Tunajifunza nini kuhusu kuachiwa huru kwa Mbunge kijana Bob Wine wa Uganda?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,156
Habari zilizopatikana kutoka nchini Uganda hivi leo ni kuwa Mwanamuziki maarufu nchini humo ambaye pia ni mbunge wa upinzani wa Jimbo la Kyadondo nchini huko Uganda, ameachiliwa huru baada ya kelele nyingi zilizopigwa na vikundi vya kutetea haki za kibinadamu za ndani ya nchi hiyo na kutoka Jumuia ya kimataifa

Tujikumbushe kidogo kuwa Bob Wine na wabunge wenzie 4 kutoka kambi ya upinzani, alikamatwa tarehe 14/8/2018 na kuwekwa ndani na kutakiwa kufunguliwa mashitaka katika Mahakama ya kijeshi kwa makosa ambayo serikali hiyo ya Museveni ilikuwa ikimtuhumu ya uhaini

Baada ya kuwekwa ndani na kutolewa tuhuma za kuteswa akiwa Mahabusu, ndipo vikundi mbalimbali vya kijamii vilifanya maandamano ndani ya Uganda pamoja na nchi jirani ya Kenya, kushinikiza mwanamuziki huyo aachiwe huru

Hatimaye shinikizo hilo linaelekea kuzaa matunda baada ya mwanamuziki huyo kuachiwa huru kwa dhamana na kubadilishwa kwa mashitaka yake badala ya kusikilizwa na Mahakama ya kijeshi, hivi sasa mwanamuziki na Mbunge huyo kijana atafunguliwa mashitaka katika Mahakama za kawaida za kiraia

Je sisi watanzania tunajifunza nini kwa yale yakiyotokea kwa mwanamuziki huyo kukamatwa na kutaka kufunguliwa mashitaka katika Mahakama ya kijeshi na kubadilisha hivi sasa na kumfungulia mashitaka katika Mahakama za kawaida?
 
bado hakuna cha kujifunza.
maana kushtakiwa kwake katika mahakama ya kawaida bado hakumpi nafasi ya kuwa na Uhuru wa kawaida kwani watoa hukumu bado ni wale wake japo tu sasa siyo chini ya jeshi.
 
Mleta mada acha uzushi hajaachiwa kilichofanyika ni kuwa katolewa mikononi mwa jeshi alikokuwa kashikiliwa Na kakabidhiwa polisi ili waendelee naye Na kesi zake
 
Habari zilizopatikana kutoka nchini Uganda hivi leo ni kuwa Mwanamuziki maarufu nchini humo ambaye pia ni mbunge wa upinzani wa Jimbo la Kyadondo nchini huko Uganda, ameachiliwa huru baada ya kelele nyingi zilizopigwa na vikundi vya kutetea haki za kibinadamu za ndani ya nchi hiyo na kutoka Jumuia ya kimataifa

Tujikumbushe kidogo kuwa Bob Wine na wabunge wenzie 4 kutoka kambi ya upinzani, alikamatwa tarehe 14/8/2018 na kuwekwa ndani na kutakiwa kufunguliwa mashitaka katika Mahakama ya kijeshi kwa makosa ambayo serikali hiyo ya Museveni ilikuwa ikimtuhumu ya uhaini

Baada ya kuwekwa ndani na kutolewa tuhuma za kuteswa akiwa Mahabusu, ndipo vikundi mbalimbali vya kijamii vilifanya maandamano ndani ya Uganda pamoja na nchi jirani ya Kenya, kushinikiza mwanamuziki huyo aachiwe huru

Hatimaye shinikizo hilo linaelekea kuzaa matunda baada ya mwanamuziki huyo kuachiwa huru kwa dhamana na kubadilishwa kwa mashitaka yake badala ya kusikilizwa na Mahakama ya kijeshi, hivi sasa mwanamuziki na Mbunge huyo kijana ayafunguliwa mashitaka katika Mahakama za kawaida za kiraia

Je sisi watanzania tunajifunza nini kwa yale yakiyotokea kwa mwanamuziki huyo kukamatwa na kutaka kufunguliwa mashitaka katika Mahakama ya kijeshi na kubadilisha hivi sasa na kumfungulia mashitaka katika Mahakama za kawaida?
Tuache bangi utapondaje jiwe gari la Rais hadi unavunja kioo! Hata hapa ukiponda mawe msafara wa mkuu utapigwa.
 
Mleta mada acha uzushi hajaachiwa kilichofanyika ni kuwa katolewa mikononi mwa jeshi alikokuwa kashikiliwa Na kakabidhiwa polisi ili waendelee naye Na kesi zake
Ndivyo nilivyosema kuwa katolewa kutoka Mahakama ya kijeshi na atashiitakiwa kwenye Mahakama ya kiraia
 
Hakuna uhuru hapo bado kwa mtazamo wangu, maana katoka mikononi mwa mahakama ya jeshi kakabidhiwa mikononi mwa mahakama ya kiraia, mambo bado ni yale yale tuuu. Na hakuna cha kujifunza pia hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa Watanzania Bado sana
Kwanza inahitajika Elimu ya kujitambua..Ila kwa Sasa hata tupangiwe siku za kulala na Wake zetu tutalalamika na mwisho tunaishia kusema namwachia Mungu.
 
hakuna la kujifunza..hao wajeda weshamdunga misindano ya sumu.. muda si mrefu atarest in peace
 
Nilichojifunza matumizi ya 'Hashtag' yana nguvu sana Kenya na Uganda.

Hashtag za Wabongo huko Twitter huwa hazina nguvu sijui huwa tunakosea wapi!!
 
Tunajifunza kuwa jeshi hawana mamlaka ya kufatilia kesi za watu ndio maana kakabidhiwa kwa polisi wafanye kazi yao
 
Sijui Kwanini Risasi alizopigwa Lissu hazikuistua Dunia Kama kichapo cha Huyu Jamaa alichopata
 
MLIOSAMBAZA PICHA FAKE YA BOB WINE AKIWA NA MAJERAHA USONI KOMENI KUWA MNASAMBAZA VITU MSIVYOKUWA NA UHAKIKA NAVYO. MBONA LEO MAHAKAMANI HATUJAMUONA NA JERAHA LOLOTE USONI
 
Unajifunza nini sasa au hujui kama viongozi wa upinzani ndo wamezidi kukamatwa siku ya Leo.Hizo kelele Ni za chura Tu.Labda kama angefutiwa mashitaka tungejifunza maanake ndo lengo la hizo kelele.
 
Nilichojifunza ni kuwa chadema hawana cha kufundisha watu wengine nchi zingine Ila wao ndio kutwa wana cha kujifunza kutoka nchi zingine tofauti Na CCM ambao nchi nyingi zina cha kujifunza kutoka CCM
 
Back
Top Bottom