo limewasaidia kuwa vigumu kuwatumikisha kwenye umachinga wanapokuja mjini.

Cc BAK
 
Mkuu huo uwanja haukutengewa bajeti na Bunge. Kilichotengwa ni bilioni 2 tu kwa ajili ya feasibility study. Nduli akachota hazina zaidi ya bilioni 50 bila idhini ya Bunge kuhakikisha uwanja unajengwa na pia kupeleka wanyama huko ili kuvutia watalii hotel yake ipate wateja. Unadhani huyo nduli asingekuwepo Ikulu uwanja huo ungejengwa? Kwa kipaumbele gani kwa Watanzania Mkuu!?
Alichukua pesa iliyotengwa Kwa ajili ya kajunguti airport akaipeleka chato
 
Mwanzilishi wa thrd!! Kwa kweli umewapata watu hawa. Kwa majibu kama haya ndo utaona jinsi gani wote hawa hawana uhalali wa kukemea upendeleo. Yaani wote hawako tayari kusema upendeleo walioupata ktk makabila yao ulikuwa mbaya. Naona hata takwimu zisizohusiana na majadiliano, zinaletwa!
Jamani! Tukubali nchi hii ina watu wabaguzi nawapendeleaji tangu tupate Uhuru.Hakuanza Magufuli kama tunavyoonesha. Kama tunaona imetosha, tuseme wote kwamba tulikosea na tuache. Ukianza kujidai eti tuko hivi kwa kuwa tumesoma, sijui tunaakili ya kazi kuliko wengine, hiyo inanonesha bado tunayo hamu ya kupendelewa. Mbona hatutaki kukubali kwamba tulisoma na tuna tabia ya kupendeleana?

Wewe kibwengo uwe unaquote ukiwa unajibu vitu vya maana, ungeandika bila kuquote ungepungukiwa nini? Toe
 
Hivi unafikiri wamisionari walikuwa wajinga? Waliona hao wachaga wana hari ya mafanikio na wanabebeka! Sehemu nyingine watu wanawaza ngono tu na ujuaji mwingi kama huyo muhutu.
Hapa umeandika kwa hisia. Jaribu kwenda na facts kwenye nyuzi kama hizi.
 
Hii ya Chato ni mbaya! Lakini kwa nini hatuko tayari kulaani yote yaliyotokea na yanayotokea nchi hii?

Ukiamua kutetetea tuuuu hapo ndo tunasema wengi tunafurahia upendeleo unaotufikia kwa neema. Tunalazimisha kutumia hata takwimu zisizokuwepo na hasa hilo la elimu. Hapa TZ Wilaya pekee inayoweza kujivunia wasomi wa kiwango cha juu kabisa kuliko wilaya yoyote nyengine ni Ukerewe. Nasema tena Ukerewe na hiyo inafahamika. Kwa nini hawakujaa juu kote? sema jingine tu!

Kusoma kwa miaka ile, usiwape pongezi wazee wa kichaga, toa pongezi kwa wamisionari, hata Ukerewe ni hilo!

Zygot,
Wewe unataka kutuletea mitizamo hasi na finyu kama ya rafikiyo Bashite wakti wa msiba wa Reginald Mengi(rip).
Unaposema Wachaga wameendelea kwa upendeleo inaonesha jinsi ulivyo mbumbumbu wa historia ya nji hii.
Kama Rais Magufuli ameanza kupendelea Chato ili ipate maendeleo kwa vile ni kwao Rais....Katika historia ya nji hii, ni LINI TUMEWAHI KUWA NA RAIS MCHAGGA??

Wachagga ni wapiga Kazi tangu enzi za Mkolone hili hata Magufuli analijua. Hizi blabla za upendeleo wa Wachagga ni kuonesha mtu umeishiwa hoja....Tukupe pooole sana!!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Kuhusu Elinewinga (RIP mdau) umekosea. Hujatafiti kutosheleza. Cha msingi ni kwamba WATU HUJITAFUTIA MAENDELEO WENYEWE na hawapelekewi. Mifumo thabit ikiwepo husaidia EFFORTS za kujiletea maendeleo. Wapo Watanzania kama WAFUGAJI wanaozurura na nchi nzima na watoto wao wasioenda shule kulisha MIFUGO yao ambao hata ufanyeje PORI ni sehemu ya ubongo wao. Wapo wengine ambao ni WAVIVU mno licha ya kuishi kwenye maeneo yenye rutba na maji. Maisha yao ya kileo na yale ya mababu zao wa kale hayana tofauti. Priorities zao sio za kimaendeleo kama baadhi ya jamii zingine za Tanzania.
Kwa mtazamo wako mwandishi nakushauri UKAE MBALI NA UJINGA.
Hebu soma copy-paste hii ya mwanachama aliyewahi kuyasema haya siku za nyuma. Nimeifukuwa nikaiona, bahati mbaya ithrd imefungwa.

Quoting Mchunguzi, 2011
"Usiniponde mawe bure. Mwanakijiji alizungumzia ajira au nafasi za kiutawala serikalini. Hayo mambo ya kufungua bar au maduka siyo tatizo la nchi. Tunaelewa mambo kama hayo yanaweza kuwa yanatokana na tabia binafsi ya makabila. Ndo maana ma-housegirls wengi wanaonekana kutoka Iringa, Wapasua mbao wengi ni kutoka Njombe na Tabora (kuna misitu huko), Wavuvi ni wa Kigoma na Mwanza, nk. Siyo ujanja wa biashara. Mbona Uvuvi unalipa sana kule Mwanza lakini Wachagga wameshindwa? Siyo jadi. Sijachunguza wachagga kupenda biashara ya Bar ni kwa nini labda mambo ya mbege.

Kilichozungumziwa hapa ni ajira ndani ya serikali. Mimi nimeenda mbali zaidi kuonyesha kwamba kuna tabia za upendeleo wa kikabila nchi hii ndo maana nikaonyesha mambo ya NIC ya Mwaikambo, NBC ya Nsekela.

Hebu uliza Wachagga wenye umri mkubwa wakueleze walisoma wapi na kipindi gani. Utaambiwa nilisoma Tabora, Mtwara, n.k. wakati Elinawinga akiwa Waziri. Uliza makabila mengine kama yalipata nafasi ya kusoma Kilimanjaro wakati huo.

Wakati mwingine tabia hizi zinaanzia mbali ktk makuzi yetu. Mfano wangu mzuri umekuwa ni hayo unayoyaona Moshi kuwa ni mji wa biashara za wachagga tu na kuwa vigumu sana kwa makabila ya mikoa jirani wakati wachagga wanavumiliwa mikoa mingine.

Hivi karibuni nimesikia mji wa Mwanza umemchagua kijana wa kichagga kuwa mbunge, akimuondoa Antony Diallo(sp.?), msukuma. Mji wa mwanza hauna tofauti sana na Moshi na Arusha kwa ukubwa, lakini hebu fikiria kama Msukuma angegombea ubunge kupitia CHADEMA (Siyo CCM) pale mjini Moshi mambo yangekuwaje. Ni tabia ya makuzi ukizoea kusema ni sisi tu. Jamani hata Soda! Nilishafika Moshi miaka ya 2005, nambiwa hadi leo Coca cola ndo inayouzika tu kwa sababu mmiliki wa kampuni ni Mengi!

Kunakuwa na upendeleo kwa kisingizo cha kusoma sana wakati si kweli. Nawe kweli unaamini Wachagga wamesoma sana? Angalia sifa za vijana walioko TRA ambayo iliwahi kulalamikiwa bungeni. Wengi ni Form 4, 6 na walio juu wana vyeti vya CBE na IFM (vyuo vya mambo ya fedha). Kwa sifa hizo za elimu, tukikuta wachagga ni wengi tutasema ni kwa sababu wamesoma sana? Kumbuka miaka ya 1995, 96, 97 graduate walilalamika kwamba TRA haitaki wenye degree.

Unaweza ukatetea tabia hii wakati inapokupa nafasi, lakini mambo yakigeuka huwa na uchungu usiosemeka.

Tusikwepe ubaya unaotumika na kuweka sababu tamu, bandia. Tuiseme tu!"
 
Tusipojiadhari na ubaguzi,ukanda, ukabila na udini tunajichibia shimo.sisi wenyewe .Watanzania tuachane na slogans za charity begins at home Rasilimali yeyote inayopatikana sehemu yeyote yaTanzania ni mali ya watanzania wote sio ya sehemu mali hiyo inapatikana,Dhahabu ya Geita ,Gas ya Mtwara ,mrima Kirimanjaro ni mali za watanzania wote
 
Back
Top Bottom