Tunaitoaje CCM madarakani?

Nakufananisha na wale wamisri ambao walikataa kwenda nchi ya ahadi wakayakumbuka yale masufuria na nyama walizokula kule utumwani Misri kwa Pharaoh.
 
Katiba mpya ndio kila kitu .Trump mwenyewe na uzwazwa wake wote katiba inamnyoosha.
 
Ikitoka sisiemu kwa hiyo mnaweka chama gani?
Sababu ni wazi sio chadema, hawa ni majizi na wapiga dili na hawajui uongozi. Angalia wanavyoendesha chama chao kama saccos.
Zile billion 2 na ushehe nyinyi ndio mnajua sana kuzitumia ?
 
Waweke CHADEMA madarakani uendelee kulima nyanya.Tatizo nn?
 
CCM ni Tanzania na Tanzania ni CCM.
CCM ni masta wa siasa za Afrika na dunia yaani ni zaidi ya chama cha siasa.

Unataka kuiondoa halafu waongoze nani? Hawa ambao ruzuku za vyama vyao tu ni vita, wanaofukuzana kila leo, au hawa wanaosema wakipewa urais wataruhusu ushoga Tanzania????? Acha ulofa CCM for life
 
Tatizo la Tanzania ni Watanzania wenyewe msilaumu CCM wala Chadema.
 
Eti ni masta wa siasa za Africa na dunia.Wachanicheke tu,hawa hawa wenye bunge dhaifu na wanaorudisha korosho ?
 
Hakuna anayekataa kwamba wakati mwengine ccm huwa wanacheza michezo michafu,hoja hapa ukiondoa hiyo michezo michafu bado ccm ana mtaji mkubwa tu wa kura hivyo tusihishie kusema tu kuwa ccm wanashinda kwa wizi bali pia lazima tukubali kwamba pamoja na yote hayo ccm bado ina watu wengi tu wenye kuipigia kura hadi leo.
Kwa maana hiyo huwezi kusema ccm inashindika tu kirahisi isipotumia nguvu,wakati mwengine watu wameshakariri tu kuwa ccm wanaiba kura hata pale wanaposhinda kiuhalali.
 
Siipendi CHADEMA kama ambavyo siipendi CCM ingawa napata matumaini kwa baadhi ya wanaccm kufanya vizuri ingawa wamezungukwa na wachafu wasio litakia mema Taifa hili labda tupate chama kipya chenye watu wapya wenye fikra pevu kulingana na matakwa ya kidunia.
 
Ivi mm niulize kipi ni bora kutoenda kabisa kupiga kura au kwenda kupiga nimeuliza ivi ili tuwekane sawa mwaka uliopita Wa uchaguzi watu wakijitokeza kwa wingi Sana lkn mwisho wake ni matokeo kuchakachuliwa na ccm ikashinda mm naona bora kutokwenda kwani hata tukienda bado uwezo wa kulinda kula haupo
 
tatizo sisi watanzania ni waoga sana,tukisikia hata sauti ya risasi moja tu kila mmoja anasambaratika,kingine pia upinzani bado hawana mikakati inayoeleweka mfano UKAWA
Tusipende kujiita sisi watanzania kwamba ni waoga. Huo ni uongo mkubwa sana. Hata hzi nchi za kiarabu tunazozitolea mfano kwamba wanafanya mabadiliko ya uongozi kwa njia za maandano ni kwa kupitia njia mojawapo ya hizi hapa:

1. Hao viongozi wao wanakuwa wamechokwa na western powers. Hivyo western powers wanawatumia (wanawaplant) watu
wao wa kusimaimia mazoezi hayo ya kuwaondoa watu madarakani kwa njia ya maandamano.
2. Au jeshi la nchi husika linakuwa limeshachoka kuisapoti serikali iliyoko madrakani hivyo linawaandaa watu wa kuongoza hayo
maandamano bila jeshi lenyewe kuhusika moja kwa moja lakini linajitokeza mwishoni kukamilisha zoez kwa kuchukua
madaraka japo kwa kipindi kifupi cha mpito
3. Au kuna viongozi shupavu wa upinzani wasio waoga ambao wako tayari hata kufa ambao hushawishi wananchi waliochoshwa na utawala ulioko madarakani ili kuandamana kushinikiza uongozi uliopo madarakani kuachia ngazi.

* HIVYO KWA POINT NO. 3 NI KWAMBA BADO HATUNA VIONGOZI JASIRI WA KUWEZA KUSHAWISHI NA KUONGOZA
MAANDAMNO KUDAI MABADILIKO YA UONGOZI WENGI WA VIONGOZI WA UPINZANI TZ NI WACHUMIA TUMBO,

WAOGA NA WANAFIKI WAKUBWA.
 

Mkuu ni hivi sio wakati mwingine, mahali popote ccm ilipo na ushindani wa kweli ni lazima ifanye hujuma na sasa ni za wazi. Na iwapo ingekuwa inategemea kushinda kihalali tu, leo hii isingekuwepo kwani vizazi vimebadilika, hilo moja. Na sasa hivi chini ya Magu ndio kabisa ccm inafanya hujuma za wazi kwenye box la kura.

Haya ninayokumbia sijahadithiwa bali nayaona kwa macho. Hiki kinachofanyika kwa sasa sio rafu kama tulizozoea huko nyuma bali ni ushenzi na ukatili. Sasa hivi watu wanafanyiwa ukatili wa wazi, na ni lazima kumtangaza mgombea wa ccm hata kama ameshindwa kwa uwiano mkubwa wa kura. Hapo achia mbali ukiukwaji mkubwa wa sheria toka kwa wasimamizi wa uchaguzi. Yaani sasa hivi kwenda kupiga kura ni kupoteza muda kwa yale yanayofanyika kwenye box la kura.

Nguvu pekee ya ccm ni madaraka ya mwenyekiti wa ccm anayoyapata kupitia katiba yenye mapungufu ambaye mara nyingi ni rais. Rais wetu kupitia katiba hii anapata nguvu kubwa ambayo imemlimbikizia madaraka ikiwemo kuwa juu ya vyombo vya dola na sheria. Hapa anaweza kuagiza chochote hata kilicho nje ya katiba na kikafanyika. Amri hizo za nje ya sheria na katiba huitwa amri toka juu, amri hii toka juu ina nguvu kuliko sheria na katiba, na yote haya yanachangiwa na mapungufu ya katiba iliyopo. Hapa tu ndipo ilipo nguvu ya ccm na sio Zaidi. Nasisitiza iwapo ccm italogwa ikakubali kushiriki uchaguzi huru na haki huku ikitegemea kushinda kihalali, ndani ya 10yrs rais hatatoka ccm. Na hata wao hilo wanalijua.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…